SWALI LINALOWASUMBUWA WATU WA DINI,NA DUNIA

Yohane 20:28


Tomaso akajibu, akamwambia, Bwana wangu na Mungu wangu

1 Timotheo 3:16

Na bila shaka siri ya utauwa ni kuu. Mungu alidhihirishwa katika mwili.


Wakolosai 2:9

Maana katika yeye unakaa utimilifu wote wa Mungu, kwa jinsi ya kimwili.

Isaya 9:6

Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, tumepewa mtoto mwanamume; na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

Yohana 8:58

Yesu akawaambia, . . . Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

Alikuwako ulimwenguni, hata kwa yeye ulimwengu ulipata kuwako, wala ulimwengu haukum tambua. —Yohana 1:10

1 Timotheo 2:5, 6

Kwa sababu Mungu ni mmoja, na mpatanishi kati ya Mungu na wanadamu ni mmoja, Mwanadamu Kristo Yesu; ambaye alijitoa mwenyewe kuwa ukombozi kwa ajili ya wote.

Wakolosai 1:14, 15

Ambaye katika yeye tuna ukombozi, yaani, msamaha wa dhambi; naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana.

BIBLIA (MAANDIKO) NI NENO LA MUNGU — 26

Maana unabii haukuletwa po pote kwa mapenzi ya mwanadamu; bali wanadamu walinena yaliyotoka kwa Mungu, wakiongozwa na Roho Mtakatifu. —2 Petro 1:21

Luka 1:70, 77

Kama alivyosema tangu mwanzo kwa kinywa cha manabii wake watakatifu; uwajulishe watu wake wokovu, katika kusamehewa dhambi zao.

Roho ya BWANA ilinena ndani yangu, na neno lake likawa ulimini mwangu. —2 Samweli 23:2
Kumbukumbu La Torati 6:6

Na maneno haya ninayokuamuru leo, yatakuwa katika moyo wako.
2 Timotheo 3:16

Kila andiko, lenye pumzi ya Mungu, lafaa kwa mafundisho, na kwa kuwaonya watu makosa yao, na kwa kuwaongoza, na kwa kuwaadibisha katika haki.

Warumi 15:4

Kwa kuwa yote yaliyotangulia kuandikwa yaliandikwa ili kutufundisha sisi; ili kwa saburi na faraja ya maandiko tupate kuwa na tumaini.

Mathayo 22:29

Mwapotea, kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu.

Zaburi 138:2

Kwa maana umeikuza ahadi yako, kuliko jina lako lote.

YESU NDIYE NENO LA MUNGU
Ufunuo 19:13

Naye amevikwa vazi lililochovywa katika damu, na jina lake aitwa, Neno la Mungu.
Yohana 1:1, 14

Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu.
Yesu anamdhihirisha Mungu

2 Wakorintho 4:6

Kwa kuwa Mungu, aliyesema, Nuru itang’aa toka gizani, ndiye aliyeng’aa mioyoni mwetu, atupe nuru ya elimu ya utukufu wa Mungu katika uso wa Yesu Kristo.



Yohana 1:18

Hakuna mtu aliyemwona Mungu wakati wo wote; Mungu Mwana pekee aliye katika kifua cha Baba, huyu ndiye aliyemfunua.

Mungu yuanena kuptia kwa Yesu



Waebrania 1:1, 2

Mungu, ambaye alisema zamani na baba zetu katika manabii kwa sehemu nyingi na kwa njia nyingi, mwisho wa siku hizi amesema na sisi katika Mwana, aliyemweka kuwa mrithi wa yote, tena kwa yeye aliufanya ulimwengu.



Yohana 8:38

Niliyoyaona kwa Baba ndiyo niyanenayo.
 Tunasema ni neno na ni chakula,
Biblia ni chakula kwa nafsi

Ayubu 23:12

Nimeyatunza maneno ya kinywa chake zaidi ya riziki yangu.

Mathayo 4:4
Mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno litokalo katika kinywa cha Mungu.


Biblia inaangaza njia yetu
Zaburi 119:105

Neno lako ni taa ya miguu yangu, na mwanga wa njia yangu.

Kufafanusha maneno yako kwatia nuru, na kumfahamisha mjinga. —Zaburi 119:130

Yesu ni mkate kutoka mbinguni

Yohana 6:51, 48

Mimi ndimi chakula chenye uzima kilichoshuka kutoka mbinguni; mtu akila chakula hiki, ataishi milele. Na chakula nitakachotoa mimi ni mwili wangu, kwa ajili ya uzima wa ulimwengu. Mimi ndimi chakula cha uzima.

Yesu ni nuru ya ulimwengu

Yohana 8:12

Basi Yesu akawaambia tena akasema, Mimi ndimi nuru ya ulimwengu, yeye anifuataye hatakwenda gizani kamwe, bali atakuwa na nuru ya uzima.
Biblia huleta maisha yen ye mazao
Zaburi 1:2, 3

KUNA UMUHIMU GANI WA KUTUBU DHAMBI ZETU KWA MUNGU?

Yeremia 36:3


Wapate kurudi, kila mtu akaiache njia yake mbaya; nami nikawasamehe. . . dhambi yao.

Zaburi 32:5

Nalikujulisha dhambi yangu, wala sikuuficha upotovu wangu. Nalisema, Nitayakiri maasi yangu kwa BWANA, nawe ukanisamehe upotovu wa dhambi yangu.

1 Yohana 1:9

Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.

Matendo 3:19

Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe.

Kutubu kunamaanisha kugeuka kutoka dhambini pamoja na kuungama mbele za Mungu.



DHABIHU INAYOTAKIKANA KUTUPATANISHA NA MUNGU

(Dhambi ilileta utengano.)

Mambo Ya Walawi 17:11

Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.



Waebrania 9:22

Na katika Torati karibu vitu vyote husafishwa kwa damu, na pasipo kumwaga damu hakuna ondoleo



Kutoka 12:5, 13

Mwana-kondoo wenu atakuwa hana ila, mume wa mwaka mmoja. ...Na ile damu itakuwa ishara kwenu katika zile nyumba mtakazokuwamo; nami nitakapoiona ile damu, nitapita juu yenu, lisiwapate pigo lo lote likawaharibu.



Mwanzo 22:8, 13

Ibrahimu akasema, Mungu atajipatia mwana-kondoo kwa hiyo sadaka, mwanangu. . . . Ibrahimu akainua macho yake, akaangalia, na tazama, kondoo mume yuko nyuma yake, amenaswa pembe zake katika kichaka. Basi Ibrahimu akaenda akamtwaa huyo kondoo, akamtoa awe sadaka ya kuteketezwa badala ya mwanawe.



