Je Maandiko yanaongelea nini Kuhusu pombe?

JE? POMBE TUNYWA AU TUSIYWA? MAJIBU:


UTANGULIZI:Maandiko yanaongelea nini kuhusu Pombe?

Tena msilewe kwa mvinyo, ambamo mna ufisadi; bali mjazwe Roho;

mkisemezana kwa zaburi na tenzi na nyimbo za rohoni, huku mkiimba na kumshangilia Bwana mioyoni mwenu;

na kumshukuru Mungu Baba sikuzote kwa mambo yote, katika jina lake Bwana wetu Yesu Kristo;

hali mnanyenyekeana katika kicho cha Kristo. Efeso 5:19

“Wala wevi,wachoyo, walevi, wasengenyaji, wanyang’anyi, hao wote hawatakishiriki Utawala wa Mungu 1 Kor 6:10 –

“ Basi jiangalieni ……. Na ulafi, na ulevi, na masumbufu ya maisha Luke 21:34 –

1. Msijidanganye! Mtu yeyote miongoni mwenu akijidhania mwenye hekima mtindo wa kidunia, heri awe mjinga kusudi apate kuwa na hekima ya kweli. Ikorintho3:18



2. Hoja za watu wengi kuhusiaana na andiko hili:

Paulo akamwambia Timotheo kunywa mvinyo kidogo kwa ajili ya tumbo lako

(1 Timothy 5:23 Ndugu yangu swali langu kwani wote wanaojazana huko bar matumbo yanawauma ? Basi leo kuna frajili na dawa nyinginezo. Zamani hazikuwepo, Hiyo ilikuwa ni kwa ajili ya dawa. Ni kama vile nusu kaputi ukiitumia kama dawa Mungu hana tatizo; lakini ukijidunga kwa kujifurahisha? Ni kama mtu anayebadilisha matumizi ya dawa za usingizi anajiwekea kama anasa inakuwa kama Dhambi y dawa za kulevya



Umejaa aibu badala ya utukufu; unywe nawe, uwe kama mtu asiyetahiriwa; kikombe cha mkono wa kuume wa Bwana kitageuzwa ukipokee, na aibu kuu itakuwa juu ya utukufu wako. Habakuki 2:16

Watu wanatetea kukuwa kuna nguvu inayowashukilia na kuwalazimisha kutenda wasilopenda wala kutaka,

Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini, nimeuzwa chini ya dhambi.

Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda.

Lakini kama nikilitenda lile nisilolipenda, naikiri ile sheria ya kuwa ni njema. Basi sasa si mimi nafsi yangu ninayetenda hilo, bali ni ile dhambi ikaayo ndani yangu warumi 7:14

Jibu analo yeye mwenyewe anayekunywa,

Kukaa kimya haisaidii kutokutambulika,

maneno yanafunua kilichomo ndani yetu,kukaa kimya bila kupona ndani haisaidii MATHAYO 12:34


Kama una tatizo na ulimi ujue unatatizo kubwa moyoni kuliko unavyofikiria.

· Mtu mwenye maneno makali ana moyo wenye hasira.

· Mtu mwenye maneno hasi ana moyo wa woga na hofu.

· Mtu mwenye ulimi /maneno ya kulipuka ana moyo ambao haujatulia.

 Mtu mwenye maneno ya kujivuna na kujisifia ana moyo usiojiaamini,hana usalama wa moyoni.

· Mtu mwenye maneno ya kutukana ana moyo usio safi

· Mtu ambaye wakati wote ni mkosoaji na wa kulaumu ana moyo wa uchungu


 lakini upande wa pili,mtu mwenye kutia moyo siku zote ana moyo wa furaha.mtu anazungumza kwa upole ana moyo wa upendo,anayezungumza ukweli ana moyo wa uaminifu.



B. JINSI YA KUKUFANYA ILI NIWEZE KUUTAWALA NA KUUCHUNGA ULIMI WANGU:

1. PATA MOYO MPYA Ezekeli 18:31, zaburi 51

2. OMBA MSAADA WA MUNGU KILA SIKU Zaburi 141:3 huwezi kwa nguvu zako unahitaji msaada wa Mungu

Usalama wa  ulimi ni kujifunza kusikiliza na  si kuongea,
Ufikiri kabla ya kusema-jifunze nidhamu ya kusikiliza Yakobo1:19 ,Kusikiliza kutakufanya kuwa na maneno machache.Ukiwa mwepesi kusikiliza hautakuwa mwepesi kusema, kusukiliza ni sanaa,ni jambo la kujifunza ni kazi sana, mfano katika maongezi ya simu,kuiingilia kati mwingine anapozungumza,kumkata kauri mtu mwingine,kutaka kutawala mazungumzo pekee yako,n.k.

Kusikiliza listening ni tofauti na kusikia hearing,unaweza kuwa unasikia lakini husikilizi,

kusikiliza ni ngazi ya juu ya mawasiliano inayo husisha, macho, masikio,mwitikio wamwili,lugha ya mwili,hisia za mwili-ni katika kusikiliza unaweza kumjua mtu zaidi,na kuusoma moyo wake,ana uchungu kiasi gani,ameumia kiasi gani,n.k.


Tunauweza wa kusikiliza maneno 600 kwa dakika,wakati tunauwezo wa kusema maneno 150 tu kwa dakika,tofauti ya maneno 500,tunafikiria haraka kabla ya mtu hajamaliza kusema tayari tunamaliza naye sentence,Inahitaji Nidhamu.


“Maneno yetu yana nafasi kidogo sana katika mawasiliano na kufikisha ujumbe,mawasiliano ni zaidi yakuzungumza maneno.utafit wa Kodak uligundua hili –Nusu ya mawasiliano yetu ni ujumbe usio wa maneno yeyote,kutazama ,lugha ya mwili kunachukua 58% ya kuwakilisha ujumbe,sauti yetu na namna tunavyo sema 35%,maneno yenyewe hasa ni7% ya ujumbe wote.hii ni kusema maneno au kuzungumza hakuna nafasi kubwa katika mawaasiliano tofauti na tunavyofikiria na kuamini.”

Asante kwa kushiriki na sisi



kwa nini ulimi ni hatari,

KWANINI NAPASWA KUWA MAKINI NA ULIMI WANGU?

je Unajuwa ulimi wako unakokupeleka?

Kielelezo cha usukani na lijamu.Ukitaka kujua utakuwa wapi au vipi miaka mitano ijayo akangalia nini unazungumza zaidi leo juu yako mwenyewe,maneno yetu yana tupa uelekeo wa kule tuendako.unaongea juu ya nini zaidi?.



“ulimi unatawala mwelekeo wa maisha yako.ulimi ni usukani wa maisha yako,ni mfumo wako wa uongozi wa maisha yako Ukitaka kumbadilisha mtu anvyoamini,mbadilishe vile anavyo zungumza,vile unavyozungumza mwisho wa siku nindivyo vile unavyoamini.”





yale unayo yazungumza sana,mara kwa mara mwisho wa siku ndivyo utakayo yaamini. wazo Huiingia katika ufahamu,kasha katika MOYO,MANENO hutoka moyoni na kasha MATENDO huzaliwa.(MITHALI 18:20)

Nukuu: Martin LUTHER-“huwezi kuzui ndege wasiruke juu ya kichwa chako,lakini unaweza kuzuia wasijenge kiota na kuhamia hapo”



2. ULIMI WANGU UNAWEZA KULETA UHARIBIFU NA MADHARA KWANGU NA KWA WENGINE




Kielelezo cha moto na mnyama mkali asiyefugika.Mithali 21:23 18:21 Madhara makubwa sana yameletwa na ulimi,ndoa zimevunjika, urafiki,mahusiano,makanisa ,ndugu,wamekosana n.k ulimi unasabisha magovi,chuki n.k ULIMI unadhuru unaitwa mishale…una dhuru hata mbali.Neno moja liweza kusababisha “chain reaction”unaweza kuzungumza kitu ambacho hudhamiria kilete madhara lakini matokeo yake makubwa yasiyozuilika.



