MAUTI YA PILI:
kuingia uzimani”. Ina maana AMEOKOKA kutoka mautini (jehanum). Jehanum ndio mauti ya pili. (Ufu 20:14-15)
Watu wengi wnadhani kutokunywa pombe, kutovuta sigara, kutofanya zinaa, kutoiba, n.k ndio kuokoka na hukumu ya Mungu. Wengi wanadhani, kwenda kanisani, kuimba kwaya, kuhubiri, kuwa mzee wa kanisa au kiongozi wa kikundi, n.k ndio kuokoka na hukumu ya Mungu. Kuna wokovu halisi na matendo au maisha ya wokovu. Watu wengi wanaishi maisha ya wokovu, lakini kwa uhalisi, hawajaokoka bado, hawajampa Yesu mioyo yao na maisha yao yote
Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yesu na kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Yesu alisema hivi kwa Mungu Baba,
“ Na uzima wa milele ndio huu, wakujue wewe, Mungu wa pekee wa kweli, na Yesu Kristo uliyemtuma” (Yoh 17:3). Hatuokoki na hukumu ya Mungu kwa kushika sheria, bali kwa kuipokea neema ya wokovu kwa kumwamini Yesu Kristo. “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani, ambayo hiyo haitokani na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu (zawadi). Wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu (Efe 2;8-9)
Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yesu kristo au kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake.
“hali tukijua ya kuwa, mwanadamu hahesabiwi haki kwa matendo ya sheria, bali kwa imani ya Kristo Yesu; Sisi tulimwamini Kristo Yesu ili tuhesabiwe haki kwa imani ya Kristo, wala si kwa matendo ya sheria.
Maana kwa matendo ya sheria, hakuna mwenye mwili atakayehesabiwa haki” (Gal 2:16; Gal 3:7-14) Kuna wokovu halisi na matendo au maisha ya wokovu. Watu wengi wanaishi maisha ya wokovu, lakini kwa uhalisi, hawajaokoka bado, hawajampa Yesu mioyo yao na maisha yao yote,
Kuna habari ya mtu aliyeishi maisha kama hayo hapa duniani Biblia inasema aliye shika sheria, aliyedumu katika sala, aliyefunga na kuomba, aliyetoa sadaka nyingi kwa watu maskini, n.k lakini alikuwa hajafanya hatua muhimu kuliko zote ya kumwamini na kumpokea Yesu Kristo,yaani (kuokoka) ilia pate uzima wa milele na kuokolewa. Mtu huyo jina lake Aliitwa Kornelio. Matendo ya Mitume 10:1-8, 23-48.
Mungu akamhurumia kuwa, japo amekuwa mwaminifu kushika sheria na kuishi maisha ya kumcha Mungu, lakini kwasababu hajamjua Yesu bado, asingeokoka na hukumu ya milele, kwa maana hana uzima wa milele. Mungu akamtuma malaika kumwambia Kornelio, amfuate Petro, naye atamweleza cha kufanya. Ndipo Petro akaja na akamweleza habari za Yesu, Kornelio na familia yake, wote wakamwamini na kumpokea Yesu. Wakapata wokovu halisi (uzima wa milele). Baada ya hapo, maisha ya wokovu ndipo yanakuwa na maana.
Kushika sheria za dini na kuishi maisha ya wokovu, siko kunakompendeza Mungu, kama huyo mtu hajampokea Yesu na kumwamini kama Bwana na mwokozi wa maisha yake. Inawezekana nawe umekuwa mcha Mungu kama Kornelio, lakini hujampokea Yesu moyoni na kumkiri. Mpokee sasa!
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
Blog Archive
-
▼
2012
(30)
-
▼
May
(13)
-
▼
May 04
(11)
- Nini maana ya kuokoka?(wokovu)
- Torati inasema nini juu ya Kuokoka?(Uwokovu)
- KWA NINI UOKOKE?
- Kupona kwako na Jehanamu ni Kuokoka,
- Kwanini magonjwa ya kuonee kiasi hicho? ikiwa kuna...
- Je unastahili kuwa Tajiri Ndiyo hunasababu ya kut...
- Unafahamu kuwa kuna mauti ya pili, unajua namna ya...
- Ni rahisi kabisa Kuokoka kama uko Tayari,
- UMEFANYA MAAMUZI MAZURI SANA
- kwa ushahuri na maombezi kutoka kwa balozi piga simu,
- UNGANA NA MAMIA YA WATU WALIYOKUTANA NA MAJIBU Y...
-
▼
May 04
(11)
-
▼
May
(13)