muda gani ambao ungetaka kuoa au kuolewa?
Utasikia mwingine anasema, siku Mungu atakapo nipa mume au mke, hii ni hatari sana! Biblia inasema kwenye kile kitabu cha Mhubiri.3:1 “Kwa kila jambo kuna majira yake na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu”.
Kila kitu kilichoko chini ya mbingu kimeratibiwa, kwa lugha nyingine, ni kwamba kila mwanadamu ana kalenda yake, iko kalenda yako ya kuzaliwa, na ipo kalenda ya matukio na mipango mbalimbali. Mungu anaijua. Mungu anatangaza mwisho tangu mwanzo, anajua mwisho wa maisha yako wakati wewe unapozaliwa.
Katika mwanzo wa maisha yako, Mungu anakuwa amekwishajua mwisho wako; utakavyokuwa; na kama amekwishajua mwisho wako, maana yake ameshatembea kwenye maisha yako yote toka mwanzo mpaka alipofika mwisho, na alipokamilisha maisha yako akarudi mwanzo ndipo akakuongoza kuzaliwa.
Mungu anapokuacha uzaliwe duniani, hakika ujue kabisa ya kwamba amekwisha tembea na wewe katika maisha yako, amesharatibu mambo yako na yako hatua kwa hatua; kwa mfano, kitu gani utafanya, wapi utasoma, utasoma nini, utaolewa na nani au utaoa nani na itakuwa, lini, maisha yako yatakuwaje, utamtumikiaje, mpaka mwisho wako. Akiishafika mwisho wa maisha yako anarudi mwanzo, akishafika mwanzo anatangaza mwisho tangu mwanzo; kwa hiyo kuanzia hapo unapozaliwa ujue maisha yako yote yamesharatibiwa!
Ni vizuri ufahamu hii mistari itakusaidia, maana inakujengea msingi mzuri wa maisha hapa. Isaya.46:9-10 inasema, “Kumbukeni mambo ya zamani za kale maana mimi ni Mungu wala hapana mwingine, mimi ni Mungu wala hapana aliye kama mimi. Nitangazaye mwisho tangu mwanzo, na tangu zamani za kale mambo yasiyotendeka bado, nikisema, shauri langu litasimama, nami nitatenda mapenzi yangu yote”.
Kwa lugha nyingine anatuambia ya kwamba, ‘wewe unaona kila kitu ni kipya, unapoishi kila siku ni mpya, kila dakika inayokuja ni mpya, Mungu anasema hiyo safari unayopita, mimi nilikwishaipita tayari, nikafika mwisho wa maisha yako ndipo nikakuruhusu uzaliwe. Ulipokuwa unazaliwa nikatangaza mwisho wako tangu wakati unazaliwa.
Sasa mimi ninataka nikuambie kama Mungu anajua, na shauri lake anasema litasimama katika maisha yako, ili mapenzi yake ayatende katika maisha yako, unahitaji kuwa mwangalifu. Kwa sababu kuna mpango na saa ya Mungu ya kuoa au kuolewa, - ipo!
Mungu anapokuletea mawazo ya kuoa au kuolewa, ni kwa ajili yakuimarisha maisha yako na wito wako na kazi na makusudi, ambayo ameyaweka hapa duniani. Atakuletea mtu atakaye imarisha wito wako, atakuletea mtu atakaye saidiana na wewe, uwe ni mwanamke au uwe ni mwanaume.
Mungu anapo kukutanisha na mtu wa kuoana naye ni kwa ajili ya kuimarisha nguvu zenu ili mtimize kusudi la Mungu wakati mwingine unaweza kuchelewa kuowa au kuolewa kwasababu yakutokuwa na kazi ya Mungu ya kufanya hapa duniani kwasababu ataimarishaje nguvu ambazo hazitatumika? Kwa hiyo wakati mwingine usilalamike kutooa au kuolewa ipo sababu nzuri tu anayoifahamu Mungu na si mwanadamu awae. Kwa hiyo lazima anajua kuna saa huyu mvulana anahitaji mke, au huyu msichana anahitaji mume! Lakini watu wengi sana hawalifuatilii hili. Kunakuja kuwa na watoto
Maana watoto wakiwa wadogo wote, mimi ninakuambia kumtumikia Mungu ni kuna kuwa kugumu sana, usije ukafikiri ni kurahisi. Maana unahitaji kuwa karibu nao; wanahitaji kusoma shule, wanahitaji kufanya vitu mbalimbali, wanahitaji kuwa na baba karibu, wanahitaji kuwa na mama karibu. Saa nyingine mnataka kusafiri nao; unaweza ukasafiri nao lakini usije ukafikiri ni kitu kirahisi sana ila kwa wale ambao hawajaujuwa wito wao wanaweza hata kupuuzia haya yote,
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
JE ! UKO TAYARI KUOLEWE AU KUOWA:
NIVEMA UKAJIFUNZA MASOMO HAYA KABILA YA MALALAMIKO YA MAAMUZI YAKO:
Ni swali muhimu sana lakujiuliza wewe mwenyewe, uko tayari, maana yake umefika mahali hali yako ya ndani na nje, inakuruhusu kuoa au kuolewa? Uko tayari kuoa au kuolewa? Umefika mahali pa namna hiyo?. Wengine wanasema huyu ni mtoto, lakini unajua pamoja na kwamba ni mtoto, ni vizuri kujua kama uko tayari kiumri. Lakini ninapozungumzia hapa juu ya utayari wa kuoa au kuolewa, sizungumzii tu habari za miaka, bali ninazungumzia habari za hali yako ya ndani.