3. ULIMI WANGU UNA NIDHIHIRISHA VILE MIMI NILIVYO


Kielelezo cha chemchemi namti wa matundaYAKOBO 3:9-12Watu wengi wanafikiri labda kukaa kimya pekee yake kunasaidi,cha muhimu zaidi ni ndani yako kukukojeMfano wa kisima/chemichemi na mfano wa mti na matunda-Kile kilichopo katika kisima ndicho kitakacho toka na kuwepo katika maji,kadharika kilichopo katika mti kitajidhihirisha kwa njia ya matunda.

ubarikiwe sana asante kwakushiriki na sisi hapa


Vikwazo vya Aliyetumwa


Kila aliyetumwa, Lazima akumbane na vikwazo,
Kutuma-
 ni hali ya kupewa ujumbe kwa ajili ya kupeleka palipo kusudiwa. Unaweza ukawa ujumbe wa familia au nchi. Mungu naye Ana kawaida ya kuwafumba watu duniani na Jumbe mbalimbali…

Maandiko yanayotaja uweza wa Mungu wa kutumia watu.

Kama hutaki matatizo mwachie aliyetumwa, kwa desturi Mungu huwa anatuma watu duniani na hii ni desturi ya Mungu.
Yeremia 49:14 . 14 Nimepata habari kwa Bwana, Na mjumbe ametumwa kati ya mataifa, Akisema, Jikusanyeni, mkaujie, Mkainuke kwenda vitani.



Na hawa watu hutumwa kwa makusudi mbalimbali
 Kutoka 23:20 Kwa kuwa malaika wangu atatangulia mbele yako, na kukufikisha kwenye Mwamori, na Mhiti, na Mperizi, na Mkanaani, na Mhivi, na Myebusi; nami nitawakatilia mbali.


Usiisujudie miungu yao, wala kuitumikia; wala usitende mfano wa matendo yao; bali utaiangamiza kabisa, na nguzo zao utazivunja vipande vipande.

 malaki 3: 1,Angalieni, namtuma mjumbe wangu, naye ataitengeneza njia mbele yangu; naye Bwana mnayemtafuta atalijilia hekalu lake ghafula; naam, yule mjumbe wa agano mnayemfurahia, angalieni, anakuja, asema Bwana wa majeshi.


 Lakini ni nani atakayestahimili siku ya kuja kwake? Au ni nani atakayesimama atakapoonekana yeye? Kwa maana yeye ni mfano wa moto wa mtu asafishaye fedha, ni mfano wa sabuni ya mtu afuaye nguo;

 mathayo 11:10 , Huyo ndiye aliyeandikiwa haya, Tazama, mimi namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako mbele yako.


 watu wa dunia hii kwa kumuonea mtu anakupa pamoja nao, au anaishi katikati Yao huisikia kuwa hajatumwa, lakini hata kwenye biblia watu waliotumwa walikuwa wanaishi na kula kama watu wengine.

mifano ya watu waliotumwa kwenye biblia.

Marko 1:2  Kama ilivyoandikwa katika nabii Isaya, Tazama, namtuma mjumbe wangu Mbele ya uso wako, Atakayeitengeneza njia yako.
huyu ni Yohana mbatizaji, alitumwa kuandaa njia kwa ajili ya Yesu .

Hata Yesu mwenyewe alikuwa ametumwa Kutoka mbinguni lakini alitungwa mimba, akazaliwa, na Akaishi Kama watu wengine, Hesabu 20:16 tena tulipomlilia Bwana, akatusikiza sauti yetu, akamtuma malaika, na kututoa tutoke Misri; nasi tupo hapa Kadeshi, mji wa mpakani mwako mwa mwisho;
Mungu anatabia ya kutumia. 2Samweli 12:1 zaburi 105:26. Mathayo 21:37 waamuzi 6:28 Mungu anatabia ya kutuma watu.

Mfano wa wanasayansi.

Wanasayansi wengi wa zamani amabao walikuwa wakristo na ni wavumbuzi wa zamani wa sayansi, mfano 1. isaack newton, 2. Boyle, na watu Kama wakina 3. kelvin waliogundua umeme hawa watu walikuwa wameokoka na hawa waligundua vitu mbalimbali. 4. Michael faraday Kama tulivyoona wagunduzi wa zamani wengi wanakubali kuwa Mungu yupo. 5. John Rey, 6. Creg Maxwell 7. Caros Linus, 8. Kepler. waliokuwa wameokoka.

Lakini ukiangalia maisha yao binafsi, utagundua maisha yao yakipita mambo magumu,

Mfano: isaack newton mama yake akiwa mjamzito, baba yake akafariki … Hivyo mama yake akaenda kuolewa na mume mwingine, Na hapo newto akaenda kuishi kwa mjomba yake na katika maisha magumu na kutokana na maisha magumu yale , yakamfanya newton akazane kusoma kumbe mtu aliyetumwa kuibadili dunia na hapa lazima dunia imshikilie na kumzuia, lakini mwisho wa siku alikwenda na kumaliza wito wake.

Mfano mwingine ni Robert Boyle naye alizaliwa kwenye shida pia, Faraday pia Alipitia wakati mgumu kwenye maisha yake.

Maisha halisi ya sasa.

Tunapozungumzia kutumwa ni neno pana sana na hapa inaweza ikawa mtu katumwa kubadili nchi, familia, nyumba na Hali ya jamii nzima. Lakini dunia hii tuliopo ina system mbalimbali mfano. Dini, serikari, jeshi ambavyo vinazuia ujumbe wa aliyetumwa. Marko 1:2 , “palitokea mtu ametumwa…..” unajikuta unakiu ya jambo fulani kufanikiwa, una kiu ya kufanikisha kitu fulani kinaweza kuwa cha familia au cha taifa na hapo hali ya maisha na umaskini ina kuzuia, na hii ni kawaida ya dunia kujaribu kuwashikilia watu waliotumwa..

Kumbe inawezekana kuwa Mungu amekutuma duniani, na hujijui na kwa vile dunia ilivyokushikilia inakufanya hata usahau kuwa umetumwa. Mfano: inawezekana umetumwa kuwa waziri wa mambo ya nje na hapo inakubidi upate elimu angalau, lakini dunia inakuzuia kwa kukuletea umaskini ili ukose elimu na mwisho wa siku ushindwe kufikia kwenye kule ulipotumwa.

Msaada kutoka kwa Mungu kwa Yule aliyemtuma.

Kama tulivyoona Mungu anadesturi ya kutuma malaika, binadamu ili kuitengeneza dunia kuishape dunia kuileta mahala pake… Na Mungu ili kuwasaidia aliowatuma huitikisa dunia kwa jambo fulani ili kufanya wale aliowatuma waingie kwenye system, na hapa ndio maana unaona hata nchi Kama Tanzania inapitia kwenye mtikisiko ikionyesha kuwa kuna watu waliotumwa na wanakusudiwa kuingia kwenye nafasi zao.

