Maombi ya kulinda hatima ya maisha yako






NAMNA YA KULINDA HATIMA


Utangulizi


Mwenye jukumu la kuifuata hatima ya maisha na kuilinda ni mtu mwenyewe wewe ndiyo muhusika mkuu na kiongozi wa kuiongoza hatima ya maisha yakow ewe mwenyewe, maana fikra zako unazielekeza wewe mweneyewe hata kama utashahuriwa bado wewe unajukumu kubwa la kulinda hatima ya maisha yako,kama vile mzazi anavyolinda mtoto wake ndivyo kila mmoja wetu wanatakiwa kulinda hatima yake,


Hatima inayotakiwa kulindwa ni nini?


Hatima ni Hali au uwezo  Wa mtu kufikia katika Kusudi alilokusudia au kusudiwa au ni sababu iliyo ndani ya Mutu, mipango au malengo yake kama alivyoiona au kupanga moyoni mwake, maisha ni ule uwepo wa uhai wa kiumbe chochote amacho kipo katika hii Dunia, sasa uhai wako unaambatana na mahitaji yako ili huu uhai uendelee kuwepo hadi kufikia kusudio la Mungu, kila kiumbe chenye Uhai kina mahitaji yanayo hitajika, hiyo  mipango iwepo ili kufikia ile hatima,


Imeandikwa  Mithali 16:1 Maandalio ya moyo ni ya mwanadamu; Bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana.haya maandaliyo ya moyo ni mipango ya hatima yako kumbuka katika moyo ndiko Roho mtakatifu anapaswa kukaa na ndiko karakana ya kuunda kila  unachokitaka kitokee,


Yale uliyoyaanda yote  ndani ya moyo wako na unategemea kuyakamilisha haijalishi mda


Usitafute Adui  wa hatima ya maisha yako,


Wakati mwingine tumekuwa tukiwalalamikia watu mbalimbali na wengine walikuwa watu wetu wa karibu kwamba wametuharibia maisha. Kwa mfano unaweza kusikia mtu akilalamika kuwa : “…… ameniharibia maisha yangu!”, “……..ameniaribia masomo yangu!” au “…….. amenifanya niitelekeze familia yangu!” na kadhalika. Lakini ni vizuri tukafahamu kuwa kila mmoja anawajibu wa kuilinda thamani yake aliyopewa na Mungu kabla ya wengine kuilinda na kuijali.


Pengine inawezekana tukaona kuwa kuna sababu za kuwalaumu watu kwamba walihusika kuyaharibu maisha yetu; lakini je tuliwahi kujiuliza ni hatua gani tulichukua kuzilinda hatima za maisha yetu?


Umepokea ushauri wa watu wangapi wanaokushauri vibaya kuhusu malengo hatima yako?unataka kuolewa,kusoma,kufanyabiashara,kujenga,kuanza Huduma,je hatima ya maisha yako uliilinda,


Uliwapa watu wangapi nafasi ya kuchezea hatima yako!?


Umeenda maeneo mangapi yanayopunguza kasi ya kufikia ndoto zako!?


Umependa vingapi vinavyoondoa kusudi la hatima ya maisha yako hapa duniani!


Haya ni baadhi ya maswali tunayoweza kujiuliza kama msaada wa kulinda hatima zetu  ili kuanza  hatua mpya au kuendelea mbele pamoja na hatima ya maisha yangu,


Imeandikwa  2 Petro 1:3 “kwa kuwa uweza wake wa Uungu umetukirimia vitu vyote vipasavyo uzima na utauwa kwa kumjua yeye aliyetuita kwa utukufu wake na wema wake mwenyewe.


Kwakuwa tulivyo navyo vipo ndani yetu jukumu la kulinda ni la mtu binafsi, na hatima ya Mtu inaanzia wapi?


Hatima ya mtu inaanzia katika mawazo ya Mungu inakamilishikia tumbomi mwa mama imeandikwa yeremia 1:4


WATAMBUWE MAADUI WA HATIMA YAKO


Nini maana ya adui ni nguvu ya upizani au uasi  unaokutana nao juu ya hatimaya maisha yako,


