HABARI NJEMA NI HIZI,

Yesu kriso anakupenda na anakufahamu na anakuona,

Yesu ni wa kweli, anajua jina lako na kila kitu kinacho kuhusu, pia anakupenda. Hayuko mbali nawe, yuko karibu nawe, anataka ujue kuwa yupo, anaishi, na anataka kukusaidia ikiwa utapenda kusaidiwa na yeye. Na kama utapenda kumfahamu zaidi, unaweza kumfahamu. Ikiwa utahitaji msaada, atakusaidia, kama utaongea nae atakusilikiza, naye ataongea nawe pia.







Yesu ndiye aliyekufanya usome maandishi haya, kwa sababu ametuambia tukuandikie, na amehakikisha kuwa yamekufikia. Anajua kila kitu kinachokuhusu tangu mwanzo wa maisha yako hadi sasa hivi, amejumuika nawe katika huzuni, madhaifu na hata matatizo yako, atakusaidia mara tu utakapo muhitaji. Hakutaka uwe peke yako, mara nyingi ametaka umjue yeye. Ndiyo maana amekufanya kuwa rafiki kwa makusudi hayo. Mwamini yesu kristo, kwani kwa Yesu kristo urafiki ni mzuri tena wa kweli, isitoshe ni wa upendo ule wa ndani. Hatokuacha kamwe, unachotakiwa kufanya ni kumwamini na uongee nae yeye Yesu, naye atakujibu, atakusaidia, na ndipo utakapomfahamu Yesu. Anakutazama sasa unaposoma maandishi haya na amejaa upendo juu yako.






Imeandikwa kuwa, Yesu alikuja duniani, akafa, akatoa uhai wake kwa ajili yetu. Hii inaonyesha kuwa kifo kilikuwa ni cha lazima, ili kulipa deni la dhambi zetu. Kwa nini alichagua kulipa deni la dhambi kwa njia ya kifo? Ni kwa sababu anakupenda sana!


Ulistahili uwajibike wewe kama wewe, maana mshahara wa dhambi ni mauti,ila yeye akakulipia deni


Hakuna mtu mwingine katika historia ya dunia hii bali Yesu tu. Hakuwa mdhambi, dhambi ilikuwa kwa wengine. Dhambi zote zinakuja zenyewe kwa namna moja ama nyingine alionekana mnyenyekevu. Baba wa mbinguni alituumba ili tupendane sisi kwa sisi, na pia tumpemde yeye, lakini dhambi imekuwa kinyume na upendo huo na imechukua nafasi kubwa katika maisha yetu, hata kusababisha kifo. Hata hivyo, kifo ndio kimekuwa malipo makuu ya dhambi. Dhambi inatembea kutoka kwa mtu mmoja. Kwenda kwa mwingine, nchi moja kwenda nyingine, na inaleta maumivu kwa kila mtu, na ndiyo maana inawatenganisha wanadamu wote na Mungu, na inawapeleka kuzimu. Mungu hatokubali dhambi iingie Mbinguni, na mbingu ziwe kama dunia ilivyo hivi sasa, imejaa maovu na kujiona zaidi. Kwa miaka mingi Mungu aliruhusu wanyama wafe. Kwa njia hiyo wanadamu walikuwa na mahusiano ya karibu zaidi na Mungu wao mpendwa na waliongea nae. Aliwapenda na kuongea nao pia, kwa mfano, Abrahamu, Ayubu, Adamu na wengine wengi. Mungu anataka uhusiano huo leo kwako, lakini hutaki kujitolea kafara wanyama ili kuwa nae.


HEKIMA ZA MWANADAMU ZINA MIPAKA YAKE


Mwanadamu amejaribu kuwa na ukaribu na Mungu kwa kupitia njia mbali mbali, lakini si kwa njia ile ambayo Mungu alitegemea kutoka kwao. Kaini mtoto wa Adamu alitoa kafara ya mazao yake badala ya mnyama. Hata hivyo, Mungu hakupokea kafara ya Kaini kwa sababu haikuwa na thamani sawa na dhambi iliyokuwa ndani yake. Haijalishi Kaini alikuwa na mawazo mazuri au mabaya juu ya Mungu, bali kafara yake haikuwa na thamani ya kulipa deni la dhambi.






Ukweli ni kwamba watu bado hawajajua dhambi zao. Kwetu dhambi imekuwa ni neno la kidini. Wengi hawajajua kwa nini jambo lifanyike kwa ajili ya dhambi. Lakini Mungu ameona ni jinsi imekuwa ya kuume na ya kipekee tena yenye nguvu. Na jinsi ambavyo inaleta shida na masumbufu ndani yetu. Huko mbinguni kama siyo dhambi, tungeweza kuonana na Yesu uso kwa uso, tungekuwa huru kutoka dhambini na kuwa huru wenye nguvu zaidi na zaidi, pia tungekuwa mahali ambapo kila mtu awaye binadamu, au


malaika, au kiroho, angependa kuwepo. Wote tungependana na Mungu angeishi maisha ya upendo kwa wengine na siyo ya kibinafsi.


