KUZALIWA MARA YA PILI

Kuzaliwa Upya


Watu wanapotubu na kumwamini Bwana Yesu Kristo, wana”zaliwa mara ya pili”. Nini hasa maana ya kuzaliwa mara ya pili? Sura hii itafafanua zaidi hivyo kama lilikuwa ni moja ya swali lako utasaidika sana .



Ili kuweza kuelewa maana ya kuzaliwa mara ya pili, inasaidia sana kuanza kwa kuelewa asili ya wanadamu. Maandiko yanatuambia kwamba sisi si viumbe wa kimwili tu, bali wa kiroho pia. Kwa mfano: Paulo aliandika hivi:



Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa. Nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, hadi wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo (1Wathes. 5:23, maneno mepesi kukazia).



Kama Paulo alivyoonyesha, tunaweza kujihesabu kuwa viumbe wenye sehemu tatu: roho, nafsi na mwili. Maandiko hayafafanui sana hizo sehemu tatu, kwa hiyo, tunajitahidi sana kuzitofautisha kwa ufahamu wetu wa maneno yenyewe. Mara nyingi tunasema hivi: Mwili wetu ni umbo tulilo nalo – nyama, mifupa, damu na kadhalika. Nafsi yetu ni ufahamu wetu na uwezo wetu wa kujisikia – akili yetu. Roho yetu bila shaka ni ile hali yetu ya kiroho, au kama mtume Petro anavyoeleza, “utu wa ndani uliofichika” (1Petro 3:4, TLR).



Kwa sababu roho haionekani kwa macho ya kimwili, watu wasio-okoka wanakana kuwepo kwake. Lakini Biblia iko wazi kabisa kwamba wote sisi ni viumbe wa kiroho. Maandiko yanatuambia kwamba mtu anapokufa, ni mwili wake tu ndiyo unakoma kufanya kazi, lakini roho yake na nafsi vinaendelea kama kawaida. Wakati wa kufa, hivyo viwili vinatoka katika mwili (kwa pamoja) ili kwenda kuhukumiwa mbele za Mungu (ona Wabrania 9:27). Baada ya hukumu, vinakwenda mbinguni au jehanamu. Mwisho wa yote, kila roho na nafsi ya mtu itaungana na mwili wake wakati wa ufufuo.



Roho Ya Mwanadamu Ikifafanuliwa Zaidi

Katika 1Petro 3:4, Petro anazungumza juu ya roho kama “utu wa moyoni usioonekana” kuonyesha kwamba roho ni mtu. Paulo pia alizungumza juu ya roho kama “mtu wa ndani” kuonyesha imani yake kwamba roho ya mwanadamu si nguvu fulani au wazo tu, bali ni mtu. Anasema hivi:



Kwa hiyo hatulegei, bali, ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku (2Wakor. 4:16, maneno mepesi kukazia).



“Utu wa nje” bila shaka ni maelezo kuhusu mwili, na “utu wa ndani” ni maelezo kuhusu roho. Ni hivi: Japo mwili unazeeka, roho inafanywa upya kila siku.



Ona tena kwamba Paulo anataja mwili na roho kama watu. Basi, unapofikiria roho yako, usifikiri wingu fulani la kiroho. Ni afadhali ufikiri kuhusu mtu mwenye umbo linalofanana na lako. Kama mwili wako umezeeka, usidhani na roho yako imezeeka pia. Jaribu kufikiri jinsi ulivyokuwa ujanani mwako, kwa sababu, roho yako haijazeeka – iko kama ulivyokuwa ukiwa kijana! Inafanywa upya siku kwa siku.



Roho yako ndiyo sehemu yako inayozaliwa mara ya pili (kama umemwamini Bwana Yesu). Roho yako inaungana na Roho wa Mungu (ona 1Wakor. 6:17), na Yeye ndiye anayekuongoza unapomfuata Yesu (ona Warumi 10:14).



Biblia inafundisha kwamba Mungu pia ni roho (ona Yohana 4:24), na hata malaika, na mapepo pia. Wote wana maumbo na wote wapo katika ulimwengu wa roho. Ila, ulimwengu wa roho hauwezi kutambuliwa kwa hisia zetu za kimwili. Kujaribu kuwasiliana na ulimwengu wa roho kwa hisia zetu za kimwili ni sawa na kujaribu kushika mawimbi ya redio kwa mikono yetu. Hatuwezi kutambua kwa hisia zetu za kimwili kwamba mawimbi ya redio yanapita katika chumba, lakini hiyo haithibitishi kwamba hakuna mawimbi ya redio. Njia pekee ya kuyapata hayo mawili ni kuifungulia redio.



Hayo pia ni kweli kwa habari ya ulimwengu wa kiroho. Kwa kuwa ulimwengu wa kiroho hauwezi kutambuliwa na hisia za kimwili  bali katika ulimwengu wa kiroho haimaanishi kwamba haupo. Upo, na watu wakijua au wasijue, ni sehemu ya ulimwengu wa kiroho kwa sababu ni viumbe wa kiroho nidio wanaoweza kuwasiliana au kuihshi maisha hayo.ili kuweza  kuhusiana na Mungu kiroho (kama wamezaliwa mara ya pili), au wanahusiana na Shetani kiroho (kama hawajatubu).

Kuna watua mbao wamejifunza jinsi ya kuwasiliana na ulimwengu wa kiroho kwa njia ya roho zao, lakini wao wanawasiliana na ufalme wa Shetani – ufalme wa giza. maana wamekubali maagano ya shetani kwanamna ya hilo agano waliloliweka, kwa mfano hawa wachawi unaosikia wameloga wanatumia njia za ulimwengu wa kiroho kwa upande wa nguvu za giza, na kumshinda huyo nilazima na wewe uwe unaishi maisha ya k-Roho kwa upande wa Nuru yaani wa Mungu,

Blog Archive

Followers