MAHUBIRI YA MAFANIKIO BILA TOBA YANACHOCHEA TAMAA MBAYA,

. Wachungaji wana njaa ya kujifunza jinsi ya kuongeza wahudhuriaji katika makanisa yao na Si kuwafundisha watu jinsi ya kuishi Maisha matakatifu, na mara nyingi ni wepesi kupokea ushauri wa wachungaji wa kigeni kutoka inchi kama marekani Kimarekani naijeria na ninginezo nyingi, wenye makanisa makubwa, wanaodhaniwa kuwa wamefanikiwa kwa sababu ya ukubwa wa majengo yao na wingi wa watu wanaoabudu kwenye ibada zao siku za Jumapili.


Ila, wale wenye utambuzi kidogo hutambua kwamba ukubwa wa wahudhuriaji na jengo si alama ya ubora wa huduma ya kufanya watu kuwa wanafunzi. Makanisa mengine ya Marekani yamekua kwa sababu ya mafundisho yenye kuvutia, ambayo ni upotoshaji wa kweli za KiBiblia.

 Kinacho sikika kila siku ni kwamba wachungaji wengi wa Kimarekani wanaamini na kuhubiri kwamba mtu akiisha okoka tu, hawezi kupoteza wokovu wake hata akiamini nini au akiishi vipi hilo ni kukwepa ukweli wa Mungu imeandikwa aliyesimama Aangalie asije akaanguka ukianguka moja kwa moja wewe unakuwa umefarakana na mungu yaani umepoteza ufalme wa Mungu.

Pia, wachungaji wengi wa Kimarekani huhubiri Injili iliyotiwa maji kuhusu neema isiyo na gharama, sihitaji kuwazungu sana iwe kama ninawasema lah! Bali wito wangu kwako msikilize Roho mtakatifu zaidi kuliko Mwanadamu wanakuwa wakiwaongoza watu kudhani kwamba wanaweza kuingia mbinguni pasipo utakatifu.

Kuna wengi pia wanaohubiri Injili ya mafanikio, wakichochea roho ya tamaa katika watu ambao dini ni njia ya kujipatia hazina zaidi za kujiwekea hapa duniani. Hao ni wachungaji ambao mbinu zao za ukuaji wa kanisa hazifai kuigwa.Yapo mazuri na mema mengi kama kusaidia yatima wajane masikini wasiyojiweza na mengineyo siyo yakuwa watamukia kupata vitu ambavyo ujaongozwa na Mungu kuwaambia unaweza kukaharibu kundi la Mungu badala ya kulijenga,

Unapo mtamukia mtu atapata gari leo au wiki hii au mwezi huu au mwaka huu na yeye akapokea na unajuwa hana hata kazi wala kibaruwa wala shamba lakulima,wala hajafuga hata njiwa  mimi kwa nafasi yangu ya ushahuri kama Mungu hajakushuhudia usichochee tamaa kwa watu inawezekana alisha ishinda thambi lakini kwa ushawishi wako wa kuwafundisha wataokota hela na kujenga majumba na kununuwa magari mazuri mazuri ikiwa hata basikile hana inaweza ikasababisha watu wakafanya thambi ya tamaa na hata kujikuta wanaingia katika mashindano wao kwa wao na kufikia katika wizi au kama ni mwanamke anajikuta ameharibu ndoa kwakutaka asiyokuwa na uwezo nayo kisa ameambiwa avae kama wengine au aishi kama wengine watu wafundishwa namna ya kuishi maisha matakatifu

Ili mungu aseme nawao wenyewe kuhusu baraka zao hizo na hata kama zikipitia kwako basi awe na yeye anaziona katika ulimwengu wa ki-Roho siyo mtu bado ni mchanga hajafundishwa kuikana Dunia na maovu yake gafla anakumbana na matangazo ya utajiri utajiri bila Mungu si kitu usalama wa kwaza kwa mwanadamu ni kuishi na Mungu
ukisoma kwa upana sana Baathi ya vitabu juu ya mada ya ukuaji wa kanisa, nami nashindwa kutoa uamuzi juu ya vitabu hivyo kabisa .