YESU NDIYE MWANA KONDOO ALIYETOLEWA NA MUNGU

Siku ya pili yake amwona Yesu anakuja kwake, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu, aichukuaye dhambi ya ulimwengu! —Yohana 1:29

Alionewa, lakini alinyenyekea, wala hakufunua kinywa chake; kama mwana-kondoo apelekwaye machinjoni, na kama vile kondoo anyamazavyo mbele yao wakatao manyoya yake; naam, hakufunua kinywa chake. —Isaya 53:7

Wala si kwa damu ya mbuzi na ndama, bali kwa damu yake mwenyewe aliingia mara moja tu katika Patakatifu, akiisha kupata ukombozi wa milele. Kadhalika Kristo naye, akiisha kutolewa sadaka mara moja azichukue dhambi za watu wengi. . . . Basi si zaidi damu yake Kristo, ambaye kwamba kwa Roho wa milele alijitoa nafsi yake kwa Mungu kuwa sadaka isiyo na mawaa, itawasafisha dhamiri zenu na matendo mafu, mpate kumwabudu Mungu aliye hai? —Waebrania 9:12,28, 14



1 Petro 1:18, 19

Nanyi mfahamu kwamba mlikombolewa si kwa vitu viharibikavyo, kwa fedha au dhahabu; bali kwa damu ya thamani, kama ya mwana-kondoo asiye na ila, asiye na waa, yaani, ya Kristo.



UKOMBOZI NI KWA MAAFIKANO TU NA MUNGU



Warumi 3:24, 25

Wanahesabiwa haki bure kwa neema yake, kwa njia ya ukombozi ulio katika Kristo Yesu; ambaye Mungu amekwisha kumweka awe upatanisho kwa njia ya imani katika damu yake.

Bali Mungu aonyesha pendo lake yeye mwenyewe kwetu sisi, kwa kuwa Kristo alikufa kwa ajili yetu, tulipokuwa tungali wenye dhambi. Basi zaidi sana tukiisha kuhesabiwa haki katika damu yake, tutaokolewa na ghadhabu kwa yeye. —Warumi 5:8,9

Hali tukijua ya kuwa mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; sisi tulimwamini Kristo Yesu. —Wagalatia 2:16

Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. —Waefeso 2:8,9

Huyo manabii wote humshuhudia, ya kwamba kwa jina lake kila amwaminiye atapata ondoleo la dhambi. —Matendo 10:43



Matendo 4:12

Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo.





KUZALIWA KWA YESU KWATANGAZWA



Luka 1:26-38

...Malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina lake Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. ...Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto mwanamume; na jina lake utamwita Yesu. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, ...na ufalme wake utakuwa hauna mwisho. Mariamu akamwambia malaika, Litakuwaje neno hili, maana sijui mume? Malaika akajibu akamwambia, Roho Mtakatifu atakujilia juu yako, na nguvu zake Aliye juu zitakufunika kama kivuli; kwa sababu hiyo hicho kitakachozaliwa kitaitwa kitakatifu, Mwana wa Mungu.... kwa kuwa hakuna neno lisilowezekana kwa Mungu. Mariamu akasema, Tazama, mimi ni mjakazi wa Bwana; na iwe kwangu kama ulivyosema. Kisha malaika akaondoka akaenda zake.

Watu tu walioingia Ulimwenguni pasipo uzao wa Mume na Mke walikuwa Adamu na Kristo. Adamu alileta dhambi katika Ulimwengu, lakini Yesu alileta ushindi juu ya dhambi.

yesu unamtambuwaje?

Wafilipi 2:6, 8

Ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho; tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.



Yohana 10:30, 36

Mimi na Baba tu umoja. Je! yeye ambaye Baba alimtakasa, akamtuma ulimwenguni, ninyi mnamwambia, Unakufuru; kwa sababu nalisema, Mimi ni Mwana wa Mungu?

Yesu Kristo, Neno la Milele, amekuwako daima. Kwa muujiza, Mungu alisababisha atungwe mimba katika tumbo la Mariamu. Kimwili anajulikana kama Mwana wa Mtu, na Kiroho anajulikana kama Mwana wa Mungu. Maandiko yanatumia neno "Mwana" kueleza uhusiano ulioko kati ya Mungu na Neno lake—Yesu Kristo.



Waebrania 10:5

Kwa hiyo ajapo . . . Lakini mwili uliniwekea tayari.

Na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo wa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu. —Warumi 1:4

KWA MTU MMOJA DHAMBI ILIINGIA ULIMWENGUNI,

Si kwamba twatosha sisi wenyewe kufikiri neno lo lote kwamba ni letu wenyewe, bali utoshelevu wetu watoka kwa Mungu aliyeumba mbingu na dunia


DHAMBI HUTUFARAKANISHA MUNGU WETU

Warumi 5:12

Kwa hiyo, kama kwa mtu mmoja dhambi iliingia ulimwenguni, na kwa dhambi hiyo mauti; na hivyo mauti ikawafikia watu wote kwa sababu wote wamefanya dhambi.

Yakobo 1:15

Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Ezekieli 18:20

Roho itendayo dhambi, ndiyo itakayokufa.

Isaya 59:2

Lakini maovu yenu yamewafarikisha ninyi na Mungu wenu, na dhambi zenu zimeuficha uso wake msiuone, hata hataki kusikia.

Mithali 11:19

Haki huelekea uzima; afuataye maovu hufuata mauti yake mwenyewe.

2 Mambo Ya Nyakati 24:20

Mungu asema hivi, Kwani ninyi kuzihalifu amri za BWANA, hata msiweze kufanikiwa? Kwa kuwa mmemwacha BWANA, yeye naye amewaacha ninyi.

1 Samweli 15:23

Kwani kuasi ni kama dhambi ya uchawi, na ukaidi ni kama ukafiri na vinyago; kwa kuwa umelikataa neno la BWANA, yeye naye amekukataa wewe.



GHADHABU YA MUNGU   IKO JUU YA DHAMBI  ZA MWANADAMU

Zaburi 7:11

Mungu ni mwamuzi mwenye haki, naam, Mungu aghadhibikaye kila siku.

Nahumu 1:3

BWANA si mwepesi wa hasira, ana uweza mwingi, wala hatamhesabia mtu mwovu kuwa hana hatia kamwe.

Wakolosai 3:6

Kwa ajili ya mambo hayo huja ghadhabu ya Mungu.

Warumi 1:18

Kwa maana ghadhabu ya Mungu imedhihirishwa kutoka mbinguni juu ya uasi wote na uovu wa wanadamu waipingao kweli kwa uovu.

Warumi 1:29-32

Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao.



HUKUMU IKO MBELE NA SAFARI YA MWANADAMU

Na kama vile watu wanavyowekewa kufa mara moja, na baada ya kufa hukumu. —Waebrania 9:27

Ufunuo 20:12, 15

Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.

Waebrania 10:31

Ni jambo la kutisha kuanguka katika mikono ya Mungu aliye hai.

Mathayo 12:36

Basi, nawaambia, Kila neno lisilo maana, watakalolinena wanadamu, watatoa hesabu ya neno hilo siku ya hukumu.

