|
Kuoshwa miguu
Yohana 13:3-8
Neno la
msingi Yesu, hali akijua ya kuwa Baba amempa vyote mikononi mwake, na ya kuwa
alitoka kwa Mungu naye anakwenda kwa Mungu,
aliondoka chakulani; akaweka kando mavazi yake, akatwaa kitambaa, akajifunga kiunoni. Kisha akatia maji katika bakuli, akaanza kuwatawadha wanafunzi miguu, na kuifuta kwa kile kitambaa alichojifunga. Hivyo yuaja kwa Simoni Petro. Huyo akamwambia, Bwana! Wewe wanitawadha miguu mimi? Yesu akajibu, akamwambia, Nifanyalo wewe hujui sasa; lakini utalifahamu baadaye. Petro akamwambia, Wewe hutanitawadha miguu kamwe. Yesu akamwambia, Kama nisipokutawadha, huna shirika nami.
Utangulizi:
kuoshwa miguu ni moja ya tukio lililoanzishwa na Yesu
kristo na akaacha agizo kwa wanafunzi wake kwamba zoezi lakuosha miguu liendelezwe kufanyika mara zote,kama
alivyosema kushiriki meza ya bwana, kwasababu kila tukio linamaana yake
kimwili na kiroho,
Viwango viningine tunavyovitaka kila siku katika maisha
yetu haviwezekani pasipo kuunganishwa
hivyo kuna huduma tunazipata kupitia sehemu flani ila unapoonganishwa unakuwa
tofauti maana unakuwa sehemu ya kile unachokihitaji
Mfano:
Kunawakati unataka kubarikiwa ila unapounganishwa
unakuwa wewe ndiye baraka kwa wengeine,unapoonganishwa wewe unakuwa
mwanachama,unapoonganishwa unakuwa mshirika,unapoonganishwa unakuwa mwamini,unapoonganishwa
unakuwa mfuasi, unapoonganishwa unakuwa kitu kimoja,mashambulizi,na matatizo
mengi ya watu katika huduma zao hawajaonganishwa na hizo huduma,
Ni mwimbaji lakini si sehemu ya kile anachokiimba,ni
mhubiri ila hajaonganishwa na kile anachokiongea,
Kwa nini
watu waonganishwa ni kwasababu
tunataka matokeo sawa,mtazamo mmoja,jicho moja safari moja nguvu moja agizo
moja la kristo,
Watu wengi wanaishi katiki maisha ya kwao hawana
ushirika na Mungu Wanamtaja Mungu ila hawajaunganika,Yohana 1:12 kwasababu kuna watu wamehama viwango ila
hawajaonganishwa kuhama kituo na kuonganishwa ni mambo mawili tofauti,
Matokeo
mazuri ya kile unachokitaka ni maandalizi ya uliyofanya,
ili uwene mabadiliko na matokeo makubwa katika maisha
yako ya kiroho ni lazima ukubali kuonganishwa,
Faida za kuonganishwa
v Unapoonganishwa Unakuwa umeingizwa ulimwengu mpya wa kiroho,
v Faida ya kuonganishwa unaishi katika mamlaka za ki Mungu
v Unaishi duniani ila huwazi kama dunia huyaoni mambo kama Dunia inavyoona
hisia zako ni zatofauti kabisa
v Unapoonganishwa Unakuwa na uhalalimkuwa wa kuhudumiwa kipekee na Mungu wa
madhabahu,
v Unapoonganishwa mmoja kwa moja unapata fursa ya kupatajambo jipya kia
inapoitwa leo,
v Unapoonganishwa ni rahisi kuhama vituo kila inapoitwa leo,
v Unapoonganishwa na Mungu utatetewa na nguvu ya pale ulikojiunganishia
watu
v Unapata mwili wa Mungu
v Unawaza kwa ufahamu wa KiMungu
v Unaishi na moyo wa Mungu
v Utaishi maisha ya kuzidishwa,
v Utaishi maisha yako halisi
v Faida ya kuonganiswa unadumu katika Huduma,
v Faida ya kuonganishwa Mungu anakuwa upande wako
v Faida ya kuonganishwa kazi zote
unazozitenda zinafanikiwa Waphili 1:5
Matendo 1:14 wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja
katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake.
Wagalatia 2: 9.tena walipokwisha kuijua ile neema niliyopewa; Yakobo,
na Kefa, na Yohana, wenye sifa kuwa ni nguzo, walinipa mimi na Barnaba mkono
wa kuume wa shirika; ili sisi tuende kwa Mataifa, na wao waende kwa watu wa tohara;
10 ila neno moja tu walitutakia, tuwakumbuke maskini; nami neno lilo hilo nalikuwa na bidii kulifanya.
Ufanye nini kuonganishwa
Utayari wa akili moyo |
|
|
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
Subscribe to:
Posts (Atom)