Vingi vina mbinu na ushauri ambao kwa kiwango fulani ni wa KiBiblia, na hivyo vinafaa kusomwa. Lakini karibu vyote vina misingi kwenye taratibu za makanisa jengo – taratibu zenye umri wa miaka elfu na mia saba hivi – badala ya utaratibu wa KiBiblia. Basi, lengo lake si kuujenga mwili wa Kristo kwa kuwaongeza wanafunzi na wenye kufanya watu kuwa wanafunzi, bali ni kujenga makanisa jengo ya kipekee, ambayo kila mara yatahitaji majengo makubwa zaidi, watumishi wenye taaluma za hali ya juu pamoja na mipango aina hiyo, na mtiririko wa uongozi kama wa shirika au kampuni, badala ya familia ya wana wa Mungu.


Kuna mbinu za kisasa za ukuaji wa kanisa ambazo zinatosha ushauri kwamba, kwa ajili tu ya kupata washirika wengi, ibada ziwe za kuvutia kwa ajili ya watu wasiotaka kumfuata Yesu. Zinashauri kwamba kuwe na mahubiri mafupi, yasiyokuwa na maneno makali yaani ya kukemea Dhambi ya kuudhi, na ibada tulivu, na mambo mengi ya kijamii, na fedha zisitajwe kwaajili ya matoleo, na kadhalika.

Hii haisababishi kuzaa wanafunzi wanaojikana na kutii amri zote za Kristo. Husababisha watu wanaojiita Wakristo, wasioweza kutofautishwa na wana wa dunia, na ambao wanaelekea jehanamu kupitia barabara ile pana. Hiyo si mbinu ya Mungu ya kuwaleta watu Kwake bali ni ya Shetani ya kuliteka kanisa. Huo si “ukuaji wa kanisa” bali ni “ukuaji wa dunia ya yule muovu nah ii imewaumiza watumishi wengi sana, na wengine kufikia sehemu ya kupoteza uelekeo wa kazi ya Mungu, na Hata jina la Bwana likaazwa kutukanwa ovyo

Hukumu ya namna hii utaibebea wapi ndugu yangu?

KANISA ALILOLIACHA KRISTO YESU NI LIPI?

Hii  wakati mwingine inaweza kutusababishia hata sisi kupoteza kibali cha kuhudumu mbele za Mungu wetu wa Mbinguni,

Watu wengi wamekuwa wakiniuliza maswali mengi tofauti tofauti kila mara ninapokuwa na mazungumuzo na wao  ya kirafiki haswa kuhusiana na kazi ya Mungu aliyotuagiza kuifanya tuwapo hapa Duniani, napia inawezekana na wewe ukawa miongoni mwa wale wenyemaswali mbali mbali ya ki-Mungu usiogope kutuandikia uwe huru, Ndugu yangu Roho Mtakatifu yupo kwaajili ya kujibu maswali yanayowasumbuwa wanadamu,



Hapa kuna baathi ya maswali yaliyojibiwa mengine endelea kusoma safu nyingine hizo zinazo onekana hapo utayapata,


KANISA NI NINI? LENGO LA KANISA, UTAWALA WA KANISA, MWISHO: MUNGU ANATAKA NINI KWA VIONGOZI WA KANISA,


Hayo ndiyo utakayojifunza katika safu hii na haswa kwa wale ambao wameshazitambuwa huduma zao ni zipi, kwakifupi kabisa kanisa siyo jingo la mawe au matofali bali ni wewe maana Mungu anaabudiwa ndani yako, wakati unakuja watakao niabudu halisi wataniabudu mimi (Mungu) katika Roho na kweli