Fikrira za mwanadamu ni tofauti na za Mungu


Mungu ni mwerevu na kwa sababu ya hekima zake, amekuwa mkweli katika kile asemacho na afanyacho. Ikiwa hatutomficha, na kuiendea njia ile aliyotuandalia, kwa sababu ya dhambi, Bwana atajitoa na kwenda mbali nasi. Yeye ni Mungu mwenye upendo, asiye na ubinafsi, na wala hajihusishi na dhambi. Kama utaing’ang’ania dhambi na bila kinga yoyote, utajitenga mwenyewe na Mungu. Nawe hawezi kuja karibu yako ili umfahamu. Hata hivyo kumfahamu Mungu. Ni lazima uwe na kinga ya dhambi.


KUUJUWA UUNGU WA YESU KRISTO:


Kwa karne nyingi wema wa mwanadamu umekuwa ukitolewa kafara ya wanyama kwa Mungu. Wengi walidhani kuwa Mungu yuko mbali nao, lakini wachache walitambuwa kuwa Mungu yu pamoja nao. Hata hivyo, watu wengi wamekuwa wakiangalia zaidi dini, kwa matumaini kuwa wema zaidi mbele zake. Kwa kuwa hivyo, kunawafanya watu wajisikie vizuri , lakini kuna haja ya kusaidiana sisi kwa sisi. Kwa sababu sisi sote ni viumbe vya Mungu, isipokuwa kumjua Mungu kwa kupitia dini, ndicho kitutenganishacho. Tumeumbwa kwa mfano wa Mungu, naye yu kama sisi. Isipokuwa yeye si mdhambi, ni mwingi wa upendo na rehema. Ni wa upendo kwa amfikiriaye, amhisiye, ampendaye na kwa yule anayemjali, alituumba ili tuweze kumfahamu. Adamu, Ibrahimu, Musa, Paulo na wengine wengi walimpenda Mungu. Na aliwachukulia kila mmoja kuwa ni marafiki zake. Kila mmoja wao ni mzima na ana mjua Mungu. Wako pamoja nae sasa huko Mbinguni, kama alivyoahidi kuwa ikiwa utamjua yeye, nawe utakuwa nae kule Mbinguni.


Baba wa mbinguni alijua kuwa kafara ya mnyama haitoshi. Mwanadamu akaanza kupoteza hamu ya kumjua Mungu na kuridhika na mambo ya dini. Cha ajabu, Mungu akaamua kuja duniani kwa ajili ya kila mmoja wetu. Akaja, akaishi kama Mwanadamu, ili aweze kulipa deni la dhambi zetu. Kwa mara moja hiyo, watu waweze kuwa marafiki zake (Mungu). Fidia ya dhambi imekuwa kama tumekuwa nae kwa undani zaidi, kwa maumivu aliyoyapata, kwa maana huo wema wa Mwanadamu hauwezi ukalipwa kwa damu ya mnyaa kamwe.


YESU KRISTO ni yeye yule jana leo na hata milele:


Huyo ndiye Yesu tunayezungumzia habari zake, na sababu alikuja duniani kuja kukuokoa, yeye ni Mungu. Alikuja duniani kutoa kafara ya ndani kwa ajili ya dhambi zetu kila mmoja, ili kwamba yeyote atakaye mwamini Baba kupitia kifo chake, damu yake iliyomwagika msalabani kwa ajli ya dhambi zetu. Yesu hakuwa mdhambi. Hata sadaka aliyoitoa kwa kwa Mungu ilikubalika. Kifo chake kilikuwa kafara yakutosha. Alikufa na dhambi zetu. Kafara yake ilikuwa ya upendo na njia kwa kuweka daraja kati ya Mungu na mwanadamu kwamba tuweze kwenda na kumjua Mungu tena.






Yesu ni mwenye ushirikiano, ni mzuri, mwema na mwenye upendo. Matokeo ya dhambi zetu ingekuwa uharibifu, kama ambavyo dunia yote ingeharibiwa kama kipindi cha nuhu au sodoma na Gomora. Mungu angeweka huruma yake ili tuendelee kuwepo, kafara aliyoitoa ilituepusha na uharibifu wowote na kutufanya wake. Ilikuwa ni upendo wa kujitolea mno! Yesu ni Mungu, ni Mungu mwenye uhuru. Nani awezaye kumzuia katika kutuangamiza sisi? Nani awezaye kulazimisha aweze kuja kutufilia sisi hapa duniani na dhambi zetu? Watu walidhani kuwa ni kazi ya Mungu kuokoa maisha yetu. Hapana, haikuwa kazi, bali upendo tu. Tunaweza kujiuliza ni upendo wa namna gani aliyokuwa nao hata kujitoa kwa ajili yetu? Hata tukiishi miaka milioni, hatustahili kile Yesu alichotenda. Yesu ni mwanaume na mwenye nguvu. Ana mamlaka yote juu ya kifo, na hii inathibitishwa pale Yesu aliporudi katika maisha yake baada ya kuwa amekwisha uawa. Hayupo nabii wala mtume ambaye aliwahi kukishinda kifo ni yeye tu hili limewachanganya wengi sana maana akiwa anakufa walikuwepo watu na wakamshuhudia na kumzika na akiwa anafufuka walikuwepo watu na wakamshuhudia akipaa kwenda mbinguni,