Kwa maana Mungu ataleta hukumuni kila kazi, pamoja na kila neno la sir likiwa jema au likiwa baya. —Mhubiri 12:14

Mathayo 13:49, 50

Ndivyo itakavyokuwa katika mwisho wa dunia; malaika watatokea, watawatenga waovu mbali na wenye haki, na kuwatupa katika tanuru ya moto; ndiko kutakuwako kilio na kusaga meno.



HATUWEZI KUMFICHA  MUNGU MAOVU YETU

Mithali 15:3

Macho ya BWANA yako kila mahali; yakimchunguza mbaya na mwema.

Zaburi 139:1-4

Ee BWANA, umenichunguza na kunijua. Wewe wajua kuketi kwangu na kuondoka kwangu; umelifahamu wazo langu tokea mbali. Umepepeta kwenda kwangu na kulala kwangu, umeelewa na njia zangu zote. Maana hamna neno ulimini mwangu usilolijua kabisa, BWANA.

1 Samweli 16:7

Kwakuwa BWANA haangalii kama binadamu aangaliavyo; maana wanadamu huitazama sura ya nje, bali BWANA huutazama moyo.

Zaburi 94:9

Aliyelitia sikio mahali pake asisikie? Aliyelifanya jicho asione?

Yeremia 16:17

Maana macho yangu yaziangalia njia zao zote; hawakufichwa uso wangu usiwaone, wala haukusitirika uovu wao macho yangu yasiuone.

Waebrania 4:13

Wala hakuna kiumbe kisichokuwa wazi mbele zake, lakini vitu vyote vi utupu na kufunuliwa machoni pake yeye aliye na mambo yetu.



KUGEUKA NA KUTOKA DHAMBINI KUNAHITAJIKA SANA KWA MWANADAMU,

Ezekieli 18:23

Je! mimi ninafurahia kufa kwake mtu mwovu? asema Bwana MUNGU; si afadhali kwamba aghairi, na kuiacha njia yake, akaishi?

Luka 13:3

Nawaambia, Sivyo; lakini msipotubu, ninyi nyote mtaangamia vivyo hivyo.

Mithali 28:13

Afichaye dhambi zake hatafanikiwa; bali yeye aziungamaye na kuziacha atapata rehema.

Yoeli 2:12, 13

Lakini hata sasa, asema BWANA, nirudieni mimi kwa mioyo yenu yote, na kwa kufunga, na kwa kulia, na kwa kuombolea; rarueni mioyo yenu, wala si mavazi yenu, mkamrudie BWANA, Mungu wenu; kwa maana yeye ndiye mwenye neema, amejaa huruma; si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa rehema.

Hosea 14:2

Chukueni maneno pamoja nanyi, mkamrudie BWANA; mkamwambie, Ondoa maovu yote, uyatakabali yaliyo mema.

Ayubu 33:27, 28

Yeye huimba mbele ya watu, na kusema, mimi nimefanya dhambi, yeye ameikomboa nafsi yangu isiende shimoni, an uhai wangu utautazama mwanga.



KUTUBU KUNALETA MSAMAHA

Isaya 55:6, 7

Mtafuteni BWANA, maadamu anapatikana, mwiteni, maadamu yu karibu; mtu mbaya na aache njia yake, na mtu asiye haki aache mawazo yake; na amrudie BWANA, naye atamrehemu; na arejee kwa Mungu wetu, naye atamsamehe kabisa.

Zaburi 34:18

BWANA yu karibu nao waliovunjika moyo, na waliopondeka roho huwaokoa.

KWENYE UTAKATIFU KUNA UTUKUFU WA MUNGU

Hakuna aliye mtakatifu kama BWANA; kwa maana hakuna ye yote ila wewe.


Ayubu 34:10

Mungu asidhaniwe kutenda udhalimu; wala Mwenyezi kuf anya uovu.

Isaya 6:3

Mtakatifu, Mtakatifu, Mtakatifu, ni BWANA wa majeshi; dunia yote imejaa utukufu wake.

Isaya 57:15

Maana yeye aliye juu, aliyetukuka, akaaye milele; ambaye jina lake ni Mtakatifu; asema hivi; Nakaa mimi mahali palipoinuka, palipo patakatifu.

Zaburi 145:17

BWANA ni mwenye haki katika njia zake zote, na mwenye fadhili juu ya kazi zake zote.

Marko 10:18

Hakuna aliye mwema ila mmoja, ndiye Mungu.

Ufunuo 15:4

Ni nani asiyekucha, Ee Bwana, na kulitukuza jina lako? kwa kuwa wewe peke yako u Mtakatifu.



WATU WA MUNGU NI LAZIMA WAISHI MAISHA MATAKATIFU

Yakobo 2:19, 20

Wewe waamini ya kuwa Mungu ni mmoja; watenda vema. Mashetani nao waamini na kutetemeka. Lakini wataka kujua, wewe mwanadamu usiye kitu, kwamba imani pasipo matendo haizai?

1 Yohana 2:4; 3:10

Yeye asemaye, Nimemjua, wala hazishiki amri zake, ni mwongo, wala kweli haimo ndani yake. Katika hili watoto wa Mungu ni dhahiri, na watoto wa Ibilisi nao. Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

Njia ya mtu mbaya ni chukizo kwa BWANA; bali humpenda mtu afuatiaye wema. —Mithali 15:9

Waebrania 12:14

Tafuteni kwa bidii kuwa na amani na watu wote, na huo utakatifu, ambao hapana mtu atakayemwona Bwana asipokuwa nao.

Bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote. —1 Petro 1:15

Amosi 5:14

Tafuteni mema, wala si mabaya, mpate kuishi; hivyo BWANA, Mungu wa majeshi, atakuwa pamoja nanyi, kama msemavyo.



MAMBO MUNGU ANAYOYATAKA KWAKO

Mika 6:8

Na BWANA anataka nini kwako, ila kutenda haki, na kupenda rehema, na kwenda kwa unyenyekevu na Mungu wako!

Mambo Ya Walawi 19:2

Mtakuwa watakatifu; kwa kuwa mimi BWANA, Mungu wenu, ni mtakatifu.

Luka 10:27

Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote, na kwa akili zako zote; na jirani yako kama nafsi yako.

Marko 10:19

Wazijua amri, Usiue, Usizini, Usiibe, Usishuhudie uongo, Usi danganye, Waheshimu baba yako na mama yako.

Warumi 12:2

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu.

Yoshua 1:8

Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

Marko 11:22

Mwaminini Mungu.



MAMBO MUNGU  ALIYOYATAJA ANAYOCHUKIA

Mithali 6:16-19

Kuna vitu sita anavyovichukia BWANA; naam, viko saba vilivyo chukizo kwake. Macho ya kiburi, ulimi wa uongo, na mikono imwagayo damu isiyo na hatia; moyo uwazao mawazo mabaya; miguu iliyo myepesi kukimbilia maovu; shahidi wa uongo asemaye uongo; naye apandaye mbegu za fitina kati ya ndugu.