Mfano mwingine ni wa Ibrahim , ambaye ni baba wa Imani, na huyu aliahidiwa kuwa baba wa mataifa na ili kuwa baba wa mataifa lazima azae awe na watoto, lakini dunia( shetani) akaanza kupinga hiyo, kwa kumwekea utasa, na hapa tunajifunza kuwa kwa kila mtu aliyetumwa lazima atakutana na upinzani.



Mfano mwingine ni Musa , na Musa alipozaliwa tu , shetani akajua na alitumwa na Mungu kuunda taifa imara, la Israel na ndio maana alipozaliwa tu, Farao akaamuru watoto wote waangamizwe, na hapa tunajifunza kumbe ukiwa na kitu kikubwa cha Mungu , lazima utapingwa na kuzuiwa. Lakini Musa kimuujiza alienda kula mezani mwa Farao. Bila Farao kujua hadi wakati wake hutimie.

Kumbe aliyetumwa hawezi kuangamizwa hadi atimize hatma yake.

Kwahiyo Mungu anakwaida ya kuwasaidia wale aliowtuma, tunaona katika habari ya Musa alipokuwa mdogo, na hata yale mapigo aliowaandalia wamisri,

Mfano mwingine wa taifa la Israel, kipindi Sauli alipofanya machukizo… Mungu akamtuma nabii Samuel kwenda kumpaka Mafuta mfalme Daud . Mungu anakawaida ya kutuma watu. kwa hiyo samweli akamchagua na kumtia Mafuta daudi.

Vitu ambavyo vilimshikilia Daud Kama mpakwa mafuta.

1. Kudharuliwa na ndugu zake.

2. Yuko machungoni polini.

3. Alidharauliwa na watu wa taifa lake.

Lakini pamoja na yote daudi aliishia kuwa mfalme sawasawa na alivyoitwa.


Jambo la kufanya:

Ni muhimu kupambana vita vya kiroho ili kuondoa vizuizi vya dunia, ambavyo vinazuia watu waliotumwa… Kwa hiyo ni muhimu kusambaratisha nguvu ya shetani ili kutuachia watu tuliotumwa.

Mungu akubariki sana, kwakushiriki nasi,



Kafara maana yake nini?

 Ukiongelea Madhabahu kimsingi tunazungumzia vitu
vitano.. yaani kuhani wa madhabahu , Mungu wa madhabahu , Nguvu ya madhabahu ( moto wa madhabahu) , kafara ya madhabahu na madhabahu yenyewe .. na kwa leo tujikite zaidi kwenye neno hili kafara ya madhabahu


KAFARA YA MADHABAHU
Nini maana ya kafara?

Kwa akili zawatu zilivyo wakisikia neon kafala wanakimbilia kwenye waganga wa kienyeji.. lakini neno hili kafara kwenye biblia ndio linaitwa dhabihu kwenye biblia.. kuna maadiko kadhaa yanayo taja kafara kwenye biblia kama ifuatavyo :- mambo ya walawi 2 :2, 9, 16; mambo ya walawi 10 : 13, 14.. maandiko haya yanataja neon kafara kwenye biblia .. na limeonekana mara nyingi.. hii ni kukuonyesha kuwa neno kafala lipo kwenye biblia na lina maana sahihi.. kwahiyo Kafara ni sadaka inayotolewa kwa ajili ya kupokea jambo fulani kutoka ulimwengu wa roho aidha kwa Mungu au kwa shetani..

Ni Muhimu kujua matatizo mengi ya watu yanasababishwa na kafara zinazotolewa.. .. na shetani amewafunga watu wasijue vyanzo vya matatizo yao na kufungwa huku ndio biblia anaita “mafumbo ya kishetani” Ufunuo 2: 24-25 na kwa namna hii shetani amewapofusha watu wasijue siri hii ndio maana hata baadhi ya wakristo wamefungwa wasijue siri hii..

Kwa desturi watu hupanda ngazi kwenye maisha kulingana na sifa zao na haki, lakini watu wengine kwa kutumia njia ya mkato wanatoa kafara ili kuwa funika wengine na kuchukua nafasi zao.. Yeremia 32 :35 1wafalme 16 : 34 tunaona hapa kwenye hili andiko, maana Joshua alipoubomoa ukuta wa Yeriko akaweka kanuni nya kuwa yeyote atakaye taka kujenga atafiwa na mwanaye pale atakapo anza na atakapo fika katikati atafiwa na motto mwingine … lakini tunaona Hieli mbethel akaamua kumtoa kafara mwanaye kwa kuweka misingi na tena akamtoa kafara mwanaye mwingine..


Tunaona hapa kuwa kafara na kutoa kafara hayakuanza leo bali yalianza tangu kipindi cha cha zamani kwenye biblia.. 2 wafalme 3:24-27 hapa tunaona wayahudi wakavamia Moabu na wakakaribia kuteka mji wa Moabu na hapa ndio maandiko yaasema ndipo alipomtoa mwanaye ambaye angekuwa ni mtawala badala yake kwenye ukuta ili wayahudi wasiweze kuwavamia..


Ndio maana ni rahisi kumkuta mtu anasikitika kuhusu matatizo yake., lakini ni Muhimu kujua watu wa duniani hutoa kafala ili apate ushindi katika maisha na kwa njia hii hufunika wengine.. ndio maana kuna aina ya mashetani yanaitwa mizimu hawa sio roho za watu waliokufa bali ni mashetani waliokaa muda wa kutosha nafamilia hadi wakajua tabia zenu na pale mtu anapoenda kutoa kafara anakuwa anayaalika yale mapepo nyumbani au kwenye ukoo husika.. na ndio maana ni rahisi kukuta ukoo mmoja kuwa na matatizo yanayo fanana..



Kimsingi waganga wa kienyeji hutumia kafala kuwafunga watu, na ndio maana ukienda kwa mganga atakutaka ulete kafara aidha ya kuku au ya mbuzi kwa maana kwa mganga wa kienyeji ni madhabahuni pa shetani… na wachawi pale ile damu inapomwagika mashetani anamiminika pale na kufanya vile kafara inavyowataka wafanye.

Ndugu zangu kuna watu hata hawapendi kukuona unakula vizuri, au unapika vizuri au unasomesha.. na akiona huo wivu anaamua kwenda kukufanyizia kwa mganga wa kienyeji..ambapo ataambiwa atoe kafara kwa ajili ya kukuangamiza wewe..


1wakorintho 10:2020
 Sivyo, lakini vitu vile wavitoavyo sadaka wavitoa kwa mashetani, wala si kwa
Mungu; nami sipendi ninyi kushirikiana na mashetani. Hamwezi kunywea kikombe cha Bwana na kikombe cha mashetani.


21 Hamwezi kushirikiana katika meza ya Bwana na katika meza ya mashetani.

22 Au twamtia Bwana wivu? Je! Tuna nguvu zaidi ya yeye?
 .. zaburi 126:38 kumbe kuna uwezekano wa watu kutoa kafara kwa mashetani. Na biblia inalikubali hili kupitia maandiko hayo tuliyoyaona hapo.. unaweza kuwekewa pepo la udhaifu kupitia kafara.. Luka 13:10 Pepo wa udhaifu.. mtu anaweza kukutolea kafara ili ufe kifo cha Ghafla..