Ujumbe wa msalaba sasa yote yamekwisha: ila kwa waliopotea kwao ni upuuzi


Sasa kwa kuwa maisha ya Yesu yametoweka, Mungu hayupo tayari kuona mwanadamu anapotea, hata kwa damu ya wanyama, dini nyingine hata kwa imani. Nyumba ya Mungu ibaki kuwa takatifu, na kwa ajilki ya Mungu tu. Nyumba ya Mungu imetobolewa kutoka Mbinguni hadi duniani na mkono wa Mungu, wakati Yesu yuko msalabani, anafungua njia kwa ajili ya uwepo wa Mungu. Yesu alisema kuwa “imekwisha” . kifo kilihitajika kama jibu pekee la dhambi. Na ilikuwa kwa kumtoa mwana wake wa pekee afe kwa ajili ya dhambi zetu. Na baba yake alihakiki na kumpokea kwa ajili yetu.


UTAONA UWEPO WAKE UKISHA MKARIBISHA NDANI YAKO


Habari njema ni kwamba, hautokuwa mbali na Mungu ukimkiri, bali utakuja kwa Baba wa Mbinguni. Kwa unyenyekevu, mwombe atoe kafara ya mwana wake Yesu kwa ajili ya dhambi zako, na kwa furaha atafanya. Halafu utaongea nae, na ataongea nawe na kufanya urafiki na wewe ambao hautokwisha milele. Atakuwa karibu nawe, haijalishi nini kitakukuta katika maisha yako binafsi, au katika ulimwengu. Atakupenda, na atakusaidia.






Atakufanya umjue kupitia roho mtkatifu. utahisi uwepo wake, naye atajibu maombi yako. Utaanza kumfahamu Yesu ambaye ni mwingi wa upendo, rehema na utu wema. Kuhusu maisha yake na dunia kwa ujumla, kama utakavyoongea nae, atakusikia, atakuja karibu yako.






Sio tu ataongea nawe kuhusu maisha yako, bali atakuonyesha na mawazo yake juu yako kutoka moyoni mwake, kama jinsi ambavyo unajua mawazo ya rafiki, kipenzi chako yalivyo moyoni mwake. Pia atakuonyesha mahali pazuri (Mbingini) ambako utakuwa naye milele baada yaw ewe kwenda. Lakini sasa unaweza kumfahamu Mungu kwa uzuri zaidi. Kumjua Mungu siyo kwenda kanisani kwa sababu wanaompenda Kristo na kumjua, ndio walioko kwenye Kanisa Lake.usifanye kitu kama desturi tu






Mwamini Mungu, naye atakuonyesha nini cha kufanya. Biblia iliandikwa kwa uwezo wa roho mtakatifu kwa niaba yetu. Lakini haikumaanisha kuchukua nafasi ya kumjua yeye. Biblia ni neno la Mungu, na inatuelekeza kwa Yesu akupendaye na aliyekufa kwa ajili yako, na yupo kwako sasa hivi, anataka umjue! Wasiliana nasi kwa maelekezo zaidi kama una swali au hitaji la maombi,tuandikie kupitia






E mall : Samsonoxpel@gmal.com


Web: www.samsonoxpel.blogspot.com


Cell no 0756-809209/0784-713604/


Huduma zote hizo zinzpatikana bure, mmepewe bure nanyi toweni bure,

MAFUNDISHO YA KUISHI MAISHA MATAKATIFU

JE ? NIMAISHA YAPI TUNAYOSTAHILI KUISHI

Ni watu  wangapi wangeona wameheshimiwa sana kama mtu angewaita “mhubiri wa utakatifu”? Ni wangapi wanaojiita Wakristo wangetumia maneno hayo kwa njia ambayo si ya kudhihaki? Mbona utakatifu ni somo baya sana mawazoni mwa watu wengi wanaodai kuamini kitabu ambacho kina maneno mtakatifu au utakatifu zaidi ya mara mia sita, chenye kuwaahidi wakati ujao katika mji mtakatifu ambamo ndani yake anakaa “Aliye mtakatifu”, ambaye jina Lake ni mtakatifu, anayewapa Roho Wake Mtakatifu na ambaye kiti Chake cha enzi kitakatifu kimezungukwa na wenye uhai wanne wasioacha kusema usiku na mchana, “Mtakatifu, mtakatifu, mtakatifu ni Mungu Mwenyezi”? (ona Ufunuo 21:2; Isaya 40:25; Walawi 22:32; 1Wathes. 4:8; Zaburi 47:8; Ufunuo 4:8 – Maneno mepesi ni kutilia mkazo).