Nimeona kuna mtu mwingine ana miaka arobaini, lakini kwa kweli hayuko tayari kukaa na mwanamke, ndani yake, mawazo yake na kufikiri kwake, hayuko tayari kukaa na mwanamke, hawajibiki hata yeye mwenyewe juu yake mwenyewe. Wengine hata wana miaka hamsini, lakini ana hali kama hii. Nimeona akinadada hata wana miaka arobaini na tano, hayuko tayari kuolewa, maana akiolewa ni shida tu.
Nilienda mahali fulani, nikakuta dada ana umri mkubwa tu, lakini wakati wa maombi hakusema kama anataka tuombe ili aolewe. Nikaona ngoja nimuulize labda anaona aibu kusema hitaji hili kwa sababu umri umesogea, nikamwambia “hutaki tuombe uolewe”? Akasema, “hapana, sitaki kuolewa” (Na alikuwa ana umri wa miaka kama arobaini na zaidi). Nikamuuliza, “kwa nini”. Akasema, “kwa sababu sitaki kuomba ruhusa kwa mwanaume ninapotaka kutumika”. Nikamuuliza unafanya kazi, akasema, “ndio”.
Nikamwambia, “unapokwenda kumtumikia Mungu huwa unafanyaje, - unaomba ruhusa au unatoroka huko kazini?” Akasema, “ninaomba ruhusa”. Nikwamwambia, “kwa nini unaona ni rahisi kuomba ruhusa kwa mwajiri wako na unaona taabu kuomba ruhusa kwa mume wako?” Alishindwa kujibu hilo swali. Nikamwambia tatizo lako ni kubwa kuliko unavyo fikiri.
Unaweza ukaona kabisa ya kwamba, huyu mtu hayuko tayari kuolewa, wala msijaribu kumlazimisha aoelewe – pamoja na kwamba umri wake ni mkubwa. Usijaribu kumsukuma kwenye maamuzi ya kuolewa maana hayuko tayari kuolewa, akiingia kwenye ndoa atakwenda kuleta shida tu,
Mwingine unakuta ni msichana, wazazi wake ndio wanamtegemea karibu katika kila kitu. Mimi ninakuambia kabla hujafikiria kuoa au kuolewa, fikiria hilo swali. Kwa sababu ukiishaolewa tu biblia inakuambia wasahau watu wa nyumbani mwa wazazi wako (Zaburi 45:10). Sasa haimaanishi usiwasaidie, ila maana yake ni kwamba huwezi ukawasaidia tena ‘moja kwa moja’ kama ulivyokuwa unawasaidia zamani. Ni vitu lazima ujadiliane na mume wako juu ya kuwasaidia wazazi wenu wa pande zote mbili – maana mna mipango yenu sasa.
Na inawezekana labda umeoa au umeolewa kwa kijana ambaye hana mzigo na wazazi wake kabisa, kila mtu anaishi kivyake vyake kama simba porini, suala la kusaidia wazazi hana ndani ya moyo wake. Wewe umekuwa na huo mzigo, wazazi wako wamekulea, umefika mahali umeanza kazi, sasa na wewe unawatunza hatua kwa hatua, siku unaolewa yule baba anasema basi usiwatunze tena, - fikiri hilo.
Litakuwa linakuumiza kila siku jinsi wazazi wako wanavyopata shida. Utafika mahali utakuwa unachukua vitu kisiri siri unapeleka kwa wazazi, na hiyo ina shida yake pia. Kwa hiyo kabla hujakubali kusema mimi nataka kuolewa, fikiri kwanza na kuomba, maana ndoa inakwenda kukubadilishia mambo yako mengi.
Ni swali muhimu sana lakujiuliza wewe mwenyewe, uko tayari, maana yake umefika mahali hali yako ya ndani na nje, inakuruhusu kuoa au kuolewa? Uko tayari kuoa au kuolewa? Umefika mahali pa namna hiyo?. Wengine wanasema huyu ni mtoto, lakini unajua pamoja na kwamba ni mtoto, ni vizuri kujua kama uko tayari kiumri. Lakini ninapozungumzia hapa juu ya utayari wa kuoa au kuolewa, sizungumzii tu habari za miaka, bali ninazungumzia habari za hali yako ya ndani.
Nimeona kuna mtu mwingine ana miaka arobaini, lakini kwa kweli hayuko tayari kukaa na mwanamke, ndani yake, mawazo yake na kufikiri kwake, hayuko tayari kukaa na mwanamke, hawajibiki hata yeye mwenyewe juu yake mwenyewe. Wengine hata wana miaka hamsini, lakini ana hali kama hii. Nimeona akinadada hata wana miaka arobaini na tano, hayuko tayari kuolewa, maana akiolewa ni shida tu.
Nilienda mahali fulani, nikakuta dada ana umri mkubwa tu, lakini wakati wa maombi hakusema kama anataka tuombe ili aolewe. Nikaona ngoja nimuulize labda anaona aibu kusema hitaji hili kwa sababu umri umesogea, nikamwambia “hutaki tuombe uolewe”? Akasema, “hapana, sitaki kuolewa” (Na alikuwa ana umri wa miaka kama arobaini na zaidi). Nikamuuliza, “kwa nini”. Akasema, “kwa sababu sitaki kuomba ruhusa kwa mwanaume ninapotaka kutumika”. Nikamuuliza unafanya kazi, akasema, “ndio”.
