WAZAZI HAWAJAPITWA NA WAKATI:

Mwawado's Avatar
True friends...with in Red clothes for love. Kuishi bila baraka za wazazi ni Hatari sana kuna sababu gani ya wewe kuwatharau wazazi wako, huwezi kukumbuka hata kidogo vile alivyokuwa anakuangaikia kukuongesha kulima vibaruwa ili wewe upate kuishi wakati mwingine alitharaulika kwakuomba misaada kwaajili yako baba akajitahidi kulipia kila kilicho hitajika ili wewe upate kufurahia ukajibiwa maswali yako yote hata yale yasiyoya kimsingi ili wewe ufurahi sasa umemaliza masomo au umepata mali unawatharau wazazi kisa unaiga utamaduni wa wenzetu wao tangu awali wameumbwa hivyi na wamelelewa hivyo upo utaratibu mwingine watu wanaufuta kwakisingizio cha maendeleo kwama hizo mila hatuziitaji lakini uliza  kwa nini wazazi wetu walifanikiwa kuishi umri mkubwa moja wapo ya utamaduni wao uliwasaidia sana kwa mfano siku za leo mavazi yanayovaliwa na vijana wetu siyakutembela barabarani labda ni kwaajili ya wana ndowa tu,au kupumzikia ndani wao wanafanya ndiyo mitindo, ukitaka kukosana nao fuatilia au uliza hatakama ni kwa maana nzuri lazima yataanza mengine makubwa matusi,kwamba mzazi amepitwa na wakati,
yeye amezaliwa kabla yako miaka 20 iliyopita na sasa mnaishi wote je? ni nani aliyepitwa na wakati kama siyo wewe tukubali kuonywa ndugu zangu, kuna matendo mengine tunawafanyia wazazi tunawaachia kilio wakati wote mara nyingine mzazi anapigwa na mtoto ati mtoto anamwambia mzazi hana adabu, au angechelewa angemzaa,hiyo ni laana ya wazi kabisa kufanya hivyo wengine hawafanikiwi kimaisha kwasababu hiyo ya kuzarau wazazi,unaweza kutofanikiwa au kuchukiwa na watu na Mungu pia kwa kuwauthi wazazi tuwapende wazazi jamani pia utamaduni wa wenzetu usitubadilishie wetu,

mbona wakija kwetu huwa wanatuiga inamaanisha tuna fanya vizuri kwanzia kuvaa kwetu kula kwetu ila nikujisahau tu sasa ni jukumu lletu sote kukumbushana,wengine anatapanya mali na ovyo wazazi wanataabika huko kijijini wanakufa njaa kwanini usipate mathara ni hatari unaweza kuzuwa matatizo ambayo huwezi juwa yameanzia wapi,je wewe ukibebeshwa mtoto mgongoni na kuni kichwani jembe mkononi utaweza? je umewahi kumubeba mtoto wako mara ngapi ukatembea naye kwa miguu kilomita 5 yu ukasikia uzito wake.
uwapende wazazi kama kuna namna ya kuwasaidia tuwasaidie hizo ni baraka za kwanza kabisa maana wao ndio walio kuleta hapa duniani,,,,,,

KUKOSA TUMAINI NI HATARI SANA:


High ropes team building KUKOSA TUMAINI NI UGONJWA HATARI SANA:
Kukosa tumaini na muelekeo wa maisha yako ni hatari sana, maana unaweza kuchukuwa maamuzi ambayo hata wewe mwenyewe hukutarajia kuyafanya,unaweza kukimbia hata pasipo kukimbizwa maana huna tumaini huna ujasiri, Na kaitaka maisha ukichaguwa au kuruhusu kuishi maisha ya kukata tamaa huwezi kupata suluwisho la mahitaji yako tena maana kilakitu unakiona kama umekishindwa,

hali ya kukata tamaa inaweza kuathiri mambo mengi sana maisha yako,kutoendeleza maendeleo yako,inaweza kuathiri ndowa yako, afya yako,biashara yako au kazi yako,n.k matokeo yake hali inaweza kuwa mbaya na kusababisha matatizo mengine kuibuka bila wewe kutarajia, na wengine kama hawakushahuriwa vizuri hufikia hata hatuwa ya kujiua, kuwa na tabia sugu na hata mara nyingine unaweza kujikataa wewe mwenyewe, Habari njiema ni hizi juu ya wewe unayepitia katika hali hii, hali yako ya awali ukizingatia haya inaweza kukurudia tena, na ukawa na Tumaini,amani na upendo kama wa awali

Neno la Mungu liwazi kwa yeye aliyetayari kuliishi vile linavyoagiza  Zaburi 51:8 unifanyie kusikia furaha na shangwe,mifupa iliyopondeka ifurahi wakati wote wa maisha yako unapopitia hali ngumu kisha Mungu akakushindia  hiyo hali kinachofuata siku zote ni furaha, upo mfano wa Mama mjaa mzito akikaribia kujifunguwa anauhisi uchungu mkubwa sana kwa mjibu wa wazazi,ila akifanikiwa kujifunguwa salama huwa anakuja hisi furaha ya mda mrefu,

upo mfano mwingine mmoja kwa timu za mpira zikiwa zinapambana kisha moja ikafungwa iliyofungwa huwa na huzuni,ila ikijarudisha ushindi mikononi mwao tena huwa hushangilia kuliko wale wa awali, heri mwisho wa jambo kuliko mwanzo,wa jambo  jambo usiloliweza  wewe kulifanya yeye Mungu analiweza, kuna mambo mengine huwezi kujisaidia wewe wala mwanadamu yeyote  ndugu yangu unaye teseka kwa namna yeyote ile iwe katika ajira au katika uongozi,ndowa uchumba, huo kwako ni mzigo mkubwa sana unaona ila kwake yeye ana sema

Njooni kwangu ninyi nyote msumbukao na wenye kuelemewa na mizigo nami nitawapumzisha, awezaye kupumzisha ni yesu kristo  pekee, wengine wote ni mashabiki tu ukishindwa wanachekelea ukishinda wana shangaa hao wapo tu, na wala usitafute njia zako wewe mwenyewe wala usimpangie au kumlazimisha Mungu atumie njia unayoitaka wewe,

yupo Bwana mmoja katika biblia anafahamika sana kama Ibrahimu baba wa imani lakini kama mwanadamu,
baada ya kuona umri wake umekwenda yeye na mkewe wakashahuriana kutumia njia zao wenyewe kupata mtoto kupitia kwa mfanyakazi wao, wakaacha kusubiria mtoto wa ahadi  ashukuriwe Mungu wetu asiyedanganya kama wanadamu wanavyo danganya akawapa mtoto uzeeni ambavyo kwaakili ya mwanadamu wa kawaida asingeweza kuamini kilichofanyika acha Mungu akupe suluwisho acha kutafuta suluwisho wewe mwenyewe, inaendelea,,,,

Followers