Kama sehemu ya kwanza ya Mahubiri ya Mlimani imetufundisha kitu, ni kwamba Yesu alikuwa mhubiri wa utakatifu. Hiyo ndiyo iliyokuwa mada Yake – utakatifu, na jinsi unavyohusiana na wokovu.



Mahubiri ya Mlimani yameandikwa katika Injili ya Mathayo sura ya 5, 6 na 7. Mpaka sasa tumetazama sura ya 5 tu. Hapo, katika zile “Heri” tulijifunza tabia au sifa za wanaokwenda mbinguni. Pia tuligundua kwamba Yesu hakuja kuibatilisha au kuiondoa Torati, na kwamba kushika sheria ni muhimu sana. Tulijifunza kwamba hatuwezi kuingia katika ufalme wa mbinguni kama haki yetu haitazidi ile ya waandishi na Mafarisayo, walioishika sheria kama ilivyokuwa ila wakapuuza maana yake.



Sehemu ya pili ya Mahubiri ya Mlimani – yaani Mathayo 6 na nusu ya kwanza ya sura ya 7 – ina amri zingine tena ambazo Kristo aliwapa wafuasi Wake. Je, kuzishika kunahusika kwa lolote na wokovu? Hakika kabisa. Sehemu ya mwisho ya sura ya saba inaonyesha jambo hilo waziwazi kabisa, kama tutakavyoweza kujionea.



Hebu tuendelee kusoma yale ambayo Yesu aliwaagiza wafuasi Wake wa kweli, ambao waliamini kwamba Yeye ni Mwana wa Mungu, ni Masiya. Tujiulize swali hili, zito kabisa: Ikiwa wasikilizaji wa Yesu hawakumwamini, walimtii kwa sababu gani? Mbona watake hata kusikiliza akifanya madai ambayo yangeathiri kila eneo la maisha yao? Jibu ni wazi: Kwa kuwa waliamini, walitaka kutii. Wangeonyesha imani yao kwa matendo yao.





Ona katika sehemu hii ya kwanza Yesu anahesabu kwamba wafuasi Wake watatenda haki, naye anawaonya wahakikishe kwamba makusudi yao ni kumpendeza Mungu badala ya kuwapendeza watu.




“Angalieni msifanye wema wenu machoni pa watu, kusudi mtazamwe na wao; kwa maana mkifanya kama hayo, hampati thawabu kwa Baba yenu aliye mbinguni. Basi wewe utoapo sadaka, usipige panda mbele yako, kama wanafiki wafanyavyo katika masinagogi na njiani, ili watukuzwe na watu. Amin nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe utoapo sadaka, hata mkono wako wa kushoto usijue ufanyalo mkono wako wa kuume; sadaka yako iwe ya siri; na Baba yako aonaye sirini atakujazi” (Mathayo 6:1-4 – Maneno mepesi kutilia mkazo).



Yesu alitazamia kabisa kwamba wafuasi Wake wangetoa sadaka kwa maskini (kama tulivyojifunza katika sura ya 3 ya kitabu hiki). Torati iliagiza hivyo (ona Kutoka 23:11; Walawi 19:10; 23:22; 25:35; Kumbu. 15:7-11), na waandishi na Mafarisayo walifanya hivyo kwa kupiga matarumbeta, kwa kusudi la kuwafanya watu maskini waone utoaji wao. Lakini – ni wangapi wanaojiita Wakristo (na hata makanisa ya Kikristo) wanaotoa chochote kwa maskini? Hawajafikia hata mahali pa kutaka kuchunguza makusudi yao ya utoaji zaka! Kama uchoyo na ubinafsi uliwasukuma waandishi na Mafarisayo kutangaza kutoa kwao sadaka, ni nini kinachowasukuma wanaojiita Wakristo kupuuza hali ya maskini? Je, haki yetu inazidi ile ya waandishi na Mafarisayo?



Kama ambavyo Paulo atarudia katika 1Wakorintho 3:10-15, tunaweza kufanya matendo mema ambayo hayatapata thawabu ikiwa nia na makusudi yetu si safi. Wafuasi wa kweli wa Kristo wanapaswa kuwa na nia safi katika kila tendo jema, lakini si wote walio nayo. Paulo aliandika kwamba inawezekana hata kuihubiri Injili kwa makusudi yasiyo safi (ona Wafilipi 1:15-17). Njia iliyo bora ya kuhakikisha kwamba kutoa kwetu kunasukumwa na makusudi safi ni kutoa kwa siri kiasi iwezekanavyo.