Kwetu tuliookoka..


Unapomkubali Yesu unakuwa umejiunganisha na mauti ya Yesu hivyo hakuna haja ya kutoa kafara tena.. maana Yesu alifanyika kafara kwa ajili yetu na damu ya Yesu ilimwagika ili kutufungua wote na Yesu alipigwa na kufa ili sisi kutookoa kama kafara kwaajili yetu.. watu wa dunia wanaweza kwenda kwa waganga na kutoa kafara lakini sisi tuna Damu ya Yesu ambayo ni nguvu ya madhabahu yetu..


Hivyo sasa kwa kutumia damu ya Yesu unaweza sasa kuharibu kafara na madhabahu zao zote,, ukishughulikia madhabahu na kafara unakuwa umeiangamiza nguvu ya madhabahu nza kishetani na tatizo ulilonalo litakwisha .. kwahiyo ni muhimu kuharibu makuhani wa madhabahu yaani wachawi na waganga, madhabahu yenyewe yaani wanapokusanyikia, inatubidi kubomoa kafara yao, nguvu yao na pia Mungu wa madhabahu zao ambazo ni shatani.. na hapo utapata ushindi mkamilifu..


Mathayo 17:14 utajiuliza inakuaje, Yesu anaamua kumtoa pepo wakati tatizo lake lilitajwa ni kifafa, hapo utagundua kuwa matatizo ya watu wengi yanatoka na mapepo au majini yanayo tumwa na kumfanya awe vile alivyo.. lakini unatakiwa ushughulikie madhabahu na mambo yanayofuatana nayo…

Balozi wa serekali ya mbinguni



Maana ya kuzimu na mauti




Kila jambo lina nguzo linazozitegemea, na kila utawala una nguzo unaotegemea.. vilevile utawala washetani umejengwa juu ya nguzo ziitwazo MAUTI na KUZIMU.. Ayubu 38:18 na nguzo hizi mbili ndizo ambazo zinashikilia utawala wa shetani na ndio maana maeneo mengi ambayo kuzimu inatajwa basin a mauti ipo pia.. mfano katika kitabu cha zaburi 116 :3 .. HAPA UTAONA kila mahali ambapo mauti imetajwa basi kuna mahusiano na kuzimu ..



MAANA YA MAUTI NA KUZIMU :

MAUTI ni roho ambayo kazi yake ni kuuondoa uhai ulio ndani ya mtu. Na KUZIMU ni roho ambayo kazi yake ni kuwahifazi wale waliokufa.. ufunuo 6: 9, Isaya 28 :15 ..



Mauti ni roho yenye akili na yenye kupanga.. ndio maana wanafunzi wa Yesu , walipomuona Yesu yuko juu ya maji, biblia inasema wanafunzi wa Yesu wakadhani wameona roho.. kumbe roho ina personality ina akili kili, inaweza kupanga na kutekeleza na pia yaweza kumpagaa mtu. Kwahiyo mauti ni roho yenye personslity hapo tunaweza sema mauti ni mtu.. Tunaweza sema mauti ni mtu ina “personality” ufunuo 20 : 13.. mauti inaweza kumeza watu..



ufunuo 20 : 14 kila mahali inapotajwa mauti kuzimu inafuata pale, hii inaonyesha kuwa mauti inaanza alafu kuzimu inafuata.. katika hiki kitabu cha ufunuo 20 : 14 tunaona kuwa “ mauti na kuzimu vikatupwa kwenye jehanamu” kumbe mauti unaweza uka ikamata kabisa na kuitupa mahali.. kama mauti na kuzimu vingekuwa ni matukio basi visingeweza kushikwa na kutupwa kwenye moto. Ndio maana Yesu alipokufa alishinda mauti na kuzimu. ( yohana 20 :3)



tuangalie hili andiko mwanzo 37:25 katika agano la kale kuzimu lilikuwa linatumika kama mahali wafu walipokuwa wanakwenda, na palikuwa panaitwa “sheol” kwa lugha ya kingereza na huko wako wafu wote waliotenda haki na walitenda maovu walikuwa wanakwenda kule.. lakini palikuwa wamepagawa mahali pa watenda haki na mahali pa watenda maovu.. na mahali walipokuwa wanaenda watenda palikuwa panaitwa Kifuani pa Ibrahimu, ( yaani wale walioamua kuungana na imani ya Ibrahim) na sasa kunaitwa paradiso..



TOFAUTI YA JEHANAMU NA KUZIMU:



Jehanamu ni shimo la rohoni la moto watakapo angamizwa watu watendao dhambi, kwasasa jehanamu hakuna mtu ndani maana hukumu bado haijatolewa lakini watu wanaokufa kwa sasa wanaenda kuzimu (bottomless pit) hii ni roho iliyojifunua kama shimo. Isaya 14:11,15 . tunaona shetani alipoasi akatupwa kwenye hilo shimo ndio maana ya maneno yaliyo katika kitabu cha ufunuo 12:7-9 kumbe kuzimu ipo hapa katika nchi, hapaonekani kwa kuwa lipo katika ulimwengu wa roho. Ufunuo 9:15 , KUZIMU ndio kwenye makao makuu ya shetani , wanakofanyia kazi zao.. (operation centre) ufunuo 17:8 .. kwa hiyo ni muhimu kujua kuzimo ipo angani, baharini na hata kwenye nchi.. ndio maana biblia inataja mara nyingu neon hili wakuu wa anga’



KAZI ZA KUZIMU NA MAUTI.


Kuzimu ndio inayo achilia uovu duniani, inaachilia magonjwa, tabu, dhambi, mateso, balaa,mikosi, ukimwi, kuchanganyikiwa, kuchukiwa na watu, inadhoofisha, inatesa na inaleta uhalibifu.. kwahiyo kuzimu inaleta roho ya uzinzi na uasherati, uovu na dhambi na hizi zote zinamfanya mtu kudhoofika na kuishiwa nguvu. Hapo sasa mauti ndo inakuja pale mtu anapokuwa kwenye comma. KWAHIYO kuzimu kazi yake ni kudhoofisha kwanza.. na ndio maana unaweza muona mtu anaumwa hadi kudhoofika sana lakini huyo mtu hafi.. hii ni kwasababu mashetani ya mauti hayajaanza kufanya kazi..


Hapo mgonjwa anapokuwa dhaifu ndipo sasa mauti inakuja na kufanya kazi yake, ya kumuua . na mauti ikifanikiwa kuutoa uhai basi sasa mauti inatuma mapepo wa kuja kumchukua Yule mtu kama alikuwa mtenda dhambi.. na ndio maana utaona kuwa mtu anapotaka kufa waliowengi utawasikia wanasema maneno kama ‘naona giza’ au msinichukue’ basi ujue wakati huo.


Kuzimu inaleta duniani hata mitindo ya kuvaa.. ili kuingiza tamaa za uzinzi na uasherati.. na unapoona tamaa ya dhambi inaongezeka basi jua unakaribia kufa.. kama ulipangiwa kuishi miaka 80 utajikuta unaishi miaka 40.. kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti.

Marko 16 :19-22.. Mtu anapokata roho anachukuliwa na malaika kwenda mbinguni au anachukuliwa na malaika kwenda kuzimu..