Isaya 61:8

Maana mimi, BWANA, naipenda hukumu ya haki, nauchukia wivi na uovu.

Ufunuo 21:8

Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili.

Malaki 2:15, 16

Kwa hiyo jihadharini roho zenu; mtu awaye yote asimtende mke wa ujana wake mambo ya hiana. Maana mimi nakuchukia kuachana, asema BWANA.

Zekaria 8:17

Wala mtu wa kwenu asiwaze mabaya moyoni mwake juu ya jirani yake; wala msipende kiapo cha uongo; maana hayo yote ndiyo niyachukiayo, asema BWANA.



WATU HUPUNGUKIWA NA MATAKWA YA MUNGU,

Walakini nimewajua ninyi ya kuwa hamna upendo wa Mungu ndani yenu. —Yohana 5:42

Maana mtu awaye yote atakayeishika sheria yote, ila akajikwaa katika neno moja, amekosa juu ya yote. —Yakobo 2:10

Isaya 6:5

Ndipo niliposema, Ole wangu! kwa maana nimepotea; kwa sababu mimi ni mtu mwenye midomo michafu, nami ninakaa kati ya watu wenye midomo michafu; na macho yangu yamemwona Mfalme, BWANA wa majeshi.

Basi yeye ajuaye kutenda mema, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi. —Yakobo 4:17

Kama ilivyoandikwa, ya kwamba, hakuna mwenye haki hata mmoja. —Warumi 3:10

Warumi 3:23

Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.

1 Yohana 3:10

Mtu ye yote asiyetenda haki hatokani na Mungu, wala yeye asiyempenda ndugu yake.

Isaya 53:6

Sisi sote kama kondoo tumepotea; kila mmoja wetu amegeukia njia yake mwenyewe.

Ni nani awezaye kusimama mbele za BWANA, huyu Mungu mtakatifu? —1 Samweli 6:20



KAZI ZETU WENYEWE HAZIWEZI KUMPENDEZA MUNGU KAMA HATUJAMSHIRIKISHA,

Warumi 10:2, 3

Kwa maana nawashuhudia kwamba wana juhudi kwa ajili ya Mungu, lakini si katika maarifa. Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya Mungu, na wakitaka kuithibitisha haki yao wenyewe, hawakujitia chini ya haki ya Mungu.

Isaya 64:6

Kwa maana sisi sote tumekuwa kama mtu aliye mchafu, na matendo yetu yote ya haki yamekuwa kama nguo iliyotiwa unajisi.

Ezekieli 33:13

Nimwambiapo mwenye haki, ya kwamba hakika ataishi; kama akiitumainia haki yake, akatenda uovu, basi katika matendo yake ya haki, hata mojawapo halitakumbukwa; bali katika uovu wake alioutenda, atakufa katika uovu huo.

Warumi 8:8; 3:20

Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu. Kwa sababu hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki mbele zake kwa matendo ya sheria.

2 Wakorintho 3:5

TOFAUTI YA MIUNGU NA MUNGU MUUMBA MBINGU NA DUNIA,

Kama Abraham alivyokuwa "rafiki Wa Mungu" kwa uvumilivu na utiifu kwa Mungu, wewe pia unaweza kumjua Mungu na kupata rehema zake, amani, na baraka. Kumjua Mungu kwa uvumilivu wa kweli katika kumwamini ni ujuzi muhimu zaidi katika maisha. Ni ajabu namna gani kwamba Mungu hujidhihirisha Mwenyewe kwa wote wanao Mtafuta kwa mioyo yao yote!




Ikiwa utageuka kuiacha njia yako na kweli kujitolea kwa Mungu, Roho Wake ataishi ndani yako. Hakuna kitakacho kutenganisha na upendo Wake unapo tumainia ahadi Zake na Kumfuata kwa utiifu. Yeye atakuwa Mungu wako, nawe utakuwa hazina Yake Mwenyewe. Utagundua kwamba alikununua kwa gharama kuu, na anataka kuwa na ushirika nawe—sasa na hata milele.



Uliza Mungu akupe ufahamu unapojifunza kurasa hizi za vifungu kutoka Neno la Mungu. Mungu aliongoza watu wamchao kuandika maneno haya na kwa kimiujiza ameyahifadhi katika vizazi vyote kutoka kwa majaribio yote ya Shetani ya kuyakomesha.

______________________________________________________________

Maandiko yanayo husika katika kijitabu hiki yametolewa kutoka Biblia: Sheria (Torah), Zaburi (Zabur), maandiko ya manabii, na Injili (Injil).



KUNA MUNGU WA KWELI MMOJA TU

Kumbukumbu La Torati 6:4, 5

BWANA, Mungu wetu, BWANA ndiye mmoja. Nawe mpende BWANA, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote.



Isaya 45:18

Maana BWANA, aliyeziumba mbingu, asema hivi; Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa, aliiumba ili ikaliwe na watu; Mimi ni BWANA, wala hapana mwingine.

1 Wafalme 8:60

Watu wote wa ulimwengu Wajue ya kuwa BWANA ndiye Mungu; hakuna mwingine.

Mimi ni BWANA; ndilo jina langu; na utukufu wangu sitampa mwingine, wala sitawapa sanamu sifa zangu. —Isaya 42:8

Isaya 43:10, 11

Ninyi ni mashahidi wangu, asema BWANA,. . . mpate kujua, na kuniamini, na kufahamu ya kuwa mimi ndiye; kabla yangu hakuumbwa Mungu awaye yote, wala baada yangu mimi hatakuwapo mwingine. Mimi, naam, mimi, ni BWANA, zaidi yangu mimi hapana mwokozi.

Isaya 45:22

Niangalieni mimi, mkaokolewe, enyi ncha zote za dunia; maana mimi ni Mungu; hapana mwingine.



MUNGU NI WA REHEMA NA NEEMA

Zaburi 103:8, 11

BWANA amejaa huruma na neema, haoni hasira upesi, ni mwingi wa fadhili. Maana mbingu zilivyoinuka juu ya nchi, kadiri ileile rehema zake ni kuu kwa Wamchao.

Zaburi 103:17, 18

Bali fadhili za BWANA zina Wamchao tangu milele hata milele,...maana, wale walishikao agano lake, na kuyakumbuka maagizo yake ili wayafanye.

Mika 7:18

Ni nani aliye Mungu kama wewe, mwenye kusamehe uovu,...kwa maana yeye hufurahia rehema.

Maombolezo 3:22

Ni huruma za BWANA kwamba hatuangamii, kwa kuwa rehema zake hazikomi.

Maombolezo 3:32

Maana ajapomhuzunisha atamrehemu, kwa kadiri ya wingi wa huruma zake.