Nikamwambia, “unapokwenda kumtumikia Mungu huwa unafanyaje, - unaomba ruhusa au unatoroka huko kazini?” Akasema, “ninaomba ruhusa”. Nikwamwambia, “kwa nini unaona ni rahisi kuomba ruhusa kwa mwajiri wako na unaona taabu kuomba ruhusa kwa mume wako?” Alishindwa kujibu hilo swali. Nikamwambia tatizo lako ni kubwa kuliko unavyo fikiri.
Unaweza ukaona kabisa ya kwamba, huyu mtu hayuko tayari kuolewa, wala msijaribu kumlazimisha aoelewe – pamoja na kwamba umri wake ni mkubwa. Usijaribu kumsukuma kwenye maamuzi ya kuolewa maana hayuko tayari kuolewa, akiingia kwenye ndoa atakwenda kuleta shida tu,
Mwingine unakuta ni msichana, wazazi wake ndio wanamtegemea karibu katika kila kitu. Mimi ninakuambia kabla hujafikiria kuoa au kuolewa, fikiria hilo swali. Kwa sababu ukiishaolewa tu biblia inakuambia wasahau watu wa nyumbani mwa wazazi wako (Zaburi 45:10). Sasa haimaanishi usiwasaidie, ila maana yake ni kwamba huwezi ukawasaidia tena ‘moja kwa moja’ kama ulivyokuwa unawasaidia zamani. Ni vitu lazima ujadiliane na mume wako juu ya kuwasaidia wazazi wenu wa pande zote mbili – maana mna mipango yenu sasa.
Na inawezekana labda umeoa au umeolewa kwa kijana ambaye hana mzigo na wazazi wake kabisa, kila mtu anaishi kivyake vyake kama simba porini, suala la kusaidia wazazi hana ndani ya moyo wake. Wewe umekuwa na huo mzigo, wazazi wako wamekulea, umefika mahali umeanza kazi, sasa na wewe unawatunza hatua kwa hatua, siku unaolewa yule baba anasema basi usiwatunze tena, - fikiri hilo.
Litakuwa linakuumiza kila siku jinsi wazazi wako wanavyopata shida. Utafika mahali utakuwa unachukua vitu kisiri siri unapeleka kwa wazazi, na hiyo ina shida yake pia. Kwa hiyo kabla hujakubali kusema mimi nataka kuolewa, fikiri kwanza na kuomba, maana ndoa inakwenda kukubadilishia mambo yako mengi.
MAANDALIZI YA KUOWA AU KUOLEWA
Ndowa inakuunganisha na kukuingizakatika familia nyingine mya.
Unafahamu watu wengi sana wakioa au kuolewa wanafikiria tu mahusiano ya wao wenyewe tu; na hii ni hatari sana. Kwa sababu unapooa unaingia kwenye undugu na familia nyingine kabisa tofauti, na sio mahusiano ya kwenu tu wawili. Ninyi ni kigezo tu cha kuunganisha hizo familia mbili, lakini mkiishaoana hizo familia zenu mbili ni ndugu kuanzia wakati huo.
Ndio maana unapofika unataka kuoa au kuolewa, sio suala la kumtazama kijana tu, au kumtazama msichana yeye mwenyewe tu; kwa mfano alivyosoma, lakini ni lazima pia utazame na hali ya familia yake ili ujue unajiingiza kwenye familia ya namna gani. Unapofika kwenye masuala ya namna hiyo kuna vitu vingi sana vya kuangalia.
Unaweza ukaingia kwenye familia ambayo ni wavivu, mimi ninakuambia jasho litakutoka ukioa msichana wa namna hiyo; au ukipata kijana toka kwenye familia ya namna hiyo. Itakuwa kazi sana kumshawishi mwenzako juu ya kujishughulisha na maisha. Maana inategemea; kwa kuwa unaweza kuoa msichana hata kusonga ugali hajui. , kwa mfano kwetu tuna wasichana watatu, tumezaliwa watoto 6 wa kiume 3, wasichana 3
Lakini mama yetu alikuwa na bidii ya kutufundisha wote kufanya kila kitu kwa bidii sana, alitufundisha kupika, alitufundisha kulima, kufanya biashara ndogo ndogo Kwa hiyo nilijifunza kwanza kutoka kwa wazazi wangu hayo yote.