NGUZO MBILI ZA KIPINDI CHA SAMSON

SAMSON alikuwa mnadhiri alikuwa na jukumu la kuangamiza wafilisti, lakini wafilisti walimnasa baada ya kudanganywa na mkewe, ILI kutoa siri ya nguvu zake, baada ya kujua wafilisti wakmnyoa nywele , wakamtoboa macho na kumweka asage ngano, mfano huu wa Samson unaonyesha hali ya kanisa ya sasa baada ya kanisa kukosa nguvu, na kudharauriwa Mungu ameanza kulipa nguvu kanisa kama nywele za samason zilipoanza kuota.. Samson alipopata nguvu akajitegemeza kwenye nguzo mbili ambazo jingo linazitegemea. Na akazitikisa hadi jingo lote likaanguka kabisa. Ndivyo kanisa linavyotakiwa kuwaangamiza nguzo za mauti na kuzimu.. ili liweze kurudi kwenye uweza wake na ndio maana ushindi wa Yesu msalabani kimsingi ni ushindi dhidi ya mauti…

Na balozi wa serekali ya Mbinguni




Fahamu mambo machache, yanayokuchosha tofauti na huduma

SABABU YA KUCHOKA SANA:


1. Kazi nyingi kupita kiasi

2. Kuwa mtu wa kukubaliana kila kitu na mkuu wako au bosi wako.

3. Kuhisi umekwama katika ujuzi wako/taaluma yako.
4. Kuwa mlevi wa kazi5. Kulazimishwa katika mazingira yanayokukandamiza. Kuona una majukumu kupita kiasi

6. Kufanya kazi na wateja ambao hawana mwitikio na ushirikiano. Matatizo ya kifamila kama fedha.

7. Mafanikio ya uponyaji.


TIBA YA UCHOVU
1. Jifunze kuweka mipaka.



● Jifunze kuwa na hisia za uchechi-uwe rahisi na unaye weza kukalibiwa kirahisi. Tengeneza mtandao usiwe mpweke, gawa majukumu kwa wegine. Unapokuwa peke yako kimbia kwa kasi lakini kwa muda mfupi.mnapokuwa wengi kimbia taratibu lakini kwa muda mrefu..

2. Uwe na shughuli nyingine mbali na shughuli za kanisa,kama vile michezo,matembezi.


3. Wakati wote tunza akilini mwako lengo yako.


4. Jifunze kuthamini kudhihirisha hisia hasi zako.


5. Hudhuria semina mahali kwingine,katika makanisa mengine na maeneo mengine.


6. Tengeneza tabia ya kupumzika –chukua siku moja kupumzika katika wiki na chukua likizo ndefu.


7. Chukua tabia ya afya njema:kula vizuri,fanya mazoezi,lala vizuri.



JINSI YA KUZIMA HALI YA KUCHOKA


1. Shughulikia mfadhaiko wako kwa kufanya mazoezi ya viungo


● Tumia mazoezi rahisi.


● Andiko maneno rahisi hewani kama vile Jina lako n.k. kwa kutumia mwili waka au mwenendo wa kichwa.

● Chukua siku moja ya kupumzika.


2. Tawala muda wako.-usihairishe mambo,uwe na orodha ya mambo ya kufanya.


3. Gawa majukumu,epuka kujitegemea mwenyewe.


4. Pata uwajibikaji-mthibitishe mtu unayemwamini.


5. Fanyaia kazi nidhamu za kiroho kama vile Maombi,Kusoma Biblia,kufunga,n.k..



tiba ya uchovu ya Huduma

1. Badilisha Eneo,toka nje ya eneo na mazingira yako ya huduma


2. Badilisha shughuli-pumzika

3. Badilisha Muda

4. Badilisha Vipaumbele vyako

· Wewe na Mungu-maisha yako binafsi ya Kiroho
· Wewe na Mke wako-maisha yako ya ndoa,hakuna ndoa ,hakuna huduma yako.

· Wewe na watoto wako-familia –Kanisa huanza nyumbani

· Wewe na Huduma.

· Wewe na watu wengine
Dumu katika neno La Mungu

Sababu za Mtumishi kuvunjika moyo katika huduma

. DALILI  AU ALAMA ZA KUCHOKA KATIKA HUDUMA  YAKO



Kuna aina mbili za dalili za kuchoka –dalili za ndani na dalili za nje


. DALILI ZA NJE NI PAMOJA NA MAMBO YA FUATAYO

· Kuongezeka kwa shughuli lakini uzalishaji/ufanisi unabaki uleule, ambao unaitwa uwendawazimu insanity-kufanya jambo lilelile kwa muda mrefu na kupata matokeo yale yale. Kuwa na shughuli nyingi si Kiroho.Kimsingi unapaswa kutumia nguvu kidogo tu na kuwa na matokeo makubwa-maarifa ni ya muhimu zaidi ya nguvu na bidii nyingi.

 Kuchoka kimwili,kuishiwa nguvu-kuchoka mfululizo ni dalili ya Burn-out,kujiona hupendi kufanya jambo lolote lile.Kupenda kulala tu,kuona kero kuamka hasa alfajiri.

 Kutokuwa tayari kujihatarisha au kuthubutu-kukwepa changamoto katika huduma,kukwepa watu na marafiki,kupoteza imani juu yako mwenyewe na kupoteza uwezo wa kukamilisha mambo.

· Kukwazika kirahisi/kukasirishwa na mambo na watu ,hata Mungu mwenyewe kirahisi- Musa na Yeremia ni mfano mzuri –Hesabu 11:11 Yeremiah 20:7,

 Kukosa usingizi ,kupoteza hamu ya kula,Kuwa na mawazo mengi,kupenda kuwa pekee yako , “kujificha katika upweke”


Kupooza /stroke,shinikizo la moyo,kipanda uso,kichwa kuuma mara kwa mara

 Matatizo ya kuyeyusha chakula,matatizo katika utumbo mkubwa (coronary problem),vidonda ya tumbo/ulcers.


. DALILI ZA NDANI NI PAMOJA NA MAMBO YAFUATAYO:


 Kupoteza ujasiri

 Kupoteza kujiamini na uthamani wako binafsi

· Kuwa na mtazamo hasi

 Kupoteza makusudi- kumwona Mungu ni chanzo cha kushindwa kwako,kujikasirikia mwenyewe kwa kushindwa kufikia malengo

 Kuchoka kihisia,depression,mkandamizo

 Hatia ya kujiona hufanyi vya kutosha,huna matokeo ya kutosha, na kufikiri pengine ukiongeza bidii nyingi ndipo utaona matokeo,kwa wengine hupelekea kufunga sana mfululizo kuomba sana,kukesha sana,wakifikiri kwa kufanya hivyo kutakuwa na matokeo kinyume chake,hupelekea uchovu zaidi na hakuna matokeo.

 Martha complex-kuwa na shughuli nyingi sana na kukosa muda binafsi wa Mungu kukuhudumia


. Kuanza kuwadharau watu ulioitwa kuwapenda na kuwahudumia

. Unaanza kurushu mawazo yako kuchukuliwa na mambo mengine ambayo ungeweza kuyafanya zaidi yakufanya huduma .

. Unajihisi ni kama “mashine ya huduma” hivyo unafanya yale ufanyayo ukiwa na hatia ya kwamba ni Lazima uyafanye badala ya kutenda kwako kutokane na kutembea kwako karibu na Mungu(Mahusiano),kazi ya Bwana Vs Bwana wa Kazi.Juhudi vs Ufanisi.