Zaburi 18:25

Kwa mtu mwenye fadhili utakuwa mwenye fadhili.

1 Mambo Ya Nyakati 16:34

Mshukuruni BWANA kwa kuwa ni mwema; kwa maana fadhili zake ni za milele.



MUNGU ANAKUPENDA  KULIKO UNAVYOWEZA KUWAZA WEWE

Yeremia 31:3

BWANA alinitokea zamani, akisema, Naam, nimekupenda kwa upendo wa milele, ndiyo maana nimekuvuta kwa fadhili zangu.

Yeremia 29:11

Maana nayajua mawazo ninayowawazia ninyi, asema BWANA, ni mawazo ya amani, wala Si ya mabaya, kuwapa ninyi tumaini siku zenu za mwisho.

Malaki 1:2

Nimewapenda ninyi, asema BWANA.

Zaburi 103:13

Kama vile baba awahurumiavyo watoto wake, ndivyo BWANA anavyowahurumia wamchao.

Isaya 38:17

Tazama; nalikuwa na uchungu mwingi kwa ajili ya amani yangu; Lakini kwa kunipenda [ee Mungu] umeniokoa na shimo la uharibifu; kwa maana umezitupa dhambi zangu zote nyuma yako.

1 Yohana 4:16, 19

Nasi tumelifahamu pendo alilo nalo Mungu kwetu sisi, na kuliamini. Sisi twapenda kwa maana yeye alitupenda sisi kwanza.

Sefania 3:17

BWANA, Mungu wako, yu katikati yako shujaa awezaye kuokoa; atakushangilia kwa furaha kuu, atatulia katika upendo wake. Atakufurahia kwa kuimba.



JAMBO KUBWA MUHIMU MAISHA NI MTU  KUMJUA MUNGU NA ANATAKA UFANYE NINI,

Danieli 11:32

Lakini watu wamjuao Mungu wao watakuwa hodari, na kutenda mambo makuu.

Yeremia 9:24

Bali ajisifuye na ajisifu kwa sababu hii, ya kwamba ananifahamu mimi, na kunijua, ya kuwa mimi ni BWANA, nitendaye wema, na hukumu, na haki, katika nchi; maana mimi napendezwa na mambo hayo, asema BWANA.

Kumbukumbu La Torati 30:19, 20

Nimekuwekea mbele yako uzima na mauti, baraka na laana; basi chagua uzima, kumpenda BWANA, Mungu wako, kuitii sauti yake na kushikamana naye: kwani hiyo ndiyo uzima wako.

Zaburi 119:2

Heri wazitiio shuhuda zake, wamtafutao kwa moyo wote.

Zaburi 42:1

Kama ayala aioneavyo shauku mito ya maji. Vivyo hivyo nafsi yangu inakuonea shauku, Ee Mungu.

Kutoka 33:14

Akasema, Uso wangu utakwenda pamoja nawe, nami nitakupa raha.



KUJITEGEMEA PASIPO MUNGU NI KUJIANGAMIZA WEWE MWENYEWE

2 Mambo Ya Nyakati 15:2

BWANA yu pamoja nanyi, mkiwa pamoja naye; nanyi mkimtafuta ataonekana kwenu; lakini mkimwacha atawaacha ninyi.

Yeremia 17:9

Moyo huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?

Mithali 16:25

Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu; lakini mwisho wake ni njia za mauti.

2 Petro 2:4, 9

Kwa maana ikiwa Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa, bali aliwatupa shimoni, akawatia katika vifungo vya giza, walindwe hata ije hukumu. Basi, Bwana ajua kuwaokoa watauwa na majaribu, na kuwaweka wasio haki katika hali ya adhabu hata siku ya hukumu.

1 Samweli 12:15

Bali msipoisikia sauti ya BWANA, mkiiasi amri ya BWANA, ndipo mkono wa BWANA utakuwa juu yenu.

Yohana 15:6

Mtu asipokaa ndani yangu, hutupwa nje kama tawi na kunyauka; watu huyakusanya na kuyatu. pa motoni yakateketea.



UKIMJUA MUNGU NI LAZIMA UTAMTAFUTA NA KUFANYA MAPENZI YAKE.

Yeremia 29:13

Nanyi mtanitafuta, na kuniona, mtakaponitafuta kwa moyo wenu wote.

Mithali 2:4, 5

Ukiutafuta kama fedha, . . . ndipo utakapo . . . pata kumjua Mungu.



Mathayo 7:7

Ombeni, nanyi mtapewa; tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa.

Waebrania 11:6

Lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza; kwa maana mtu amwendeaye Mungu lazima aamini kwamba yeye yuko, na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao.

Mithali 8:17

Nawapenda wale wanipendao, na wale wanitafutao kwa bidii wataniona.

Maombolezo 3:25

BWANA ni mwema kwa hao wamngojeao, kwa hiyo nafsi imtafutayo.

Matendo 17:26, 27

Naye alifanya kila taifa la wanadamu kutoka katika mmoja. ...Ili wamtafute Mungu, ingawa ni kwa kupapasa-papasa, wakamwone, ijapokuwa hawi mbali na kila mmoja wetu.



MUNGU ANATUTAKA TWENDE KWAKE

2 Mambo Ya Nyakati 30:9

Kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ndiye mwenye neema, na mwenye rehema, wala hatawageuzia mbali uso wake, mkimrudia.

Zaburi 86:5

Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, umekuwa tayari kusamehe, na mwingi wa fadhili, kwa watu wote wakuitao.

Yakobo 4:8

Mkaribieni Mungu, naye atawakaribia ninyi.

Zaburi 145:18

BWANA yu karibu na wote Wamwitao, wote wamwitao kwa uaminifu.

Isaya 1:18

Haya, njoni, tusemezane, asema BWANA Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.

Mathayo 11:28, 29

Njoni kwangu, ninyi nyote msumbukao na wenye kulemewa na mizigo, nami nitawapumzisha. Jitieni nira yangu, mjifunze kwangu; kwa kuwa mimi ni mpole na mnyenyekevu wa moyo; nanyi mtapata raha nafsini mwenu.

Yohana 6:37

Wala ye yote ajaye kwangu sitamtupa nje kamwe.



MUNGU NI MTAKATIFU, NA ANATAKA TUWE WATAKATIFU KAMA YEYE ALIVYO MTAKATIFU

Kutoka 15:11

. . . Ni nani aliye kama wewe, Ee BWANA, . . . mtukufu katika utakatifu.

1 Samweli 2:2 Maandiko yana tuakikishia wazi wazi,

KUVUNJA USHIRIKA NA MUNGU

Dhambi inamuharibia mwanadamu ushirika na Mungu,

Mkristo anapotenda dhambi haimaansihi kwamba amevunja uhusiano wake na Mungu. Maana yake ni kwamba amevunja ushirika wake na Mungu. Yeye bado ni mtoto wa Mungu, lakini sasa ni mtoto asiyeti. Ikiwa mwamini hataungama dhambi yake na kutubu, anajiweka kwenye nafasi ya kuadhibiwa na Bwana.