Sasa wengine hawapati nafasi ya namna hiyo kwa sababu ya wazazi kuachana au kutokuwa na uhusiano mzuri na familia zao, na ni mbaya zaidi haswa kwa wasichana. Mungu amenipa nafasi ya kuwa na mtoto mmoja wa kike na itakuwa ni aibu kwetu kama wazazi, ikafika wakati wanaingia katika ndoa zao na hawajui kupika ni aibu kwetu sisi wazazi japo wengi wazazi hawalikubali hilo jambo lolote baya au la aibu litakalo onekana kwa binti anayeolewa ni aibu kwa wazazi; wengine baada ya kutegea kumlea mtoto katika maadili,mtoto akipata mme wa kumwoa anawapa wa mama eti wamfundishe kwenda kuishi na mwanaume, kinachonishangaza wao walimu wanaofundisha, karibia ya wote hawana ndowa,sasa watafundisha kitu gani,
Kama umechelewa kumfundisha mtoto wako ni heri ukampeleka kwa watumishi wa Mungu,ambao una uhakikanao kwa matendo yao,maana wingine wanajiita tu ni watumishi wa Mtungu ila haijulikani hata ailiyewatuma kwasababu ya matendo yao, kwa hiyo lazima uwafundishe watoto wako wajue kupika hata wakiume maana ipi siku wataendakuanza maisha yao kuishi bila wazazi, . Maana kwa kujua hilo anaonyesha anatoka familia ya namna gani, na imemlea kwa namna gani! Sikatai wewe kumuweka mtumishi wa kazi za ndani nakini na wewe pia kama mzazi simama nafasi yako ya mzazi,
Unaweza ukafikiri unamlea mtoto wako vizuri kwakuto mshugulisha ila utakuwa unamuumza bila yaw ewe kufahamu, maana siku hizi kuna shida ya kuwa na wafanya kazi majumbani mwetu. Ukishakuwa na mfanyakazi nyumbani basi watoto wengine hawafanyi kitu chochote, wakati mwingine wanakula chakula na wanaacha sahani hapo hapo mezani hawafuti meza hawatandiki kitanda.
Kuna watoto wengine inakuwa mpaka yuko sekondari hawezi kufua nguo zake. Kwa kuwa nyumbani kama hakuna wa kumfulia basi kuna mashine za kufulia. Huko unakokwenda kuolewa inawezekana hata mashine ya kufulia hawajawahi kuiona wala kuisikia! Unafika pale na unauliza mashine iko wapi, wanakuambia yakufanyia nini au ipi, - ya kusagia mahind ipo pale mtaa wa pili Maana ndio wanayoijua kuwa ndio mashine!
Hujui hata namna ya kushika kioo cha taa ya chemli wala namna ya kuiosha kule ndani lile vumbi likaondoka. Inawezekana mwingine umezaliwa kwenye nyumba yenye umeme, lakini utakapokuwa katika ndoa unaenda kwenye nyumba ambayo haina hata umeme, unafika kule na unashangaa kweli maana hujui hata namna kuwasha taa ya chemli! Kwa hiyo tunawaambia vijana suala la kujifunza hivi vitu sio suala la kuchagua, hata kama kuna mtu pale nyumbani wa kuwasaidia, ni lazima wajue kufanya kazi! Zamani mimi niliwasikia wazazi wangu wakisema kijana alikuwa hapati mchumba bilaya kuonyesha nizamu na bidii ya kufanya kazi acha wale wanaotoroka kijijini wanakuja mjini maisha yakiwaonea kidogo tu basi wanajirahisisha na kujipeleka wenyewe kwenye ndowa,ndowa siyoyakujipeleka ni maisha yako hivyo ukikosea unakosea kuishi unaweza ukafa muda wako bado kabisa,
Nilienda kwenye mkoa mmoja wakasema, sisi ukitaka kuoa kwenye nyumba ya mtu, ukitaka kujua huyo msichana amelelewa vizuri au vibaya wakasema usimtazame alivyovaa. Badala yake wanafika kwenye uwanja wa nyumba ya wazazi wake, na wanaangalia ile barabara inayokwenda nyumbani kwao, na wakiikuta chafu, basi wanajua huyu msichana ni mchafu, hawahangaiki tena kuja kuzungumza, wanajua hapa kama tunaamua kuoa tujue tunacho oa, huyu msichana ni mchafu!
Ukienda kuoa kwenye familia nyingine utakuta wanasumbuliwa na ugonjwa wa kurithi, na usipojua kitu cha kufanya unaweza ukapata shida sana. Lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba, uamuzi wa kuoa au kuolewa unakuingiza kwenye familia nyingine kabisa, na inaunganisha hiyo familia yao na familia yako; kwa hiyo hayo sio maamuzi madogo. Kumbuka unapooa au kuolewa unawaingiza watu katika famila ambazo kama usipokuwa mwangalifu inaweza ikaleta shida sana, lakini pia inaweza ikaleta baraka!.
Ukienda kuoa kwenye familia nyingine utakuta wanasumbuliwa na ugonjwa wa kurithi, na usipojua kitu cha kufanya unaweza ukapata shida sana. Lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba, uamuzi wa kuoa au kuolewa unakuingiza kwenye familia nyingine kabisa, na inaunganisha hiyo familia yao na familia yako; kwa hiyo hayo sio maamuzi madogo. Kumbuka unapooa au kuolewa unawaingiza watu katika famila ambazo kama usipokuwa mwangalifu inaweza ikaleta shida sana, lakini pia inaweza ikaleta baraka!.
Unafahamu watu wengi sana wakioa au kuolewa wanafikiria tu mahusiano ya wao wenyewe tu; na hii ni hatari sana. Kwa sababu unapooa unaingia kwenye undugu na familia nyingine kabisa tofauti, na sio mahusiano ya kwenu tu wawili. Ninyi ni kigezo tu cha kuunganisha hizo familia mbili, lakini mkiishaoana hizo familia zenu mbili ni ndugu kuanzia wakati huo.