Ndugu yangu Roho haikai ndani ya jingo inakaa ndani ya mwanadamu ndiyo maana ninamaanisha kanisa ni Mtu yule aliyeamuwa kukatashahuri na kumkaribisha Mungu Ndani yake akakataa uovu wote, haya majengo tunayo yaita makanisa siyo kosa bali ifahamike zaidi kwamba tunayaita makanisa kwasababu sisi tunakusanikia humo, hivyo ndio maana halisi kwa wale wanye masali kama hayo,kwahiyo kahabari ya majengo haijalishi ni jingo la namna gani kubwa au dogo,ila tunapokusanyika pamoja tukaaza kujifunza Neno la Mungu Tayari hilo ni kanisa,


Lengo la kanisa nikuyatimiza mapenzi ya Mungu anayoyataka yatendeke kupitia kanisa kwa utukufu wake,


Uawala, Ndani ya kanisa hakuna utawala bali kuna uongozi kwamaana tunaongozwa na roho wa Mungu,utawala upo Duniani kwa mambo ya kidunia kama kutawala inchi na mengineyo,


Wewe ni mchungaji wa kanisa lako Mungu alilokukabithi na utaulizwa siku ya mwisho kwamba ulijisimamia vipi, akasema ninyi ni mahekalu ya Roho mtakatifi ya kuabudia atakayeliharibu hekalu langu nami (Mungu) nitamuharibu, iwe unajisimamia mwenyewe au kundi la Bwana kuwa makini na ni Duwa yangu na maombi ukase mwendo mpaka ujio wa kristo utakapokuja,

umeshatambuwa kinachuzungumziwa hapa
Sasa wewe

 
Kumbe wewe ni mchungaji na ungependa kanisa lako likue. Hiyo ni shauku ya kawaida kabisa kwa wachungaji wingi. Lakini – kwa nini unataka kanisa likue? Sababu ya kweli ndani ya moyo wako ni nini?unaweza usimwambie mwanadamu ila Mungu hafichwi na jambo lolote lile,



Je, unataka kanisa likue ili ujisikie umefanikiwa? Je, unataka uheshimiwe na kuwa na ushawishi mkubwa serekalini? Je, unataka kuwa na mamlaka juu ya watu? Je, unatazamia kutajirika? Hizo zote ni sababu mbaya za kutaka kanisa lako likue.


Ukitaka kanisa lako likue ili Mungu atukuzwe kadiri watu wengi wanavyobadilishwa maishani kwa Roho Mtakatifu, basi hiyo ni sababu nzuri ya kutamani kukua kwa kanisa.


Inawezekana kujidanganya – kufikiri kwamba makusudi yetu ni safi na huku ni ya kimwili kabisa, tena ya kibinafsi.


Tunawezaje kujua ukweli wa makusudi yetu? Tunawezaje kujua kama kweli tunataka kujenga ufalme wa Mungu au kujenga ufalme wetu binafsi tu?


Njia moja ni kwa kufuatilia jinsi tunavyoitikia mafanikio ya wachungaji wengine. Kama tunafikiri makusudi yetu ni safi, kama tunafikiri kwamba kweli tunataka ufalme wa Mungu na kanisa Lake likue, lakini tukigundua wivu mioyoni mwetu tunaposikia juu ya kukua kwa makanisa mengine, hiyo inadhihirisha kwamba makusudi yetu si safi. Huonyesha kwamba kweli hatujali sana kukua kwa kanisa, bali tunajali kuhusu kukua kwa kanisa letu (kusanyiko). Mbona iwe hivyo? Kwa sababu makusudi yetu yana kiasi fulani cha ubinafsi ni tofauti kabisa na mpango mzima wa Mungu.


Pia tunaweza kukagua makusudi yetu kwa kupima itikio letu la ndani tunaposikia kwamba kanisa jipya limeanzishwa katika eneo letu. Tukijisikia kutishika au kutofurahia, hiyo ni ishara kwamba tunajali zaidi kuhusu ufalme wetu kuliko ufalme wa Mungu.


Hata wachungaji wa makanisa makubwa au yanayokua wanaweza kukagua makusudi yao hivyo hivyo. Wanaweza kujiuliza maswali kama haya: “Je, ningekubali kuanzisha makanisa mapya kwa kuwatuma na kuwaachilia kabisa viongozi muhimu na watu wa kanisani kwangu, na kwa njia hiyo kupunguza idadi ya washirika wangu?” Mchungaji anayepinga sana wazo hilo bila shaka anajenga kanisa lake kwa ajili ya utukufu wake.

