. TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA UMASKINI
Angalia, utakapokuwa umekula na kushiba, na kujenga nyumba nzuri na kukaa ndani yake. Na fedha yako na dhahabu yako itakapoongezeka. Na kila kitu ulichonacho kitakapoongezeka; Basi hapo moyo wako usiinuke ukamsahau Bwana Mungu wako,
aliyekutoa katika nchi ya Misri,(utumwa) katika nyumba ya utumwa … hapo usiseme moyoni mwako, nguvu zangu na uwezo wa mkono wangu, ndio ulionipatia utajiri huo; Bali utamkumbuka Bwana Mungu wako, maana ndiye akupaye nguvu za kupata utajiri, ili alifanye imara agano lake … (Kumb 8:12-18)
Lakini hawatakuwepo masikini kwenu, kwakuwa Bwana atakubariki kweli, katika nchi akupayo Bwana Mungu wako, uimiliki, iwe urithi wako. (Kumb 15:4)ukisha kombolewa ninaamini Maisha yako yanaanza kubadilika ile siku ya kwanza ulipokubali kumkiri kristo Yesu,
Naye Abrahamu alikuwa tajiri sana kwa mifugo, kwa fedha na kwa dhahabu (Mwa 13:2) naomba ufahamu utajiri unaoongelewa hatadondoka kama maemba juu ya mti, bali bidii ya kumtumikia Mungu na ya kujishuguliza na kazi halali za mikono yako, ili baraka zipitie mikononi mwako, ukweli swala hili limewasumbuwa watu wengu sana, na si washirika pekeyao, bali hata kwa baadhi ya watumishi, wachungaji,wainjilisti,mitume na manabii, kisingizio kwamba wanakulia madhabauni, wengi Tunatafsiri tunavyo taka kwa maslahi yetu sisi wenyewe bali si kwaajili ya vile bwana anavyo taka, Mungu ni wautaratibu, nitaifafanuwa vizuri sana kitabu kijacho maana hayo nayo nimafundisho yake, niendelee kwanza na hili la shule ya awali, Linaloanza na Uwokovu nini na fida zake,
Maana mmejua Neema ya Bwana wetu, Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa masikini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajri. Ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. (2Kor 8:9) … mkitajirishwa katika vitu vyote, mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. (2Kor 9:11) …
Na Mungu wangu atawajazeni kila mnachokihitaji kwa kadiri ya utajiri wake, katika utukufu, ndani ya Kristo Yesu. (Fil 4:19) … Maana yeye yule ni Bwana wa yote, mwenye utajiri kwa wote wamuitao; kwa kuwa, kila atakayeliitia jina la Bwana ataokoka. (Rum 10:12)
Leteni zaka kamili ghalani, ili kiwemo chakula katika nyumba yangu, mkanijaribu kwa njia hiyo, asema Bwana wa majeshi, mjue kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni, na kuwamwagieni baraka, hata isiwepo nafasi ya kutosha, au la.
Nami kwa ajili yenu nitamkemea yeye alaye, wala hataharibu mazao ya ardhi yenu; wala mzabibu hautapukutisha matunda yake kabla ya wakati wake katika mashamba, asema Bwana wa majeshi. Na mataifa yote watawaiteni heri; maana mtakuwa nchi ya kupendeza sana, asema Bwana wa majeshi. (Malaki 3:10 – 12)
Thawabu ya unyenyekevu, ambao ni kumcha Bwana, ni utajiri na heshima, nayo ni uzima.
(Mith 22:4)
Itakuwa utakaposikia sauti ya Bwana, Mungu wako, kwa bidii, kutunza kuyafanya maagizo yake yote nikuagizayo leo, ndipo Bwana, Mungu wako, atakapokutukuza juu ya mataifa yote ya dunia; na baraka hizo zote zitakujilia na kukupata usikiapo sauti ya Bwana, Mungu wako. Utabarikiwa mjini, utabarikiwa na mashambani, utabarikiwa na uzao wa tumbo lako, na uzao wa nchi yako, na uzao wa wanyama wako wa mifugo. Maongeo ya Ngombe wako, na wadogo wa kondoo zako: utabarikiwa kapu lako, na chombo chako cha kukandia unga.