Vita Baada ya kukata shahuri

Kama umejikuta unatamani kufanya mambo unayojua ni makosa, basi umeanza kukabiliana na “tamaa ya mwili”. Bila shaka umegundua pia kwamba unapojaribiwa na mwili kufanya kisicho sawa, kuna kitu ndani yako kinachopinga majaribu hayo. Hicho ni “tamaa ya Roho”. Na kama unajua jinsi kujisikia hatia kunavyokupata ukikubaliana na majaribu, basi unaifahamu sauti ya roho yako, tunayoiita “dhamiri” yetu.

Mungu alijua vizuri sana kwamba tamaa zetu za mwili zingetujaribu tufanye makosa. Lakini, hiyo si sababu inayoturuhusu kukubaliana na tamaa za mwili. Bado Mungu anatutazamia tutende kwa utii na utakatifu, na tushinde asili ya mwili.

Lakini nasema hivi: Enendeni katika Roho, nanyi hamtazitimiza tamaa za mwili (Wagalatia 5:16, .

Hakuna mbinu ya kiuchawi ya kushinda mwili. Paulo alisema tu kwamba “tuenende katika Roho” nasi “hatutatimiza tamaa za mwili” (Wagalatia 5:16). Hakuna Mkristo mwenye uwezo zaidi ya mwenzake katika jambo hili. Kutembea katika Roho ni uamuzi ambao kila mmoja wetu lazima aufanye, na kujitolea kwetu kwa Bwana kunaweza kupimwa kwa kiwango cha kutojitolea kwetu kwa tamaa za mwili.

Paulo akaandika hivi tena:

Na hao walio wa Kristo Yesu wameusulubisha mwili pamoja na mawazo yake mabaya, na tamaa zake (Wagalatia 5:24).

Ona anachosema Paulo: Wale walio wa Kristo wameusulubisha mwili (anatumia lugha ya wakati uliopita). Hayo yalitokea wakati tulipotubu na kumwamini Bwana Yesu Kristo. Hapo, tulisulubisha ile asili ya dhambi, tukaamua kumtii Mungu na kupingana na dhambi. Sasa, si swala la kusulubisha mwili tena, bali kudumisha kule kusulubiwa.

Si rahisi kuendelea kuusulubisha mwili, lakini ni kitu kinachowezekana. Kama tutatenda kulingana na kuongozwa kwa utu wa ndani badala ya kukubaliana na misukumo ya mwili, tutaonyesha maisha ya Kristo na kuenenda katika utakatifu mbele Zake.

Asili Ya Roho Kurejeshwa tena Upya,

Kuna neno moja lenye kueleza vizuri zaidi asili ya roho zetu zilizoumbwa tena. Neno hilo ni Kristo. Kwa njia ya Roho Mtakatifu ambaye ana asili ile ile ya Yesu, sisi ndani yetu tuna asili ya Yesu. Paulo aliandika hivi: “Si mimi ninayeishi tena, bali Kristo anaishi ndani yangu” (Wagalatia 2:20,

Kwa sababu tuna uwezo Wake na asili Yake ndani yetu, tunao uwezo wa ajabu sana wa kuishi kama Kristo. Hatuhitaji upendo zaidi, au uvumilivu, au kiasi – ndani yetu tunaye Mtu mwenye upendo sana, mwenye uvumilivu sana, mwenye kiasi sana – anakaa ndani yetu! Tunachohitaji kufanya ni kumruhusu Yeye kuishi kwa kututumia sisi.

Ila, wote tuna adui mmoja mkubwa ambaye anapambana na asili ya Yesu, akiizuia isijidhihirishe kupitia kwetu, naye ni mwili wetu. Ndiyo maana Paulo alisema lazima kuusulubisha mwili wetu. Ni wajibu wetu kufanya kitu juu ya mwili wetu, na ni kupoteza wakati kumwomba Mungu afanye chochote kuhusu mwili. Hata Paulo alikuwa na matatizo na asili yake ya kimwili, lakini aliwajibika na kuushinda. Anasema hivi:

Ninautesa mwili wangu na kuufanya mtumwa, ili, baada ya kuwahubiri wengine, mimi mwenyewe nisije nikakataliwa (1Wakor. 9:27,

Hata wewe itabidi kuufanya mwili wako kuwa mtumwa wa roho yako, kama unataka kuenenda kwa utakatifu mbele za Bwana. Na, inawezekana! kabisa ila ukitaka mwili ufanye mapenzi yake nayo ni hatari kwa mkristo unaweza kumpeleka pabaya

K2 MAUTI YA KI-ROHO

Fuatilia yale aliyo yasema Yesu ili kupa muongozo zaidi kuhusiana na kile kinacho sadikika kufa ki-roho maana wengi wamezowea kusikia mtu amefariki ile ya mwili kutengana na roho,ila kuna ile ya mtu kutengana na Mungu inakuwaje?unaweza ukawa kimwili uko hai ila kiroho ukawa tayari ni marehemu,

Maneno ya Yesu ni maelezo sahihi kabisa ya washika dini wote ambao hawajawahi kuzaliwa upya kwa njia ya Roho Mtakatifu. Kuzaliwa upya huwasafisha watu ndani, si nje tu.


Mabadiliko Kwa Nafsi Wakati Roho Inapozaliwa Upya?

Roho ya mtu inapozaliwa upya, nafsi yake hapo mwanzoni inabakia kama ilivyokuwa (ingawa kwa akili zake anakuwa amefanya uamuzi wa kumfuata Yesu). Ila, Mungu anatazamia kwamba tufanye kitu na nafsi zetu mara tunapokuwa watoto Wake. Nafsi zetu (au nia) zinapaswa kufanywa upya kwa Neno la Mungu ili tuweze kufikiri kama Mungu anavyofikiri. Kwa kufanywa upya nia zetu, badiliko la kudumu la nje linafanyika maishani mwetu, na kutufanya tuzidi kufanana na Yesu.

Wala msiifuatishe namna ya dunia hii, bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu (Warumi 12:2, maneno mepesi kukazia).

Hata Yakobo naye aliandika kuhusu mfuatano huo wa mambo katika maisha ya mwamini, hivi:

Kwa hiyo wekeni mbali uchafu wote na ubaya uzidio, na kupokea kwa upole neno lile lililopandwa ndani, liwezalo kuziokoa nafsi zenu (Yakobo 1:21,

Ona kwamba Yakobo alikuwa anawaandikia Wakristo – watu ambao roho zao zilikuwa zimekwisha zaliwa upya. Ila, walihitaji nafsi zao kuokolewa, na hayo yangefanyika tu wakati anapopokea “neno lile lililopandwa ndani”. Hii ndiyo sababu waamini wapya wanatakiwa kufundishwa Neno la Mungu.

