Kukaa kimya haisaidii kutokutambulika,

maneno yanafunua kilichomo ndani yetu,kukaa kimya bila kupona ndani haisaidii MATHAYO 12:34


Kama una tatizo na ulimi ujue unatatizo kubwa moyoni kuliko unavyofikiria.

· Mtu mwenye maneno makali ana moyo wenye hasira.

· Mtu mwenye maneno hasi ana moyo wa woga na hofu.

· Mtu mwenye ulimi /maneno ya kulipuka ana moyo ambao haujatulia.

 Mtu mwenye maneno ya kujivuna na kujisifia ana moyo usiojiaamini,hana usalama wa moyoni.

· Mtu mwenye maneno ya kutukana ana moyo usio safi

· Mtu ambaye wakati wote ni mkosoaji na wa kulaumu ana moyo wa uchungu


 lakini upande wa pili,mtu mwenye kutia moyo siku zote ana moyo wa furaha.mtu anazungumza kwa upole ana moyo wa upendo,anayezungumza ukweli ana moyo wa uaminifu.



B. JINSI YA KUKUFANYA ILI NIWEZE KUUTAWALA NA KUUCHUNGA ULIMI WANGU:

1. PATA MOYO MPYA Ezekeli 18:31, zaburi 51

2. OMBA MSAADA WA MUNGU KILA SIKU Zaburi 141:3 huwezi kwa nguvu zako unahitaji msaada wa Mungu

Usalama wa  ulimi ni kujifunza kusikiliza na  si kuongea,
Ufikiri kabla ya kusema-jifunze nidhamu ya kusikiliza Yakobo1:19 ,Kusikiliza kutakufanya kuwa na maneno machache.Ukiwa mwepesi kusikiliza hautakuwa mwepesi kusema, kusukiliza ni sanaa,ni jambo la kujifunza ni kazi sana, mfano katika maongezi ya simu,kuiingilia kati mwingine anapozungumza,kumkata kauri mtu mwingine,kutaka kutawala mazungumzo pekee yako,n.k.

Kusikiliza listening ni tofauti na kusikia hearing,unaweza kuwa unasikia lakini husikilizi,

kusikiliza ni ngazi ya juu ya mawasiliano inayo husisha, macho, masikio,mwitikio wamwili,lugha ya mwili,hisia za mwili-ni katika kusikiliza unaweza kumjua mtu zaidi,na kuusoma moyo wake,ana uchungu kiasi gani,ameumia kiasi gani,n.k.


Tunauweza wa kusikiliza maneno 600 kwa dakika,wakati tunauwezo wa kusema maneno 150 tu kwa dakika,tofauti ya maneno 500,tunafikiria haraka kabla ya mtu hajamaliza kusema tayari tunamaliza naye sentence,Inahitaji Nidhamu.


“Maneno yetu yana nafasi kidogo sana katika mawasiliano na kufikisha ujumbe,mawasiliano ni zaidi yakuzungumza maneno.utafit wa Kodak uligundua hili –Nusu ya mawasiliano yetu ni ujumbe usio wa maneno yeyote,kutazama ,lugha ya mwili kunachukua 58% ya kuwakilisha ujumbe,sauti yetu na namna tunavyo sema 35%,maneno yenyewe hasa ni7% ya ujumbe wote.hii ni kusema maneno au kuzungumza hakuna nafasi kubwa katika mawaasiliano tofauti na tunavyofikiria na kuamini.”

Asante kwa kushiriki na sisi



Followers