Ndio maana unapofika unataka kuoa au kuolewa, sio suala la kumtazama kijana tu, au kumtazama msichana yeye mwenyewe tu; kwa mfano alivyosoma, lakini ni lazima pia utazame na hali ya familia yake ili ujue unajiingiza kwenye familia ya namna gani. Unapofika kwenye masuala ya namna hiyo kuna vitu vingi sana vya kuangalia.
Unaweza ukaingia kwenye familia ambayo ni wavivu, mimi ninakuambia jasho litakutoka ukioa msichana wa namna hiyo; au ukipata kijana toka kwenye familia ya namna hiyo. Itakuwa kazi sana kumshawishi mwenzako juu ya kujishughulisha na maisha. Maana inategemea; kwa kuwa unaweza kuoa msichana hata kusonga ugali hajui. , kwa mfano kwetu tuna wasichana watatu, tumezaliwa watoto 6 wa kiume 3, wasichana 3
Lakini mama yetu alikuwa na bidii ya kutufundisha wote kufanya kila kitu kwa bidii sana, alitufundisha kupika, alitufundisha kulima, kufanya biashara ndogo ndogo Kwa hiyo nilijifunza kwanza kutoka kwa wazazi wangu hayo yote.
Sasa wengine hawapati nafasi ya namna hiyo kwa sababu ya wazazi kuachana au kutokuwa na uhusiano mzuri na familia zao, na ni mbaya zaidi haswa kwa wasichana. Mungu amenipa nafasi ya kuwa na mtoto mmoja wa kike na itakuwa ni aibu kwetu kama wazazi, ikafika wakati wanaingia katika ndoa zao na hawajui kupika ni aibu kwetu sisi wazazi japo wengi wazazi hawalikubali hilo jambo lolote baya au la aibu litakalo onekana kwa binti anayeolewa ni aibu kwa wazazi; wengine baada ya kutegea kumlea mtoto katika maadili,mtoto akipata mme wa kumwoa anawapa wa mama eti wamfundishe kwenda kuishi na mwanaume, kinachonishangaza wao walimu wanaofundisha, karibia ya wote hawana ndowa,sasa watafundisha kitu gani,
Kama umechelewa kumfundisha mtoto wako ni heri ukampeleka kwa watumishi wa Mungu,ambao una uhakikanao kwa matendo yao,maana wingine wanajiita tu ni watumishi wa Mtungu ila haijulikani hata ailiyewatuma kwasababu ya matendo yao, kwa hiyo lazima uwafundishe watoto wako wajue kupika hata wakiume maana ipi siku wataendakuanza maisha yao kuishi bila wazazi, . Maana kwa kujua hilo anaonyesha anatoka familia ya namna gani, na imemlea kwa namna gani! Sikatai wewe kumuweka mtumishi wa kazi za ndani nakini na wewe pia kama mzazi simama nafasi yako ya mzazi,
Unaweza ukafikiri unamlea mtoto wako vizuri kwakuto mshugulisha ila utakuwa unamuumza bila yaw ewe kufahamu, maana siku hizi kuna shida ya kuwa na wafanya kazi majumbani mwetu. Ukishakuwa na mfanyakazi nyumbani basi watoto wengine hawafanyi kitu chochote, wakati mwingine wanakula chakula na wanaacha sahani hapo hapo mezani hawafuti meza hawatandiki kitanda.
Kuna watoto wengine inakuwa mpaka yuko sekondari hawezi kufua nguo zake. Kwa kuwa nyumbani kama hakuna wa kumfulia basi kuna mashine za kufulia. Huko unakokwenda kuolewa inawezekana hata mashine ya kufulia hawajawahi kuiona wala kuisikia! Unafika pale na unauliza mashine iko wapi, wanakuambia yakufanyia nini au ipi, - ya kusagia mahind ipo pale mtaa wa pili Maana ndio wanayoijua kuwa ndio mashine!
Hujui hata namna ya kushika kioo cha taa ya chemli wala namna ya kuiosha kule ndani lile vumbi likaondoka. Inawezekana mwingine umezaliwa kwenye nyumba yenye umeme, lakini utakapokuwa katika ndoa unaenda kwenye nyumba ambayo haina hata umeme, unafika kule na unashangaa kweli maana hujui hata namna kuwasha taa ya chemli! Kwa hiyo tunawaambia vijana suala la kujifunza hivi vitu sio suala la kuchagua, hata kama kuna mtu pale nyumbani wa kuwasaidia, ni lazima wajue kufanya kazi! Zamani mimi niliwasikia wazazi wangu wakisema kijana alikuwa hapati mchumba bilaya kuonyesha nizamu na bidii ya kufanya kazi acha wale wanaotoroka kijijini wanakuja mjini maisha yakiwaonea kidogo tu basi wanajirahisisha na kujipeleka wenyewe kwenye ndowa,ndowa siyoyakujipeleka ni maisha yako hivyo ukikosea unakosea kuishi unaweza ukafa muda wako bado kabisa,
Nilienda kwenye mkoa mmoja wakasema, sisi ukitaka kuoa kwenye nyumba ya mtu, ukitaka kujua huyo msichana amelelewa vizuri au vibaya wakasema usimtazame alivyovaa. Badala yake wanafika kwenye uwanja wa nyumba ya wazazi wake, na wanaangalia ile barabara inayokwenda nyumbani kwao, na wakiikuta chafu, basi wanajua huyu msichana ni mchafu, hawahangaiki tena kuja kuzungumza, wanajua hapa kama tunaamua kuoa tujue tunacho oa, huyu msichana ni mchafu!