. Unaanza kufanya maaumzi kulingana na nini ni rahisi kuliko vile unavyojua ndivyo Mungu anakutaka ufanye.


. Unazidi kuwa mkosoaji na kupita kiasi juu ya makanisa,watu,na huduma za watu wengine ambazo unafikiri Mungu anazibariki kuliko huduma yako na wewe


. Hukumbuki lini mara ya mwisho ulifungua Biblia kwaajili kwaajili ya ushirika wako binafsi na Mungu,bali ni kwaajili ya kutafuta Mahubiri na Masomo ya kufundisha Biblia


. Unaanza kuwaona watendakazi wanaotumika pamoja na wewe kama watumishi wako badala yakuwaona kama ni watumishi wa Mungu.

 Unatumia kugawa majukumu kama udhuru ya kuwa mvivu,una kwepa majukumu kwa kuwagawia wengine wafanye.

. Hukumbuki mara ya mwisho ni lini ulikuwa na mazungumzo na mke wako ambayo haya husiani na mambo ya kanisa

Hukumbuki mara ya mwisho ni lini ulitumia muda na watoto wako na mkafurahia pamoja.

. Unaanza kutilia mashaka nguvu za Mungu ndani yako na ndani ya maisha ya watu wengine.



Nguvu ya Kusikia



Nguvu ya kusikia
Utangulizi:

 CHANZO CHA IMANI



  warumi 10:17, “Imani chanzo chake ni kusikia; na kusikia huja kwa neno la kristo.” Mambo ya kujifunza ni kuwa imani chanzo chake ni kusikia, tukiishia hapo tunajifunza kitu hapa, tukiangalia kwenye biblia utagundua baada ya neno kusikia kuna alama ya mkato ikimaanisha imani chanzo chake ni kusikia. Kumbe imani yoyote ya kushindwa au ya kushindwa yanatokana na kile unachosikia.


Kama tulivyoona kwenye andiko hapo juu, kuwa imani inaandia kwenye kusikia. “masikio yetu yanaweza kutupelekea katika kuanguka au kuinuka” ni muhimu kujua kila unachosikia kinaleta IMANI ndani ya mtu, ambayo yaweza kuwa nzuri au mbaya kutegemea kile ulichosikia. Na ndio maana , shetani hutumia sana masikio kuwafanya watu wamtumikie yeye.

.1 Uzuri wa kusikia.

Unaponahabari za Mungu, na neno la kristo basi imani na nguvu ya Mungu itaingia kwenye maisha yako. Kwa maana hata wale wakoma walisikia neno kutoka kwa kristo. Na hapo wakapata imani ya kuchukua hatua na baada ya kuchukua hatua ya kuamua kwenda kujionyesha hapo wakapokea utakaso wao.. lakini la kujifunza hapa ni kwamba imani yao imepatikana baada ya kusikia NENO kutoka kwa kristo.

 Hatari ya mambo tunayoyasikia.

Ni muhimu kujua kile unachosikia kina leta kesho yako, “maisha unayoishi leo ni matokeo yayale uliyowahi kusikia” na ndio maana shetani anatumia hiyo kukamata na anataka usikie mambo mabaya ili utende mabaya. Na ndio maana ukifuatilia kwenye maisha yako huwezi kukumbuka kama kuna mtu aliyewahi kukufundisha dhambi, lakini unajikuta unatenda kwa kuwa habari za dhambi zimeenea zaidi kuliko taarifa za nuru.

3. MAPENZI YA MUNGU

2 Timotheo 4:7 “nimevipiga vita vilivyo vizuri, mwendo nimeumaliza, imani nimeilinda”. Yohana 10:10 “mwivi haji ili aharibubu,kuua na kuchinya lakini mimi nilikuja ili muwe na uzima tele” kumbe kazi ya Yesu duniani ni bayana nay a shetani ni bayana.. Paulo alisema amemaliza kazi ya kristo. Na ndiomaana neno imani linaingia pale, kwasababu huwezi kutenda kazi ya kristo bila kuwa na imani ya YESU ndani yako. Na imani chanzo chake ni kusikia kumbe unaposikia habari za kristo unajikuta unatenda kazi ya kristo. Na unaposikia habari za upande wa shetani utajikuta unatenda kazi za shetani.

Unalolisikia laweza kukuingiza kwenye laana nau Baraka. Jifunze kusikia neno la Mungu. Nandio maana biblia inasema kwenye kitabu cha 2 wakorintho 10:3-5 “tukiteka nyara kila fikra” kumbe fikri zetu na mawazo yetu ni muhimu yawe katika kumtii Mungu , lakini ili fikra iweze kumtii Mungu ni lazima isikie neno la Mungu. (warumi 10:17)



Hatuwa ya muhimu kwa muongofu

Unapoanza maisha haya mapya katika Yesu Kristo nakushauri mambo yafuatayo:




1. Zungumza na Mungu kwa maombi kila siku
(Yohana 15:7)

 Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.


Hivyo hutukuzwa Baba yangu, kwa vile mzaavyo sana; nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.
 Kama vile Baba alivyonipenda mimi, nami nilivyowapenda ninyi, kaeni katika pendo langu.

 Mkizishika amri zangu, mtakaa katika pendo langu; kama vile mimi nilivyozishika amri za Baba yangu na kukaa katika pendo lake.

Hayo nimewaambia, ili furaha yangu iwe ndani yenu, na furaha yenu itimizwe.

 Amri yangu ndiyo hii, Mpendane, kama nilivyowapenda ninyi.

 Hakuna aliye na upendo mwingi kuliko huu, wa mtu kuutoa uhai wake kwa ajili ya rafiki zake.

 Ninyi mmekuwa rafiki zangu, mkitenda niwaamuruyo.

 Siwaiti tena watumwa; kwa maana mtumwa hajui atendalo bwana wake; lakini ninyi nimewaita rafiki; kwa kuwa yote niliyoyasikia kwa Baba yangu nimewaarifu.


2. Soma Neno la Mungu (Biblia) kila siku
(Matendo ya Mitume 17:11)

Watu hawa walikuwa waungwana kuliko wale wa Thesalonike, kwa kuwa walilipokea lile neno kwa uelekevu wa moyo, wakayachunguza maandiko kila siku, waone kwamba mambo hayo ndivyo yalivyo.


Basi watu wengi miongoni mwao wakaamini, na wanawake wa Kiyunani wenye cheo, na wanaume si wachache.

 Lakini Wayahudi wa Thesalonike walipopata habari ya kwamba neno la Mungu linahubiriwa na Paulo hata katika Beroya, wakaenda huko nako wakawachafua na kuwafadhaisha makutano.

 Mara hiyo wale ndugu wakampeleka Paulo aende zake mpaka pwani; bali Sila na Timotheo wakasalia huko.


3.Mruhusu Roho Mtakatifu akutawale
(Wagalatia 5:16-25;
Lakini mkiumana na kulana, angalieni msije mkaangamizana.


 Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.

Kwa sababu mwili hutamani ukishindana na Roho, na Roho kushindana na mwili; kwa maana hizi zimepingana, hata hamwezi kufanya mnayotaka.

 Lakini mkiongozwa na Roho, hampo chini ya sheria.
Warumi 8:14-17)


 Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho wa Mungu, hao ndio wana wa Mungu.