(Kwa upande wa pili, mchungaji mwenye kanisa kubwa anaweza kuanzisha makanisa mapya kwa ajili ya utukufu wake pia, ili aweze kujigamba kuhusu idadi ya makanisa yaliyozaliwa na kanisa lake.) Swali lingine la kujiuliza ni hili: “Je, nina mahusiano na wachungaji wa makanisa Mengine hata yale madogo au machanga? au nimejitenga nao, nikijiona kwamba niko juu kuliko wao?

Je, nitakuwa tayari kuwa mchungaji wa watu kumi na mbili hadi ishirini katika kanisa la nyumbani, au hiyo itaniathiri katika ubinafsi wangu?” ni mambo machache sana wewe kama mtu wa Mungu unayoweza kujiuliza wewe mwenyewe maana inawezekana ukiulizwa ukarusha ngumi au ukaanza kulaani hii nafasi ni yako na inawezekana uko peke yako hata saa hii chunguza uliza roho mtakatifu kama bado hujamuacha,usije ukawaubiri wengine na wewe ukabaki ni Mbaya sana, inaendelea

BARAKA ZA KWELI

BARAKA ZA MUNGU KWA MWANADAMU NI ZIPI?


Baraka za kweli ni kule kuishi hapa ulimwenguni ukifurahia aina Zote za mafanikio Mungu aliyokupatia,Na pia kuwa na matumaini ya maisha ya abaadaye kule mbinguni katika maisha ,katika hizo Baraka za kweli,ukiwa unajitahidi kuishi maisha matakatifu ya kumpendeza Mungu,,,

tena ukiwa unatafakari kwamba Je Mungu akikuita hivi sasa ujipime kwamba utakuwa na ujasiri wa kufikiria maisha ya mbinguni?

kwa hayo maisha unayoishi?kuishi maisha yasiyo mpendeza Mungu ni kama Dereva anayeendesha Gari ambayo haijalipiwa Bima,ikitokea uharibiu wa gaghafla inakuwa inamgarimu,na sisi ni hivyo hivyo kuishi maisha yasiyoongozwa na Mungu,ni kama kuishi maisha yasiyo na Bima huna uhakika nayo maana mwanadamu Hapa Duniani anaishi kwa sekunde tu



Kwa uhakika mulize Dakitari huwa mapigo ya moyo ya mwanadamu Huwa anayapima kwa kutumia nini, utamuona anatumia (Saa) utapata uhakika wa haya niliyoyaandika hapa,huna sababu ya kumyanyasa mwanadamu mwezako aliyeumbwa kama wewe,na kupita kama wewe,kisicho pita ni Neno la Mungu tu,maana limeandikwa kabla mababu na mabibi kuzaliwa lakini mpaka leo,bado nijipya na ni muongozo wa vizazi vyote vitakavyo pita katika hii Dunia,haijalishi kwa yule anaye kataa au asiye kataa,



Maana anayeamini na asiyeamini wote hawa watasimama mbele za Mungu kutowa hesabu ya yale waliyoyafanya wakiwa hapa Duniani,na kipimo hakita pendelea,kuwa ulikuwa masikini au ulikuwa Taji,wala ulikuwa msomi au hukusoma,wapo wengine wataukumiwa hata kwa yale waliyoyasikia kutoka kwa watumishi wa Mungu mbaili mbail,hivyo usiichezee nafasi uliyoipata ya kuishi hapa ulimwenguni,ta futa kusudi la wewe kuwepo hapa ulimwenguni ni nini?



ndiyo maana ukimuuliza yeyote anayeishi hapa duniani kuhusu habari ya Dakika tano zijazo hawezi kukujibu,Bali Mungu akipendezwa na mumoja kati yako Basi unaweza ukajulisha kinachoweza kutokea Mbele ya Maisha yako

uhakika wa kwenda kuishi kule tuliko andaliwa Mbinguni.

Followers