Ukienda kuoa kwenye familia nyingine utakuta wanasumbuliwa na ugonjwa wa kurithi, na usipojua kitu cha kufanya unaweza ukapata shida sana. Lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba, uamuzi wa kuoa au kuolewa unakuingiza kwenye familia nyingine kabisa, na inaunganisha hiyo familia yao na familia yako; kwa hiyo hayo sio maamuzi madogo. Kumbuka unapooa au kuolewa unawaingiza watu katika famila ambazo kama usipokuwa mwangalifu inaweza ikaleta shida sana, lakini pia inaweza ikaleta baraka!.
Ukienda kuoa kwenye familia nyingine utakuta wanasumbuliwa na ugonjwa wa kurithi, na usipojua kitu cha kufanya unaweza ukapata shida sana. Lakini ninachotaka kukuambia ni kwamba, uamuzi wa kuoa au kuolewa unakuingiza kwenye familia nyingine kabisa, na inaunganisha hiyo familia yao na familia yako; kwa hiyo hayo sio maamuzi madogo. Kumbuka unapooa au kuolewa unawaingiza watu katika famila ambazo kama usipokuwa mwangalifu inaweza ikaleta shida sana, lakini pia inaweza ikaleta baraka!.
KABLA YA NDOWA LIPI UJIFUNZE?
mabadiliko unayotakiwa kuyafahamu kabla ya kuoa au kuolewa< Mvulana au binti)
NI VEMA UKIWA NA BIBLIA PEMBENI:
Mwanzo.2:24 anasema, “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili moja”. Ukiangalia (Zaburi.45:10-11) anasema, “Sikia binti utazame (maana yake anazungumza na msichana) utege sikio lako. Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako na mfalme atautamani uzuri wako, maana ndiye bwana wako naye umsujudie”.
Najua watu wengi sana wanataka waingie kwenye ndoa, waoe au waolewe, lakini uhusiano wao na wazazi wao usibadilike, haiwezekani. Biblia imeweka wazi kabisa, unataka kuoa, mwanamume lazima kwanza aachane na baba yake na mama yake, maana yake kuna mabadiliko. Kuna mabadiliko mahali pakuishi, kuna mabadiliko juu ya mtazamo wako wa kwanza wa maisha yako. Mke wako hawezi kuwa mama yako, na mume wako hawezi kuwa baba yako. Mke wako anakuwa mke wako na si mama yako. Mume wako anakuwa mume wako na si baba yako.
Na kabla hujafikia maamuzi ya namna hiyo - ukiingia kwenye ndoa, ndoa yako itakuwa ngumu. Maana inawezekana unaishi vizuri na wazazi wako, kiasi ambacho maamuzi yako yoyote unayofanya lazima ushirikiane nao, na hiyo ni hatua nzuri kabisa. Lakini ukiishaingia kwenye ndoa, mtu wa kwanza wakushirikiana naye ni mke wako kama umeoa, na ni mume wako kama umeolewa lakini, sio baba yako, sio mama yako.
Na wazazi wengine wasingetaka kuona kwamba unakuwa mbali nao kwa jinsi hii, wanataka waendeleze maamuzi yao na utawala wao waliokuwa nao juu yako mpaka kwenye ndoa yako, haiwezekani. Biblia inakataa. Sasa ukisoma ile Mwanzo unaweza ukafikiri ni wanaume tu wakioa ndio wanatakiwa watoke, waachane na wazazi wao, lakini Zaburi 45:10,11 inatuambia wazi kabisa, inasema, “Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Naye Mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie”.
Sasa haimaanishi usiwasalimie, haimanishi usiwasaidie, lakini ningekuwa nazungumza kwa kiingereza ningekuambia, “your priorities must change” lazima ubadilike jinsi ambavyo unaweka kipaumbele katika watu ulio nao.
Unapoamua kuolewa, wa kwanza sio baba yako wala sio mama yako, wa kwanza ni mume wako baada ya Yesu. Katika mahusiano ya kibinadamu anayekuja pale wa kwanza baada ya Yesu moyoni mwako ni mume wako. Ikiwa hujafikia maamuzi ya namna hii moyoni mwako basi bado hujafikia utayari wa kuolewa. Na ina madhara yake magumu. Maana biblia inasema, kabla hujawasahau watu wako na watu wa nyumba ya baba yako, mume wako hawezi kuutamani uzuri wako, ukitaka autamani uzuri wako lazima uwasahau kwanza watu wa nyumbani kwa wazazi wako.
Sasa kuna tofauti ya kupenda na kutamani. Kabla hujaolewa au kabla hujaoa huruhusiwi kutamani. Lakini ukiisha oa unaruhusiwa kutamani lakini mke wako tu. Ukiishaoa kutamani mke wako ruksa, na biblia imeweka vizuri kabisa, na ukiishaolewa kutamani mume wako ni ruksa. Lakini biblia imeweka utaratibu wa ajabu sana kwamba, ili mume amtamani mke wake, lazima mke wake awasahau kwanza watu wa nyumbani mwa wazazi wake. Hiki ni kigezo kigumu sana.