Kwa kuwa hamkupokea tena roho wa utumwa iletayo hofu; bali mlipokea roho ya kufanywa wana, ambayo kwa hiyo twalia, Aba, yaani, Baba.

Roho mwenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu;

na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo; naam, tukiteswa pamoja naye ili tupate na kutukuzwa pamoja naye.
 Kwa maana nayahesabu mateso ya wakati huu wa sasa kuwa si kitu kama utukufu ule utakaofunuliwa kwetu.

Umtumaini Mungu kwa kila jambo katika maisha yako
 (1Petro 5:7;

 huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote, kwa maana yeye hujishughulisha sana kwa mambo yenu.


 Mwe na kiasi na kukesha; kwa kuwa mshitaki wenu Ibilisi, kama simba angurumaye, huzunguka-zunguka, akitafuta mtu ammeze.

 Nanyi mpingeni huyo, mkiwa thabiti katika imani, mkijua ya kuwa mateso yale yale yanatimizwa kwa ndugu zenu walioko duniani.

 Na Mungu wa neema yote, aliyewaita kuingia katika utukufu wake wa milele katika Kristo, mkiisha kuteswa kwa muda kidogo, yeye mwenyewe atawatengeneza, na kuwathibitisha, na kuwatia nguvu.

Zekaria 4:6)

Nami nikajibu, nikamwambia yule malaika aliyesema nami, nikasema, Ee Bwana wangu, vitu hivi ni nini?


Ndipo malaika aliyesema nami akajibu, akaniambia, Hujui vitu hivi ni nini? Nikasema, La, Bwana wangu.

Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi.

 Nani wewe, Ee mlima mkubwa? Mbele ya Zerubabeli utakuwa nchi tambarare; naye atalileta lile jiwe la kuwekwa juu kabisa pamoja na vigelegele vya, Neema, neema, ilikalie.


5. Usiache kukusanyika na kushirikiana na wengine waliompokea Yesu Kristo kuwa Mwokozi wao kama wewe ili uimarike zaid

 (Waebrania 10:25)
 wala tusiache kukusanyika pamoja, kama ilivyo desturi ya wengine; bali tuonyane; na kuzidi kufanya hivyo, kwa kadiri mwonavyo siku ile kuwa inakaribia.


 Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea ujuzi wa ile kweli, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi;

 bali kuna kuitazamia hukumu yenye kutisha, na ukali wa moto ulio tayari kuwala wao wapingao.
Mungu akubariki sana msomaji
 
Balozi wa serekali ya mbinguni
samson na mkewe wanalo neno la kinabii juu yako
kwa msaada zaidi piga 0756 809 209,


Je Unajuwa Kuwa Wewe ni Balozi wa serekali ya Mbinguni

Kwa Watakatifu, watu wa Mungu aliye Baba yetu, na Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo. namshukuru Mungu wetu katika Yesu Kristo kwa ajili yenu niyi wote mtakao soma majibu ya swali la Ndugu yetu kebhayo,


Kwa maana Mungu tumwabuduye kwa roho na kweli katika Injili ya Mwana wake Yesu kristo, naye ni shahidi wetu kwa yale tu yanenayo au tunayoyatenda Amestahili yeye kutukuzwa kupitia maswali

Bwana wetu na Mungu wetu kwa wale wanaomwamini, kuwa yeye ndiye aliyeviumba vitu vyote, na kwa sababu ya mapenzi yake vilikuwako, navyo viliumbwa. ujumbe huu unajibiwa katika Jina lile lipitalo majina yote, Jina la Yesu Kristo, Mwana wa Mungu aliye hai, Bwana na Mwokozi wetu. Kwa kuwa majibu ni mengi ninaomba niyafupishe ila ikihitajika kwa urefu zaidi ya hapa nalo linawezekana, pia nitafanya hivyo

UTANGULIZI

• Siri ya Mungu ipo kwa wao wamchao tu, zaburi 25:14

• Kilichozwaliwa kwa mwili ni mwali na kilicho zaliwa kwa Roho ni Roho

• Heri kuchagua jina jema kuliko mali nyingi; Na neema kuliko fedha na dhahabu Mithali 22:1

Aketiye mahali pa siri pake Aliye juu Atakaa katika uvuli wake Mwenyenzi ……………….Kwa siku NYINGI nitamshibisha, nami nitamwonyesha wokovu wangu” (Zaburi 91:16)“Ili wafarijiwe mioyo yao, wakiunganishwa katika upendo, wakapate utajiri wote wa kufahamu kwa hakika, wapate kujua kabisa siri ya Mungu, yaani, Kristo’ (Wakolosai 2:2).


Basi tu wajumbe kwa ajili ya Kristo” (2Wakorintho 5:20)

Kuwa mjumbe kwa ajili ya Kristo maana yake nini? Tunatakiwa tuwe wajumbe kwa ajili ya Kristo juu ya nini? Na kwa namna gani? Na kwa nani? Na kwa wakati gani? Neno la Kiingereza lililotafsiriwa kuwa mjumbe ni ‘Ambassador” Na neno zuri linalotoa picha nzuri ya maana ya ‘Ambassador’ ni neno Balozi. Balozi ni mjumbe na mjumbe ni balozi

Neno balozi na neno mjumbe lina maana sawa lakini kwa jinsi tunavyoyatumia maneno haya, utafikiria neno balozi lina uzito zaidi kuliko neno mjumbe.

Kwa hiyo tunaweza kusema: “ Basi tu mabalozi (wajumbe) kwa ajili ya Kristo” Katika nchi ya Tanzania tuna mabalozi wa nyumba kumikumi, ambao pia wanajulikana kuwa ni wajumbe wa nyumba kumikumi. Pia tuna mabalozi walioko nchi za nje waliotumwa kuiwakilisha nchi hii katika maswala na majukumu mbalimbali.

Sasa na tuliangalie katika ngazi ya kitaifa. Balozi ni mjumbe au mwakilishi wa nchi moja katika nchi nyingine. Kwa mfano: Balozi wa Tanzania nchini Kenya; kwanza ni raia wa Tanzania anayefahamu vizuri msimamo wa nchi hii katika maswala mbalimbali. Yuko Kenya kwa ajili ya Serikali ya Tanzania na raia wa Tanzania.

Yeye ndiye msemaji mkuu wa Serikali ya Tanzania nchini Kenya. Serikali ya Tanzania inapopeleka ujumbe kwa serikali ya Kenya, inapitia kwa balozi wake aliyeko Kenya.

Balozi huyo ni picha kamili ya Watanzania kwa watu wa Kenya, katika maneno yake na mwenendo wake. Yeye ni mlinzi wa hadhi ya Tanzania nchini Kenya. Na makazi yake ni nchini Kenya.

Balozi ni mjumbe aliyetumwa na mtu mwingine. Balozi wa Tanzania katika umoja wa Mataifa, ametumwa na nchi yetu, awe msemaji na mtetezi wa mawazo ya Tanzania katika maswala mbalimbali ya kimataifa. Balozi hasemi mawazo yake mwenyewe. Balozi anasema tu kile alichotumwa kusema na anafanya kile tu ambacho ametumwa kufanya.

Tunasisitiza hivi, BALOZI HASEMI MAWAZO YAKE MWENYEWE: BALOZI ANASEMA TU KILE ALICHOTUMWA KUSEMA, NA ANAFANYA KILE TU AMBACHO AMETUMWA KUFANYA.Na kitu cha kwanza anachofanya anapofika katika nchi aliyotumwa ni kutoa vitambulisho vilivyo na muhuri na sahihi ya kiongozi wa nchi anayotoka.