Yesu pia aliwatazamia wafuasi Wake waombe na kufunga. Hiyo ilikuwa lazima. Hakusema “Kama mtaomba”. Alisema “Mwombapo”. Hatari ilikuwa wangeweza kuyaruhusu makusudi yao kuchafuka, kama ilivyokuwa kwa makusudi ya wasioamini waliokuwa wanaomba na kufunga. Kama hayo yangetokea, wangepoteza thawabu ile ambayo wangepata kama makusudi yao yangekuwa safi. Basi aliwapa mashauri yafuatayo:



“Tena msalipo, msiwe kama wanafiki; kwa maana wao wapenda kusali hali wamesimama katika masinagogi na katika pembe za njia, ili waonekane na watu. Amin nawaambieni, Wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe usalipo, ingia katika chumba chako cha ndani, na ukiisha kufunga mlango wako, usali mbele za Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi. Nanyi mkiwa katika kusali, msipayuke-payuke kama watu wa mataifa; maana wao hudhani ya kuwa watasikiwa kwa sababu ya maneno yao kuwa mengi. Basi msifanane na hao; maana Baba yenu anajua mnayoyahitaji kabla ninyi hamjamwomba…”



“Tena mfungapo, msiwe kama wanafiki wenye uso wa kukunjamana; maana hujiumbua nyuso zao ili waonekane na watu kuwa wanafunga. Amin nawaambia, wamekwisha kupata thawabu yao. Bali wewe ufungapo, jipake mafuta kichwani, unawe uso, ili usionekane na watu kuwa unafunga, ila na Baba yako aliye sirini; na Baba yako aonaye sirini atakujazi” (Mathayo 6:5-8; 16-18).



Narudia tena: Je, ni wangapi wanaojiita Wakristo ambao hawatumii muda wao mwingi katika maombi, na ambao hawajawahi kufunga kabisa? Haki yao inalinganishwaje na haki ya waandishi na Mafarisayo, ambao walifunga na kuomba (japo kwa sababu mbaya)?



Maombi aliyoagiza yesu tuyafanye :

Yesu pia aliwaambia wanafunzi Wake jinsi walivyotakiwa kuomba. Maombi Yake mfano ni ufunuo wa hali ya juu sana kuhusu matazamio Yake kwa habari ya pendo lao, utii wao na vipaumbele.



“Basi ninyi salini hivi: ‘Baba yetu uliye mbinguni, Jina lako litukuzwe, Ufalme wako uje, Mapenzi yako yatimizwe hapa duniani kama huko mbinguni. Utupe leo riziki yetu’.” (Mathayo 6:9-11)



Jambo la kwanza muhimu sana kwa mwanafunzi wa kweli wa Yesu iwe jina la Mungu litukuzwe. Yaani, jina la Mungu liheshimiwe, liabudiwe na kutakatifuzwa.



Bila shaka wale wanaoomba kwamba jina la Mungu litukuzwe wanatakiwa wao wenyewe kuwa watakatifu, wanaolitukuza jina la Mungu. Itakuwa ni unafiki kufanya vinginevyo. Kwa hiyo, sala hii inaonyesha shauku yetu kwamba na wengine wajinyenyekeze kwa Mungu kama ambavyo sisi tumefanya. Na – kama nilivyouliza katika sura nyingine hapo nyuma – mtu anaonyeshaje kiwango cha shauku yake kwamba anataka jina la Mungu litakaswe kama anajistarehesha kwa kutazama picha ambazo zinachezwa na wachezaji wenye kutumia vibaya jina la Mungu na la Mwana Wake? Kulingana na uchunguzi wangu, hiki ni kitu ambacho wengi wanaojiita Wakristo hufanya mara kwa mara. Je, wewe ungechukizwa na sinema ambayo waigizaji wanatumia jina lako kama neno la kuapa au kushangaa?



Ombi la pili katika sala hiyo linafanana na la kwanza: “Ufalme wako uje.” Wazo la ufalme huonyesha kwamba kuna Mfalme anayetawala ufalme Wake. Mwanafunzi Mkristo anatamani kuona mfalme Wake – yule atawalaye maishani mwake – akitawala dunia nzima. Laiti kila mtu angepiga goti lake kwa Mfalme Yesu, katika imani tiifu!



Ombi la tatu linarudia yale mawili ya kwanza: “Mapenzi yako yafanyike hapa duniani kama huko mbinguni.” Hapa tena – tunawezaje kuomba kwa dhati ombi la namna hii bila sisi wenyewe kuwa tumejinyenyekeza chini ya mapenzi ya Mungu katika maisha yetu? Mwanafunzi wa kweli anatamani kwamba mapenzi ya Mungu yatafanyika duniani kama huko mbinguni – kikamilifu na kabisa.



Kwamba jina la Mungu litakaswe, na mapenzi Yake yafanyike, na ufalme Wake uje vinatakiwa kuwa muhimu zaidi kwetu kuliko chakula cha kutuhifadhi, au “riziki yetu”. Hili ombi la nne linawekwa hapo kwa sababu. Inaonyesha mpangilio mzuri wa mambo ya muhimu maishani mwetu, na hakuna dalili za uchoyo hapo. Huyu mwanafunzi anayeomba anamtumikia Mungu, si mali.

