3. TORATI INASEMA NINI JUU YA UWOKOVU, Pia tutambuwe kuwa tunavyosema Torati maana Sheria,
“Fahamuni basi, yakuwa wale walio na imani, hao ndio wana wa Ibrahim. Na andiko, kwa vile lilivyoona tangu zamani kwamba Mungu atawahesabia haki mataifa kwa imani, lilimhubiri Ibrahim habari njema zamani, kusema, katika wewe mataifa watabarikiwa. Basi hao walio na imani hubarikiwa pamoja na Ibrahim aliyekuwa mwenye imani. Kwa maana wale wote walio wa matendo ya sheria, wako chini ya laana maana imeandikwa amelaniwa kila mtu asiyedumu katika yote yaliyoandikwa katika kitabu cha Torati, ayafanye.
Ni dhahiri ya kwamba hakuna mtu ahesabiwaye haki mbele za Mungu katika sheria; kwa sababu mwenye haki ataishi kwa imani. Na torati haikuja kwa imani, bali ,ayatendaye hayo, ataishi katika hayo. Kristo alitukomboa katika laana ya Torati, kwa kuwa alifanywa laana kwa ajili yetu;
maana imeandikwa , amelaaniwa kila mtu aangikwae juu ya msalaba; ili kwamba baraka ya Ibrahim iwafikirie mataifa katika Yesu Kristo, tupate kupokea ahadi ya roho kwa njia ya imani”. (Gal 3:7-14, 23-29).
“Kwa maana Kristo ni mwisho wa sheria, ili kila aaminiye ahesabiwe haki. (Rum 10:4) Kwa kule kusema, Agano jipya, amelifanya lile la kwanza kuwa kuukuu. Lakini kitu kianzacho kuwa kikuukuu na kuchakaa ki karibu na kutoweka”. (Ebr 8:13)
Basi twaona ya kuwa mwanadamu huhesabiwa haki kwa imani pasipo matendo ya sheria tena,…
Basi, mtu asiwahukumu ninyi katika vyakula au vinywaji, au kwa sababu ya sikukuu au mwandamo wa mwezi, au Sabato; ( Rum 3:28; Kol 2:16)
Pia Mdo 15:1-10-29; Gal 2:16; Rum 8:3; Rum 7:12,14-16; Rum 8:1-4; Yer 31:31-34 mimi ninaandika muongozo, mengi
maandiko Matakatifu yanathibitisha, Yote ila kama una swali na ungependa kuuliza ninakushahuri ujiulize au uliza kwakutaka kumwelewa kristo zaidi na kazi zake,
na siyo kupinga au kubishana na wengine, angalizo kitabu hiki hakitowi nafasi kwaajili ya malumbano au mabishano,ya Dini au mafundisho ya chuo chochote bali ni kwaajili ya kuwasaidia wale wote wenye nia ya kutaka kuwa wanafunzi wazuri wa Yesu kristo au walimu wazuri, kama unapenda au unataka kubishania Maneno matakatifu, basi kitabu hiki hakiwezi kukusaidia, kabisa
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
Blog Archive
-
▼
2012
(30)
-
▼
May
(13)
-
▼
May 04
(11)
- Nini maana ya kuokoka?(wokovu)
- Torati inasema nini juu ya Kuokoka?(Uwokovu)
- KWA NINI UOKOKE?
- Kupona kwako na Jehanamu ni Kuokoka,
- Kwanini magonjwa ya kuonee kiasi hicho? ikiwa kuna...
- Je unastahili kuwa Tajiri Ndiyo hunasababu ya kut...
- Unafahamu kuwa kuna mauti ya pili, unajua namna ya...
- Ni rahisi kabisa Kuokoka kama uko Tayari,
- UMEFANYA MAAMUZI MAZURI SANA
- kwa ushahuri na maombezi kutoka kwa balozi piga simu,
- UNGANA NA MAMIA YA WATU WALIYOKUTANA NA MAJIBU Y...
-
▼
May 04
(11)
-
▼
May
(13)