Biblia inatuambia kuwa sisi ni mabalozi kwa ajili ya Kristo hapa duniani; sisi ni wajumbe tuliotumwa kwa ajili ya Kristo hapa duniani. Ndiyo maana Paulo alisema kuishi kwake ni Kristo. Wewe ni mjumbe wa Kristo na kwa ajili ya Kristo hapa duniani. Ikiwa wewe ni Mjumbe, basi wewe ni balozi wa Kristo na kwa ajili ya Kristo.

Kumbuka kuwa balozi hasemi mawazo yake mwenyewe. Wewe ni balozi wa Kristo hapa duniani kwa hiyo kutokana na wadhifa huo uliopewa unatakiwa usiseme mawazo yako, wala kufanya mambo yako hapa duniani; bali USEME MAWAZO YA KRISTO NA MANENO YAKE; NA UFANYE YAKE TU ALIYOKUTUMA KUFANYA.

Lakini ni wazi kwamba huwezi kusema mawazo na maneno ya Kristo wakati huyafahamu. Na ikiwa hapa duniani wewe ni balozi basi, inamaanisha hapa duniani si kwako. Na ikiwa hapa duniani si kwako, na wala wewe si mwenyeji wa hapa duniani; basi unatokea wapi na uenyeji (uraia) wako ni wa wapi?

Wewe ni mwenyeji wa wapi? Hili swali ni muhimu sana ambalo ni budi ufahamu jibu lake katika roho yako. Bila kufahamu ulikotoka utaifanye kazi ya ubalozi au ya kuwa mjumbe wa Kristo. Balozi (Mjumbe) yeyote anajua alikotoka; anafahamu uraia wake ni wa wapi. Je wewe unafahamu kuwa wewe ni balozi wa nchi gani ukiwa hapa duniani?

ninakazia swali hili kwa sababu ujumbe utakokuwa unatoa; au mahubiri unayofanya mbele za watu; na matendo yako yanategemea sasa mahali gani umetoka kiroho na kimazingira.

Kuna wengine ni mabalozi wa miili yao wenywe. Wanahubiri kwa sababu ya mwili ili wapate mishahara yao na kuvaa. Wao wanaona kuwa kuhubiri ni kama kazi nyingine ya kuajiriwa.

Lakini la kushangaza ni kwamba wote wanasema ni mabalozi wa Kristo, wajumbe wa neno la Injili. Na hii si kweli. Muda umefika ambapo Roho wa Mungu amekududia kuliweka wazi hili. Mabalozi wa Kristo wawe wazi; mabalozi wa madhehebu wawe wazi, na mabalozi wa miili yao wawe wazi.

Muda umefika wa kufichuliwa watu wote wanaojiita mabalozi wa Kristo, wameokoka, na ni wakristo?, watumishi wa Kanisa kumbe ni mbwa mwitu wakali wanaowaendea watu wakiwa wamevaa mavazi ya Kondoo (Mathayo 7:15).

Muda umefika ambao watu wote wanokaa karibu na wewe, vitu vyote vinavyokuzunguka, mahali unapopita, watu wote hao wanaokuzunguka wajue, kwamba wanajua KUWA WEWE NI BALOZI WA KRISTO MJUMBE KWA AJILI YA KRISTO!Kweli

UTASEMA MAWAZO NA MANENO YA KRISTO. NA UTAFANYA MATENDO YA KRISTO KWA AJILI YA KRISTO MAHALI POPOTE ULIPO NA UTAKAPOKUWA DUNIANI:

Kuishi kwako hapa duniani ni Kristo na kufa kwako ni faida! Mtume Paulo alipoandika kuwa “Basi tu wajumbe (Mabalozi) kwa ajili ya Kristo,” alikuwa anamhusisha kila mtu ambaye amefanyika kuwa kiumbe kipya ndani ya Kristo. Ikiwa wewe ni kiumbe kipya ndani ya Kristo, basi wewe ni mjumbe(balozi) kwa ajili ya Kristo.

Ikiwa basi wote waliozaliwa mara ya pili, walio viumbe vipya ndani ya Kristo (waliookoka) wanatakiwa kuwa mabalozi wa Kristo; mbona basi ubalozi wao hauonekani ukifanya kazi? Ubalozi hauonekani katika maisha yako, kwa sababu hujafuatilia katika Biblia kujua neno linasemaje juu ya hili.

Ni Duwa yangu na maombi kila atakayepata ujumbe huu akubali kwanzia leo yeye awe Balozi wa serekali ya mbinguni Baada ya kujitabuwa lati tingefahamu uzito wa wadhifa huu wa kuwa mjumbe wa Kristo hapa duniani, hali ya mambo isingekuwa kama ilivyo hivi sasa ya kukata tamaa – iliyojaa katika mioyo ya yetu.na kujiweka mbali na Mungu kiasi hicho

Laiti basi wewe ungejua uzito wa wadhifa huu wa kuwa mjumbe wa Kristo mahali ulipo ikiwa in nyumbani, kazini, safarini, kanisani, sokoni, hali ya mambo isingekuwa kama unavyoiona sasa. Nchi yetu inaharibika kwakuwa watu wameyaacha majukumu yao wakatamani ya wengine wasiyoyaweza je tunakwenda wapi,Hoko?

Ubalozi uzalendo uraia wa mbinguni

Mtu yeyote Yule aliyemwamini kristo kama Bwana na muokozi wa maisha yake yeye ni raia wa mbinguni. Na mzalendo wa Mbinguni kwa mjibu wa maandiko matakatifu,

“Basi tangu sasa ninyi si wageni wala Wapitaji, bali ninyi ni wenyeji pamoja na watakatifu, watu wa nyumbani mwake Mungu” (Waefeso 2:19).

Yesu Kristo alipokuwa akituombea alisema:

“Mimi nimewapa neno lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa WAO SI WA ULIMWENGU, kama mimi nisivyo wa ulimwengu. Mimi siombi kwamba uwatoe katika ulimwengu; bali uwalinde na yule muovu. Wao SI WA ULIMWENGU KAMA MIMI NISIVYO WA ULIMWENGU. Uwatakase kwa ile kweli; neno lako ndiyo kweli. Kama vile ulivyonituma mimi ulimwenguni, nami vivyo hivyo NILIWATUMA HAO ULIMWENGUNI (Yohana 17:4-18)

Weka jambo ili katika moyo wako. Watu wa Kristo si wa ulimwengu huu, bali ni wenyeji wa mbinguni. Watu wa Kristo wako hapa ulimwenguni kwa sababu Kristo amewatuma kufanya kazi muhimu. Kumbuka upo hapa duniani kwa kuwa kuna KAZI ambayo KRISTO amekupa uifanye kabla ya kurudi nyumbani kwetu MBINGINU.kama huitambui leo Roho mtakatifu kupitia Balozi wa Serekali ya Mbinguni ameamua utambuwe sasa, ila kwa msaada zaidi piga simu yangu ya mkono au ya meza Ext;1961/ 0756 809 209, kwa maswali zaidi na msaada,niko tayari usiku na mchana 24 kwa siku 7 za juma hakuna aliyechelewa kuaza kazi ya ubalozi anza sasa kama jana hukufanya

Balozi wa serekali ya mbinguni
(Samson)

Blog Archive

Followers