Ndio maana unaweza ukakuta mtu ana mke mzuri sana lakini hamtamani. Unaweza ukafikiri labda ni kwa kuwa hajajipamba vizuri; lakini hata kama atajipamba, atajikwatua kuanzia asubuhi mpaka jioni, - anaweza hata akatumia muda mwingi kwenye kioo kuliko kwenye maombi akijitengeneza, lakini bado mume wake asimtamani; kwa nini? Kwa sababu ndani yake hajaachia watu wa nyumba ya wazazi wake. Au watu wa nyumba ya baba yake wana nafasi kubwa moyoni kuliko mume wake.
Ni mabadiliko ambayo lazima uyatarajie, watu wengi sana huwa hawafikirii hayo, wanafikiri ni kitu rahisi. Unaweza sasa ukaelewa kwa nini watu wengine ikifika siku ile ya “send off”, yaani ya kum’send’ msichana ‘off’ asikae tena nyumbani kwa baba yake, hiyo siku ni ngumu sana kwa wazazi. Kwa sababu wanajua, wanaagana na msichana wao, mahusiano yao waliokuwa nayo toka mwanzoni, tangu alipozaliwa, alipokuwa tumboni mpaka wakati huo yanabadilishwa, yanajengwa mengine, sasa anakwenda kuwa mke wa mtu, hawawezi tena kuingilia maamuzi juu yake, amefunga agano mahali pengine.
Unakuta siku hiyo wazazi wengine wanalia, unakuta vijana wengine wanalia, wasichana wengine wanalia. Usije ukafikiri ni kitu rahisi. Ndani ya nafsi kuna vitu vinaachana, kati ya wazazi na wale watoto wanaoana.
NI VEMA UKIWA NA BIBLIA PEMBENI:
Mwanzo.2:24 anasema, “Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili moja”. Ukiangalia (Zaburi.45:10-11) anasema, “Sikia binti utazame (maana yake anazungumza na msichana) utege sikio lako. Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako na mfalme atautamani uzuri wako, maana ndiye bwana wako naye umsujudie”.
Najua watu wengi sana wanataka waingie kwenye ndoa, waoe au waolewe, lakini uhusiano wao na wazazi wao usibadilike, haiwezekani. Biblia imeweka wazi kabisa, unataka kuoa, mwanamume lazima kwanza aachane na baba yake na mama yake, maana yake kuna mabadiliko. Kuna mabadiliko mahali pakuishi, kuna mabadiliko juu ya mtazamo wako wa kwanza wa maisha yako. Mke wako hawezi kuwa mama yako, na mume wako hawezi kuwa baba yako. Mke wako anakuwa mke wako na si mama yako. Mume wako anakuwa mume wako na si baba yako.
Na kabla hujafikia maamuzi ya namna hiyo - ukiingia kwenye ndoa, ndoa yako itakuwa ngumu. Maana inawezekana unaishi vizuri na wazazi wako, kiasi ambacho maamuzi yako yoyote unayofanya lazima ushirikiane nao, na hiyo ni hatua nzuri kabisa. Lakini ukiishaingia kwenye ndoa, mtu wa kwanza wakushirikiana naye ni mke wako kama umeoa, na ni mume wako kama umeolewa lakini, sio baba yako, sio mama yako.
Na wazazi wengine wasingetaka kuona kwamba unakuwa mbali nao kwa jinsi hii, wanataka waendeleze maamuzi yao na utawala wao waliokuwa nao juu yako mpaka kwenye ndoa yako, haiwezekani. Biblia inakataa. Sasa ukisoma ile Mwanzo unaweza ukafikiri ni wanaume tu wakioa ndio wanatakiwa watoke, waachane na wazazi wao, lakini Zaburi 45:10,11 inatuambia wazi kabisa, inasema, “Sikia, binti, utazame, utege sikio lako, Uwasahau watu wako na nyumba ya baba yako. Naye Mfalme atautamani uzuri wako, Maana ndiye bwana wako, nawe umsujudie”.
Sasa haimaanishi usiwasalimie, haimanishi usiwasaidie, lakini ningekuwa nazungumza kwa kiingereza ningekuambia, “your priorities must change” lazima ubadilike jinsi ambavyo unaweka kipaumbele katika watu ulio nao.
Unapoamua kuolewa, wa kwanza sio baba yako wala sio mama yako, wa kwanza ni mume wako baada ya Yesu. Katika mahusiano ya kibinadamu anayekuja pale wa kwanza baada ya Yesu moyoni mwako ni mume wako. Ikiwa hujafikia maamuzi ya namna hii moyoni mwako basi bado hujafikia utayari wa kuolewa. Na ina madhara yake magumu. Maana biblia inasema, kabla hujawasahau watu wako na watu wa nyumba ya baba yako, mume wako hawezi kuutamani uzuri wako, ukitaka autamani uzuri wako lazima uwasahau kwanza watu wa nyumbani kwa wazazi wako.
Sasa kuna tofauti ya kupenda na kutamani. Kabla hujaolewa au kabla hujaoa huruhusiwi kutamani. Lakini ukiisha oa unaruhusiwa kutamani lakini mke wako tu. Ukiishaoa kutamani mke wako ruksa, na biblia imeweka vizuri kabisa, na ukiishaolewa kutamani mume wako ni ruksa. Lakini biblia imeweka utaratibu wa ajabu sana kwamba, ili mume amtamani mke wake, lazima mke wake awasahau kwanza watu wa nyumbani mwa wazazi wake. Hiki ni kigezo kigumu sana.