  • Kukatisha tamaa juu ya jambo ulilofanya,au unalojaribu,au wazo zuri unalopanga kulifanya
  • 2. Kumwonea wivu mtu kwa sababu ya mafanikio yake ya kimwili au kiroho – imeandikwa MWANZO 37:9-11;
  • Marafiki wasiyokutakia mema  watu wasiyotaka kuona unasonga mbele Jiepushe nao,
  • Kukusudia mabaya juu ya wengine  MWANZO 50:20; NEHEMIA 6:2; EZEKIELI 38:10-
  • Marafiki wasiyokuwa na mtazamo mkubwa na wakuona mbali
  • Marafiki wanaotaka kunufaika kupitia wewe
  • Kuhisi umefika safari yako ikiwa bado
  • Kuhisi wewe unaweza kufanya chochote bila wengine,kujiona wewe wa muhimu kuliko wengine
  • Kuona wewe ni Zaidi ya watu wote yaani kuwa nakiburi cha mali,uzima,heshima
  • Dharau kwa wenzako ikiwa ili ufanikiwe unahitaji watu katika maisha ,kuuza au kununua unahitaji watu,
  • Tabia ya asili yaani tabia inayotokana na desturi ya ukoo au kablia
  • familia
  • Mazingira ya kifamilia ya kwenu,ikiwa mlikuwa masikini inaweza  yanaweza kuwa adui kwako ukafikiri hayo ndiyo maisha halili unayotakiwa kuishi maana ndiyo uliyoyakuta,
  • Kutokubali mabadiliko katika yanayoweza kukufanikisha jambo Fulani,
  • Kutamani madaraka Zaidi kama Namani na modikae
  • Kukosa umakini na mafanikio ya hatua ya kwanza
  • Kutokutambuwa udhamani wa maisha nan a talanta uliyopewa
  • Kuwa na marafiki wenyemitazamo ya yakushindwa,
  • Kukosa uvumilivu wakati wa kujaribiwa
  • a yaani wakati wa magumu,
  • hali ngumu ya uchumi inasababisha kukata tamaa na kulalamika,
  • mafanikio ya kiuchumi kuwa juu
  • au kupata madaraka makubwa bila matarajio ya hiyo nafasi,
  • Jinsia inaweza kuwa adui wa hatima yako kujiona kwakuwa wewe uko hivyo ulivyo,mke,mme,
  • Kutodhubutu hatuwa ya mafundisho unayofundishwa,
  • Kutumia ulimi wako vibaya
  • Kukosa maarifa juu ya hatima ya maisha yako,
  • Kupoteza shahuku ya kuendelea mbele juu ya kufanikisha hatima yako,
  • Kukosa mlengo yaani kukosa maono ni adui wa wewe kufika katika hatima au kutunza hatima yako,
  • Kushindwa kutoa shukrani juu ya kile Mungu alichokutendea,shukuru wazazi,
  • Kukosa mvuto juu ya kile unalolitaka na juu ya watu waliyokuzunguka,
  • Kujiamini hadi kumzidi roho mtakatifu,


Dalili za mtu hatima yake imevamiwa


  • Hatima iliyoharibika mtu kuishi maisha ya kuiga wengine
  • Hana maamuzi na maisha yake
  • Ni mtu anayeishi kwa ubishi wa kila jambo
  • Hatima iliyotekwa anaishi kwakulinganisha maisha yake na wengine
  • Hatima iliyoharibika ni anaishi kwakubahatisha,(kwa kuhisi)
  • Nimtu wa kujitenga na wengine au kutaka kuhurumiwa sana
  • Mtu hatima yake iliyoharibika ni mlalamikaji san ahata umtendei jema hana shukrani maana haoni udhamani
  • Mtu hatima imeharibika ni mtu wakuvunjika moyo haraka sana
  • Mtu hatima imeharibika anahisi kukataliwa na wengine,
  • Mtu hatima imeharibika akianzisha jambo hawezi kukamilisha,


Ufanye nini kulinda hatima ya maisha yako


Jifunze kumtumaini Mungu kwa akili zako zote na kwa moyowako wote mithali 3:5


Jifunze kuwa mnyeyekevu siku zote za maisha yako kanuni ya kupanda ni kushika,


Jitahidi kukubalika mbele za Mungu na mbele za wanadamu 1timotheo 7:15


Mshukuru Mungu kwakila kiwango anachokufikisha maana kuna ambao hawajafika kiwango hiko


Tafuta macho ya rohoni na masikio ya rohoni kuweza kutembea ndani ya maono ya Mungu, marko 8:18


Jitahidi kutumia muda wako vizuri sana na furusa iliyombele yako pia,


Jikubali na jisimamie wewe mwenyewe kwa kuamini kwamba unaweza kufanya Zaidi ya hapo ulipo jikubali hivyo ulivyo haijalishi umepungukiwa nini kubali sauiti mwili,elimu uliyo nayo,


Jitahidi kuwa na subira ya ahadi za Mungu alizokuhaidi kupitia vyinywa vya manabii mambo ya nyakati 20:20


Kukubali kushinda majaribu unayotakiwa kupita,


Usikubali kukatatamaa mapema kwakutoamini Imani yako usiwe mtu wa kusita sita, waibrania 10;38


Chochea moto wa madhabahu unayoiamini,


 


Hitimisho:


Maombi ya toba kwakutojuwa hili…………..


 

Followers