Usumbufu unaoweza kujitokeza baada ya kuamuwa kuyafuata ya Mungu,

Baada ya kuzaliwa upya kwao, Wakristo wengi hugundua kwamba ni watu wenye asili mbili, na kujikuta wakikabiliana na kile kitu kinachoitwa na Paulo, vita kati ya “Roho na mwili”.

Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili, kwa maana hizi zi mepungana, hata hamwezi kufanya mnayotaka (Wagalatia 5:17).

Mabaki ya ile asili ya kale ya dhambi, yanaitwa “mwili” na Paulo. Hizo asili mbili ndani yetu huleta shauku tofauti, ambazo, kama watu watakubaliana nazo, husababisha matendo tofauti na mitindo tofauti ya maisha. Ona tofauti anayoweka Paulo kati ya “matendo ya mwili” na “tunda la Roho” katika fungu lifuatalo:

Basi matendo ya mwili ni dhahiri, ndiyo haya: Uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo. Katika hayo nawaambia mapema, kama nilvyokwisha kuwaambia ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu. Lakini tunda la Roho ni: Upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi. Juu ya mambo kama hayo hakuna sheria (Wagalatia 5:19-23).

Bila shaka inawezekana kwa Wakristo kukubaliana na mwili, vinginevyo Paulo asingewaonya kwamba kuzoea kuufuata mwili kutawafanya wasiweze kuurithi ufalme wa Mungu. Katika barua yake kwa Warumi, Paulo aliandika pia juu ya hizo asili mbili za kila Mkristo, na akaonya tena juu ya matokeo hayo hayo, kama watu watakubaliana na mwili. Anasema hivi:

Na Kristo akiwa ndani yenu, mwili wenu umekufa kwa habari ya dhambi, bali roho yenu iko hai kwa habari ya haki. … Basi ndugu, kama ni hivyo, wote tunawajibika, si kwa mwili kwamba tuishi kwa kufuata mambo ya mwili. Kwa maana, mkiishi kwa kufuata mambo ya mwili mwataka kufa, bali mkiyafisha matendo ya mwili kwa Roho, mtaishi. Kwa kuwa wote wanao-ongozwa na Roho wa Mungu ndio wana wa Mungu hao (Warumi 8:10, 12-14, TLR. Maneno mepesi kukazia).

Hilo ni onyo dhahiri kabisa kwa Wakristo kwamba, kuishi (yaani tabia ya kawaida, au mazoea) kulingana na mwili matokeoyake ni kifo. Bila shaka Paulo alikuwa anaonya juu ya kifo cha kiroho maana kila mtu hatimaye hufa kimwili – hata Wakristo wale wanao”yafisha matendo ya mwili”.

Mkristo anaweza kuangukia katika mojawapo ya dhambi ambazo Paulo aliorodhesha hapo kwa kitambo tu. Ila, mwamini anapofanya dhambi, atajisikia hukumu na pengine atatubu. Yeyote anayeungama dhambi yake na kumwomba Mungu amsamehe, atasafishwa (ona 1Yohana 1:9).

MAUTI YA KI-ROHO

Kufa ki-Roho


Nanyi mlikuwa wafu Kwa sababu ya makosa na dhambi zenu, ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu na kwa kumfuata mfalme wa uwezo wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi. Zamani sisi sote nasi tulienenda kati yao katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa kwa tabia yetu watoto wa hasira kama na hao wengine (maneno mepesi kukazia). Waefeso 2:1-3



Bila shaka Paulo alikuwa hazungumzii kifo cha kimwili kwa sababu alikuwa anawaandikia watu waliokuwa hai kimwili. Lakini akasema, hapo zamani walikuwa “wafu kwa sababu ya makosa na dhambi zao.” Dhambi hufungua mlango wa kifo cha kiroho (tazama Warumi 5:12). Kuwa wafu kiroho maana yake ni kuwa na asili ya dhambi rohoni mwako. Ona maneno ya Paulo kwamba, “kwa tabia” wakawa watoto wa hasira.



Tena, kufa kiroho maana yake kuwa na asili ya Shetani katika roho yako kwa namna fulani. Paulo alisema kwamba wale wote waliokufa kiroho wana roho ya “mkuu wa uwezo wa anga” ikitenda kazi ndani yao. Huyo “mkuu wa uwezo wa anga” ni Shetani (tazama Waefeso 6:12), na roho yake inatenda kazi ndani yao wote ambao hawajaokoka.



Yesu aliwaambia hivi Wayahudi waliokuwa hawajazaliwa mara ya pili:



Ninyi ni wa baba yenu Ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo, wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo husema yaliyo yake mwenyewe, kwa sababu yeye ni mwongo na baba wa huo (Yohana 8:44).



Kwa upande wa kiroho, wale ambao hawajazaliwa tena si tu kwamba wana asili ya Shetani katika roho zao, bali Shetani ni baba yao wa kiroho pia. Basi, ni kawaida kwao kutenda kama shetani. Wao ni wauaji na waongo.



Si kwamba watu wote ambao hawajaokoka wamefanya mauaji, bali ni kwamba wanahamasishwa na chuki ile ile kama ya wauaji, nao wangeweza kuua kama wangefanikiwa. Kuhalalishwa utoaji mimba katika nchi nyingi ni uthibitisho wa kweli hiyo. Watu ambao hawajaokoka wataua hata watoto wao wenyewe, ambao bado hawajzaliwa!



Hii ndiyo sababu mtu lazima azaliwe tena kiroho. Inapotokea hivyo, hiyo asili ya dhambi na kishetani huondolewa katika roho yake, na nafasi yake huchukuliwa na asili ya Mungu takatifu. Roho Mtakatifu wa Mungu huja na kukaa ndani ya roho yake. Hawi “mfu kiroho” tena, bali anafanywa “hai kiroho”. Roho yake haiwi imekufa tena bali inakuwa hai kwa Mungu. Badala ya kuwa mtoto wa kiroho wa Shetani, anakuwa mtoto wa kiroho wa Mungu.



Matengenezo Si Kuzaliwa Upya



Kwa sababu watu ambao hawajaokoka wamekufa kiroho, hawawezi kuokolewa kwa matengenezo, hata kama watajaribu kiasi gani. Watu ambao hawajaokoka wanahitaji asili mpya, si matendo mapya ya nje tu. Unaweza kumchukua nguruwe, ukamsafisha vizuri akawa safi, ukampulizia hata manukato na kumfungia tai ya rangi nzuri tu shingoni mwake, lakini mwisho wa siku ulicho nacho ni nguruwe aliyesafishwa tu! Bado asili yake ni ile ile. Na hautapita muda mrefu kabla hajaanza kunuka vibaya tena na kulala kwenye matope tena.



