JE? POMBE TUNYWA AU TUSIYWA? MAJIBU:
UTANGULIZI:Maandiko yanaongelea nini kuhusu Pombe?
Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;
mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;
na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;
hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Efeso 5:19
“Wala wevi,wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang’anyi, hao wote hawatakishiriki Utawala wa Mungu 1 Kor 6:10 –
“ Basi jiangalieni ……. Na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha Luke 21:34 –
1. Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. Ikorintho3:18
2. Hoja za watu wengi kuhusiaana na andiko hili:
Paulo akamwambia Timotheo kunywa mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lako
(1 Timothy 5:23 Ndugu yangu swali langu kwani wote wanaojazana huko bar matumbo yanawauma ? Basi leo kuna frajili na dawa nyinginezo. Zamani hazikuwepo, Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya dawa. Ni kama vile nusu kaputi ukiitumia kama dawa Mungu hana tatizo; lakini ukijidunga kwa kujifurahisha? Ni kama mtu anayebadilisha matumizi ya dawa za usingizi anajiwekea kama anasa inakuwa kama Dhambi y dawa za kulevya
Umejaa aibu badala ya utukufu; unywe nawe, uwe kama mtu asiyetahiriwa; kikombe cha mkono wa kuume wa Bwana kitageuzwa ukipokee, na aibu kuu itakuwa juu ya utukufu wako. Habakuki 2:16
Watu wanatetea kukuwa kuna nguvu inayowashukilia na kuwalazimisha kutenda wasilopenda wala kutaka,
Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.
Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.
Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu warumi 7:14
Jibu analo yeye mwenyewe anayekunywa,
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311