Ndio maana unaweza ukakuta mtu ana mke mzuri sana lakini hamtamani. Unaweza ukafikiri labda ni kwa kuwa hajajipamba vizuri; lakini hata kama atajipamba, atajikwatua kuanzia asubuhi mpaka jioni, - anaweza hata akatumia muda mwingi kwenye kioo kuliko kwenye maombi akijitengeneza, lakini bado mume wake asimtamani; kwa nini? Kwa sababu ndani yake hajaachia watu wa nyumba ya wazazi wake. Au watu wa nyumba ya baba yake wana nafasi kubwa moyoni kuliko mume wake.
Ni mabadiliko ambayo lazima uyatarajie, watu wengi sana huwa hawafikirii hayo, wanafikiri ni kitu rahisi. Unaweza sasa ukaelewa kwa nini watu wengine ikifika siku ile ya “send off”, yaani ya kum’send’ msichana ‘off’ asikae tena nyumbani kwa baba yake, hiyo siku ni ngumu sana kwa wazazi. Kwa sababu wanajua, wanaagana na msichana wao, mahusiano yao waliokuwa nayo toka mwanzoni, tangu alipozaliwa, alipokuwa tumboni mpaka wakati huo yanabadilishwa, yanajengwa mengine, sasa anakwenda kuwa mke wa mtu, hawawezi tena kuingilia maamuzi juu yake, amefunga agano mahali pengine.
Unakuta siku hiyo wazazi wengine wanalia, unakuta vijana wengine wanalia, wasichana wengine wanalia. Usije ukafikiri ni kitu rahisi. Ndani ya nafsi kuna vitu vinaachana, kati ya wazazi na wale watoto wanaoana.
KUOKOKA NI NINI?,,,
Hakuna wokovu katika mwingine:
“kuokoka maana yake halisi kwanza ninapenda ufahamu siyo Dini wala thehebu fulani,bali kuokoka ni kuokolewa kutoka katika hatari,sasa mtu anapookolewa kutoka katika hatari ya kwenda jehanamu kwaajili ya maovu akipata neema ya uokovu huo akatubu thambi zake zote na kuziacha basi huyo anaweza kusema ameokoka,ndiyo maana wengi unaowasikia kuwa wameokoka,kwanza wanakuwa na furaha sana,kwa kunusurika na jehanamu,
pia fahamu hili hapa duniani kuokoka kupo acha wale walioshindwa kuelewa,na anayeweza kuokowa ni mmoja tu, hayupo mwingine,awe ni kiongozi wako wa thehebu au mtume,nabii hayopo mwenye uwezo wakuokowa,wala jina lenye nguvu na mamlaka zaidi ya moja tu
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” (Matendo ya Mitume 4:12).
“Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao” (Mathayo 1:21).
“Bali wote waliompokea (Yesu Kristo) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake, waliozaliwa si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu” (Yohana 1:12 – 13)
“Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani, maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, kila atakayeliitia jina la Bwana (Yesu Kristo) ataokoka” (Warumi 10:12 – 13). Hivyo kwa siku za leo tungesema hakunatofauti ya mchaga na msukuma au nakabila lolote huu ni mfano tu,wote wanahitajika kuokolewa na mmoja tu Yesu kristo mwana wa Mungu,
“kuokoka maana yake halisi kwanza ninapenda ufahamu siyo Dini wala thehebu fulani,bali kuokoka ni kuokolewa kutoka katika hatari,sasa mtu anapookolewa kutoka katika hatari ya kwenda jehanamu kwaajili ya maovu akipata neema ya uokovu huo akatubu thambi zake zote na kuziacha basi huyo anaweza kusema ameokoka,ndiyo maana wengi unaowasikia kuwa wameokoka,kwanza wanakuwa na furaha sana,kwa kunusurika na jehanamu,
pia fahamu hili hapa duniani kuokoka kupo acha wale walioshindwa kuelewa,na anayeweza kuokowa ni mmoja tu, hayupo mwingine,awe ni kiongozi wako wa thehebu au mtume,nabii hayopo mwenye uwezo wakuokowa,wala jina lenye nguvu na mamlaka zaidi ya moja tu
Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo” (Matendo ya Mitume 4:12).
“Naye atazaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu, maana, yeye ndiye atakayewaokoa watu wake na dhambi zao” (Mathayo 1:21).
“Bali wote waliompokea (Yesu Kristo) aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake, waliozaliwa si kwa damu, wala si kwa mapenzi ya mwili wala si kwa mapenzi ya mtu, bali kwa Mungu” (Yohana 1:12 – 13)
“Kwa maana hakuna tofauti ya Myahudi na Myunani, maana yeye yule ni Bwana wa wote, mwenye utajiri kwa wote wamwitao; kwa kuwa, kila atakayeliitia jina la Bwana (Yesu Kristo) ataokoka” (Warumi 10:12 – 13). Hivyo kwa siku za leo tungesema hakunatofauti ya mchaga na msukuma au nakabila lolote huu ni mfano tu,wote wanahitajika kuokolewa na mmoja tu Yesu kristo mwana wa Mungu,
Subscribe to:
Posts (Atom)