MTAWALA MZURI NI WANAMNA GANI?

Kwanza hebu tufahamu  kidogo mtawala ni mtu wa namna gani  kwa tafsiri niliyoiona nyepesi  Mtawala ni mtu  aliyechaguliwa na watu au kundi la watu kwaajili ya kusimamia maamuzi waliyokubaliana kwa pamoja  kwa manufaa yao wotw na haki zao zote zinazostahili kupatikana au kufanyika, na yeyote atakayefanya kinyume maana yake amekiuka utaratibu yaani kwa maana nyingine amewafanyia mwengine jambo la uovu, wasilokubaliana katika makubaliano yao, 

Kwa mfano mtu akikubali kuoa kwa ndowa ya kikristo ya mke mmoja, wakakubaliana hao wawili sasa ikaja siku mmoja wao akafanya kinyume akaoa au kuolewa kwa siri au kwa wazi basi yeye aliyefanyifa tendo hilo la kuachwa bila rithaa anakuwa amefanyiwa uovu usiyokubalika mbele za Mungu na mbele za wanadamu pia,  tuangalie Maandiko matakatifu yanaelezea nini kuhusu mtawala, 

 wenye haki wakiwa na amri, watu hufurahi: Bali muovu atawalapo watu huuguwa, Mithali 29:2 ukiendelea mbele kidogo inasema Mwenye haki huyaangalia madai ya masikini bali mtu mbaya  Hana ufahamu hata ayajue watu wenye dharau huwasha mji moto: Bali wenye hekima hugeuzia mbali ghadhabu, mwenye hekima akijadiliana na mpumbafu: Akikasirika au Akicheka,pia hapana raha. wamwagao Damu humchukia mtu mkamilifu Bali mwenye Hekima hutuza nafsi yake,mithali 7:10)

Sifa za mtawala kwanza kabisa kabla ya kuchunguza mambo yote anatakiwa ule uhalisi wa uumbaji wa Mungu unatakiwa kuwa ndani yake yaani awe na hofu ya Mungu ndani yake ili aweze kujuwa thamani ya mwanadumu ni nini,

kwa nini muovu shetani anatesa watu anajaribu kuharibu ile thamani ya mandamu aliyopewa na Mungu, hivyo kama mtu hana hofu ya Mungu huyo hanatofauti na mnyama,

myama yeye hafanyi ibada hategemei kwenda mbinguni na hana habari na mbingu,

kama mtawala akiwa na mahusiano na Mungu nirahisi kuyaona hata mambo ya mbeleni maana mungu anaweza hata kutumia maono au ndoto kumjulisha ila kama hana mahusiano na Mungu atakuwa kama mfalume Nebokadraze anaoteshwa ndoto maana ikakosekana tena heri yeye washahuri wake walikuwa wana hofu ya Mungu wakashahuriana watafutwe watumishi wa Mungu wakaenda kutafsiri Ndoto ya mflume,



sasa  kama  mfalme hana mahusiano na  Mungu akipata tatizo sana sana atakimbilia kwa wachawi badala ya Kumgeukia Mungu, tumwangalie mfalme baada ya kutafsiriwa ndoto yake nini kilitokea?

Hata hivyo, hakuamini, kuwa mateka hawa vijana walikuwa ni watu wenye ufahamu mkubwa wa imani ambo walikuwa wako tayari kufa kuliko kumwacha BWANA, Mungu wao.




Danieli 1 na 2



DANIELI NA RAFIKI ZAKE WANAPEWA JARIBIO: Danieli 1:3-21

Kama sehemu yake ya kuwashawishi wafalme vijana ili wawe waabuduo miungu ya Babeli, mfalme Nebukadreza alibadilisha majina yao na akawaita kwa mjina ambayo yanaheshima kwa miungu ya Babeli.

Kisha akaamuru wapewe kila siku chakula na divai kutoka katika meza ya mfalme. Danieli na rfiki zake walitambua kuwa chakula hicho na divai viliwekwa kwanza wakfu kwa miungu ya mfalme, maana hiyo ndiyo iliyokuwa desturi ya nchi ya Babeli.

Wao wakamwambia msimamizi mkuu awapatie mtama (maharagwe na dengu) na maji badala ya chakula cha mfalme. Akimwongopa mfalme, asije kujulikana kuwa hakutii agizo lake hatimaye akakubali kuwaweka katika majaribio kwa muda siku kumi.

Na baada ya siku kumi ilikuwa ni dhahiri kwa watu wote kuwa Danieli na rafiki zake walikuwa na “nyuso zao zilikuwa nzuri zaidi na miili yao ilikuwa imenenepa zaidi” kuliko vijana wote ealiokula chakula cha mfalme (mstari 15). Mungu akawajalia kupata kibali na huruma machoni pa huyu mtumishi wa mfalme kwa sababu ya uaminifu wa utii kwa Mungu.