Ndivyo ilivyo kwa watu washika dini sana ambao hawajawahi kuzaliwa tena. Wanaweza kuwa wasafi kwa nje, lakini ndani ni wachafu tu kama kawaida. Yesu alisema hivi kwa watu washika dini wa siku Zake:



Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mnasafisha nje ya kikombe chanu, na ndani yake vimejaa unyang’anyi na kutokuwa na kiasi. Ewe Farisayo kipofu! Safisha kwanza ndani ya kikombe, ili nje yake nayo ipate kuwa safi! Ole wenu waandishi na Mafarisayo, wanafiki! Kwa kuwa mmefanana na makaburi yaliyopakwa chokaa, nayo kwa nje yaonekana kuwa mazuri, bali ndani yamejaa mifupa ya wafu na uchafu wote. Vivyo hivyo ninyi nanyi: Kwa nje mwaonekana na watu kuwa wenye haki, bali ndani mmejaa unafiki na maasi! (Mathayo 23:25-28). inaandelea mauti ya kiroho k'2

KUZALIWA MARA YA PILI

Kuzaliwa Upya


Watu wanapotubu na kumwamini Bwana Yesu Kristo, wana”zaliwa mara ya pili”. Nini hasa maana ya kuzaliwa mara ya pili? Sura hii itafafanua zaidi hivyo kama lilikuwa ni moja ya swali lako utasaidika sana .



Ili kuweza kuelewa maana ya kuzaliwa mara ya pili, inasaidia sana kuanza kwa kuelewa asili ya wanadamu. Maandiko yanatuambia kwamba sisi si viumbe wa kimwili tu, bali wa kiroho pia. Kwa mfano: Paulo aliandika hivi:



Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa. Nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, hadi wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo (1Wathes. 5:23, maneno mepesi kukazia).



Kama Paulo alivyoonyesha, tunaweza kujihesabu kuwa viumbe wenye sehemu tatu: roho, nafsi na mwili. Maandiko hayafafanui sana hizo sehemu tatu, kwa hiyo, tunajitahidi sana kuzitofautisha kwa ufahamu wetu wa maneno yenyewe. Mara nyingi tunasema hivi: Mwili wetu ni umbo tulilo nalo – nyama, mifupa, damu na kadhalika. Nafsi yetu ni ufahamu wetu na uwezo wetu wa kujisikia – akili yetu. Roho yetu bila shaka ni ile hali yetu ya kiroho, au kama mtume Petro anavyoeleza, “utu wa ndani uliofichika” (1Petro 3:4, TLR).



Kwa sababu roho haionekani kwa macho ya kimwili, watu wasio-okoka wanakana kuwepo kwake. Lakini Biblia iko wazi kabisa kwamba wote sisi ni viumbe wa kiroho. Maandiko yanatuambia kwamba mtu anapokufa, ni mwili wake tu ndiyo unakoma kufanya kazi, lakini roho yake na nafsi vinaendelea kama kawaida. Wakati wa kufa, hivyo viwili vinatoka katika mwili (kwa pamoja) ili kwenda kuhukumiwa mbele za Mungu (ona Wabrania 9:27). Baada ya hukumu, vinakwenda mbinguni au jehanamu. Mwisho wa yote, kila roho na nafsi ya mtu itaungana na mwili wake wakati wa ufufuo.



Roho Ya Mwanadamu Ikifafanuliwa Zaidi

Katika 1Petro 3:4, Petro anazungumza juu ya roho kama “utu wa moyoni usioonekana” kuonyesha kwamba roho ni mtu. Paulo pia alizungumza juu ya roho kama “mtu wa ndani” kuonyesha imani yake kwamba roho ya mwanadamu si nguvu fulani au wazo tu, bali ni mtu. Anasema hivi:



Kwa hiyo hatulegei, bali, ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku (2Wakor. 4:16, maneno mepesi kukazia).



“Utu wa nje” bila shaka ni maelezo kuhusu mwili, na “utu wa ndani” ni maelezo kuhusu roho. Ni hivi: Japo mwili unazeeka, roho inafanywa upya kila siku.



Ona tena kwamba Paulo anataja mwili na roho kama watu. Basi, unapofikiria roho yako, usifikiri wingu fulani la kiroho. Ni afadhali ufikiri kuhusu mtu mwenye umbo linalofanana na lako. Kama mwili wako umezeeka, usidhani na roho yako imezeeka pia. Jaribu kufikiri jinsi ulivyokuwa ujanani mwako, kwa sababu, roho yako haijazeeka – iko kama ulivyokuwa ukiwa kijana! Inafanywa upya siku kwa siku.



Roho yako ndiyo sehemu yako inayozaliwa mara ya pili (kama umemwamini Bwana Yesu). Roho yako inaungana na Roho wa Mungu (ona 1Wakor. 6:17), na Yeye ndiye anayekuongoza unapomfuata Yesu (ona Warumi 10:14).



Biblia inafundisha kwamba Mungu pia ni roho (ona Yohana 4:24), na hata malaika, na mapepo pia. Wote wana maumbo na wote wapo katika ulimwengu wa roho. Ila, ulimwengu wa roho hauwezi kutambuliwa kwa hisia zetu za kimwili. Kujaribu kuwasiliana na ulimwengu wa roho kwa hisia zetu za kimwili ni sawa na kujaribu kushika mawimbi ya redio kwa mikono yetu. Hatuwezi kutambua kwa hisia zetu za kimwili kwamba mawimbi ya redio yanapita katika chumba, lakini hiyo haithibitishi kwamba hakuna mawimbi ya redio. Njia pekee ya kuyapata hayo mawili ni kuifungulia redio.



Hayo pia ni kweli kwa habari ya ulimwengu wa kiroho. Kwa kuwa ulimwengu wa kiroho hauwezi kutambuliwa na hisia za kimwili  bali katika ulimwengu wa kiroho haimaanishi kwamba haupo. Upo, na watu wakijua au wasijue, ni sehemu ya ulimwengu wa kiroho kwa sababu ni viumbe wa kiroho nidio wanaoweza kuwasiliana au kuihshi maisha hayo.ili kuweza  kuhusiana na Mungu kiroho (kama wamezaliwa mara ya pili), au wanahusiana na Shetani kiroho (kama hawajatubu).

Kuna watua mbao wamejifunza jinsi ya kuwasiliana na ulimwengu wa kiroho kwa njia ya roho zao, lakini wao wanawasiliana na ufalme wa Shetani – ufalme wa giza. maana wamekubali maagano ya shetani kwanamna ya hilo agano waliloliweka, kwa mfano hawa wachawi unaosikia wameloga wanatumia njia za ulimwengu wa kiroho kwa upande wa nguvu za giza, na kumshinda huyo nilazima na wewe uwe unaishi maisha ya k-Roho kwa upande wa Nuru yaani wa Mungu,

Blog Archive

Followers