Utabarikiwa uingiapo, utabarikiwa na utokapo Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yako watakutokea kwa njia moja; lakini watakimbia mbele kwa njia saba. Bwana ataiamuru baraka ije juu yako katika ghala zako, na mambo yote utakayotia mkono wako; naye atakubariki katika nchi akupayo Bwana wako Mungu wako.
Bwana atakuweka uwe taifa takatifu kwake, kama alivyokuapia; utakapoishika maagizo ya Bwana Mungu wako na kutembea katika njia zako na mataifa yote ya dunia watakuona umeitwa kwa jina la Bwana, nao watakuwa na hofu kwako. Bwana atakufanya uwe na wingi wa uheri, katika uzao wa tumbo lako, na uzao wa wanyama wako, na uzao wa nchi yako, kama Bwana alivyowaapia baba zako kwamba atakupa.
Atakufunulia Bwana hazina yake nzuri, nayo ni Mbingu , kwa kutoa mvua ya nchi yako kwa wakati wake, na kwa kubariki kazi yote ya mkono wako; nawe utakopesha mataifa mengi wala hutokopa wewe. Bwana atakufanya uwe kichwa wala si mkia; nawe utakuwa juu tu, wala huwi chini;
utakapo yasikiza maagizo ya Bwana, Mungu wako, nikuagizayo hivi leo,kuyaangalia na kuyafanya; msipokengeuka katika maneno niwaamuruo leo kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia. (Kumb 28:1-14)
Damu ya msalaba iliyoondoa dhambi, ndiyo iliyoondoa umasikini pia, Yatupasa kuuona umasikini kama tunavyoiona dhambi. Umaskini ni matokeo ya anguko la mwanadamu katika dhambi. Tukiisha okolewa katika dhambi, yatupasa kuokolewa katika umasikini pia.
Utajiri ni matunda ya msalaba kama ilivyo wokovu. Yatupasa kuchukia umasikini kama tunavyochukia dhambi. Kifo cha Yesu, kitakuwa hakina maana kamili, kama tutaokolewa katika dhambi, halafu tubaki maskini katika mwili pia, wakati Yesu aliyefia dhambi, ndiye aliyefia umasikini pia. Msalaba ulifanya vyote, yaaani uliondoa dhambi na umasikini pia.
Biblia inasema; “Maana mmejua Neema ya Bwana wetu, Yesu Kristo, jinsi alivyokuwa masikini kwa ajili yenu, ingawa alikuwa tajiri. Ili kwamba ninyi mpate kuwa matajiri kwa umaskini wake. (2Kor 8:9) … mkitajirishwa katika vitu vyote, mpate kuwa na ukarimu wote, umpatiao Mungu shukrani kwa kazi yetu. (2Kor 9:11)
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
Blog Archive
-
▼
2012
(30)
-
▼
May
(13)
-
▼
May 04
(11)
- Nini maana ya kuokoka?(wokovu)
- Torati inasema nini juu ya Kuokoka?(Uwokovu)
- KWA NINI UOKOKE?
- Kupona kwako na Jehanamu ni Kuokoka,
- Kwanini magonjwa ya kuonee kiasi hicho? ikiwa kuna...
- Je unastahili kuwa Tajiri Ndiyo hunasababu ya kut...
- Unafahamu kuwa kuna mauti ya pili, unajua namna ya...
- Ni rahisi kabisa Kuokoka kama uko Tayari,
- UMEFANYA MAAMUZI MAZURI SANA
- kwa ushahuri na maombezi kutoka kwa balozi piga simu,
- UNGANA NA MAMIA YA WATU WALIYOKUTANA NA MAJIBU Y...
-
▼
May 04
(11)
-
▼
May
(13)