 Na ingawa walikuwa katika nchi za watu asiomjua Mungu, wakiwa mbali na nchi ambayo Mungu aliwapatia baba zao, vijana hawa waliendelea kumwabudu Mungu wao, naye akaendelea kuwabariki, “akiwapatia maarifa na ujuzi katika elimu na hekima: Danieli naye alikuwa na ufahamu katika maono yote na ndoto” (mstari 17)



NDOTO YA NEBUKADREZA: Danieli 2

Usiku mmoja, mfalme Nebukadreza aliota ndoto ya kubwa sana na ya kushangaza na ya kutisha.Ilimhangaisha sana, hata asiweze kulala usingizi tena.Aliwaita wote wenye hekima ili waweze kumwambia ndoto kwa kuwa alidhamiria kujua maana ya ndoto hiyo inayotisha sana.Ikawa wenye hekima walipokuja walimwambia mfalme,

“Tuonyeshe sisi watumishi wako ile ndoto, nasi tutakuonyesha ile tafsiri yake” (mstari 4). Nebukadreza aliwafahamu watu wake hao wenye hekima kuwa wana akili sana, na hakutaka kusikiliza maelezo yoyote ya kuvutia kugeuza kusudi la nia yake. Alitaka kujua kweli. Alikataa kuwajulisha ndoto yake. Na hii ilionekana kwao kuwa ni jambo lisilowezekana. Ni njia gani gani wangeweza kujua ndoto ya mfalme aliyoota kitandani mwake / Hata hivyo mfalme hakubadilisha nia yake.

Wamwambie ndoto na tafsiri yake ama wafe. Walilalamika, Hapana mtu duniani awezaye kulionyesha neno hili la mfalme; kwa maana hapana mfalme wala bwana, wala liwali, aliyetaka neno kma hili wala hapana mwingine awezye kumwonyesha mfalme neno hilo, ila miungu, wasio na kikao pamoja na wenye mwili” (mstari 10-11)



Mfalme akagadhabika sana, akatoa amri ya kuwaangamiza wenye hekima wote-“wakawatafuta Danieli na wenzake ili wauawe” (mstari 13).



Danieli aliposikia amri ya mfalme ya kuwaua wote,alimwomba mkuu wa walinzi, “mbona amri hii ya mfalme ina ukali namna hii” (mstari 15). Mkuu wa walinzi akamwambia sababu, Danieli mara moja akamwomba muda na atamwezesha mfalme kufahamu yote mawili ndoto na tafsiri ya ndoto hiyo. Kwa hiyo Danieli na rafiki zake watatu wakmwomba Mungu awafunulie ile ndoto ya mfalme. Mungu akasikia maombi yao, akamwonyesha Danieli yote mawili, ndoto namaana ya ndoto. Danieli, akaingia kwa mfalme Nebukadreza kwa kujiamini sana.



Danieli, akasema, “yuko Mungu mbinguni afunuaye siri, naye amemjulisha mfalme Nebukadreza mambo yatakayokuwa siku za mwisho” (mstari 28).



DANIELI ANAIFUNUA NDOTO: Danieli 2:31-35

Katika yake, mfalme aliona sanamu kubwa sana mbele yake. Ilikuwa na uzuri wa ajabu na ilikuwa na mwangaza sana na kuonekana kwake kulikuwa kwa kutisha sana.



KICHWA cha sanamu kilikuwa cha DHAHABU safi



TUMBO na MIKONO ilikuwa ya FEDHA



TUMBO na MAPAJA ilikuwa ya SHABA



MIGUU ilikuwa ya CHUMA



NYAYO zilikuwa ni za CHUMA na UDONGO



Na alipokuwa akitazama aliona jiwe, “lilichongwa mlimani bila kazi ya mikono” likipiga sanamu kwenye nyayo likaivunja sanamu vipande vipande. Na kwa kuwa nyayo zilipondwapondwa na sanamu yote ili anguka na kupondekapondeka. Sanamu yote ikawa imevunjika vunjika na upepo ukavipeperusha “vikawa kama makapi ya viwanja vya kupepetea wakati wa hari” (mstari 35). Lile jiwe lililoipiga sanamu hiyo likaongezeka, likaongezeka hata likawa mlima mkubwa sana likaijaza dunia yote.



TAFSIRI YA NDOTO: Danieli 2:37-45

Na hii ndiyo iliyokuwa ndoto ya Nebukadreza na Danieli akaendelea kumjulisha mfalme maana ya ndote yake yote. Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, na uwezo, na nguvu, na utukufu,” Danieli akamweleza, “wewe u kichwa kile cha dhahabu” (mstari 37, 38). Madini mengine manne yaliyofuata yaliwakilisha falme nne ambazo zingefuata baada ya ufalme wa Babeli.

FEDHA inasimama baada ya UMEDI-UAJEMI



SHABA inasimama baada ya ,UYUNANI



CHUMA inasimama baada ya RUMI



CHUMA na UDONGO



inawakilisha Ulaya iliyogawanyika.Ambapo leo tunaona baadhi ya nchi zina nguvu za kijeshi na zingine ni dhaifu.



Sanamu iliyosimama mbele zake iliwakilisha FALME ZA WANADAMU, maana kila utawala ulioonyeshwa katika sanamu ulikuwa ukitawali na wanadamu ambao hawakumjua kabisa au hawakumtii Mungu wa mbinguni. Wote walikuwa wagumu wa mioyo, wakatili na wapenda vita. Nia yao kubwa katika maisha yao ilikuwa ni kujiwezesha wao wenyewe kuwa na nguvu za kijeshi na utajiri, kwa kuyafanya maisha ya maelfu ya watu wanaotawaliwa kuwa ya umaskini na mateso kutoka kwa wanowatawala.



Leo tunaishi katika siku za mwisho za ufalme wa wanadamu.Uovu wa aina hiyo ulionekana katika ufalme wa zamani wa wanadamu, unaendelea kuonekana katika miongoni mwa viongozi siku hizi. Hawa wote ni watu wasiomcha Mungu wanaofurahia kutumia nguvu dhidi ya watu wengine na sifa na nyadhifa zao.



NGUVU ZA JIWE: Danieli 2:44-45

Jiwe linawakilisha nini? Lilikuwa ni dogo mwanzo, lakini linapiga nyayo za chuma na udongo na kusababisha sanamu yote kuharibika. Nguvu za JIWE zinawakilisha UFALME WA MUNGU.



Bwana Yesu Kristo atarudi kuangamiza falme za wanadamu. Kwanza kabisa atayaangamiza majeshi ya mataifa yote, ambayo yatakuwa yamekuja katika nchi ya Israeli kupigana na Yerusalemu (Zekaria 14:2). Kuanzia hapo ufalme wake utaongezeka mpaka utaijaza dunia yote. Ufalme huo utaanzishwa baada ya kuangamizwa kwa mataifa yote ya duniani.



Tofauti na Ufalme wa wanadamu, Ufalme wa Mungu utakuwa na mfalme mwenye busara na wa haki akitawala kwa kicho cha Mungu (2 Samweli 23:3). Atakuwa mwenye haki mwenye huruma na atawajali sana masikini na wahitaji.



(Zaburi 72 maelezo ya uzuri ajabu wa mfalme atakayetawala ufalme wa Mungu). Ulimwengu utakuwa na amani wakati wanadamu wote watakapomtii Mungu na mwisho dunia yote taijawa na utukufu wa Mungu (Isaya 9:6-7;11:9).



Hili litatokea lini? Danieli aliweza kueleza kuwa mambo haya yote yatapita katika siku ambazo sanamu yote itakuwa imesimama juu ya nyayo zake za chuma na udongo.



“Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme, ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake; bali utavunja falme hizi zote vipandevipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele” (Danieli 2:44).



FUNDISHO KWETU NI LIPI?

Ndoto ailiyomsumbua sana Nebukadreza ni ya muhimu sana kwetu kwasababu inazungumzia mambo ya siku zetu, inaelekea chini kabisa ukianzia kwenye kichwa cha dhahabu mpaka wakati wa nguvu za Jiwe zitakapofunuliwa.Na siku yoyote sasa Bwana Yesu Kristo anaweza kutokea. Yeye mwenyewe alitupatia maneno ya kututahadharisha: “Kesheni basi; kwa maana hamujui ni siku ipi atakayokuja Bwana wenu” (Mathayo 24:42). Yesu anatutaka sisi kuendelea kuwa waaminifu kwake, ili kwamba tuweze kumsaidia kuubadilisha ulimwengu uwe mahali pa kuishi penye utukufu na furaha.



Umewahi kujiuliza maswali haya haswa nyakati Hizi tulizo nazo? kama umewahi kupasoma hapa na kama hujawahi je? Umejifuza nini?





1. Nebukadreza alitaka awafundishe nini Danieli na rafiki zake waliokuwa utumwani?

2. Ni kwa nini Nebukadreza alibadilisha majina ya Daniele na rafiki zake?

3. Ni kwa nini walikataa chakula cha mfalme?

4. Waliomba wapewe nini badala yachakula cha mfalme?

5. Ni jinsi gani Mungu aliwabariki Danieli na rafiki zake?

6. Ni kwa nini Nebukadreza alikataa kuwapatia wenye hekima ndoto yake?

7. Wenye hekima walimwambia nini mfalme baada ya kukataa kuwapatia ndoto yake?

8. Danieli alijuaje ndoto aliyoota mfalme? Lingani sha na maisha haya tunayoyaishi hivi sasa

9. Ilitokea nini kwa sanamu baada yajiwe kuipiga kwenye nyayo za chuma na udongo?

10. Je jiwe linawakilisha nini?

11. Ni nani atakayeziangamiza falme za wanadamu?

12. Ufalme wa wanadamu utawekwa wapi? Mungu atusaidi sana,

Followers