Ni rahisi kabisa Kuokoka kama uko Tayari,

Namna ya kupata (KUOKOKA)


HATUA YA KWANZA; Tambua kuwa wewe ni mwenyedhambi na Utubu,Makosa yako hatakuto kumwamini Mungu yaani kutokumkiri ni Dhambi ya kwanza, anza na hiyo tumbu kabisa

DHAMBI ZAKO, KWA KUMAANISHA KUZIACHA.KABISA

“Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele” (Rum 3:23). “Tubuni, mkabatizwe kila mmoja kwa jina la Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Mtakatifu.” (Mdo 2:38)

HATUA YA PILI; MWANINI NA KUMPOKEA YESU MOYONI MWAKO. TOA

MAISHA YAKO KWAKE, AWE BWANA NA MWOKOZI WAKO.

Yule mlinzi wa gereza akamwambia Paulo na Sila “Bwana zangu, yanipasa nifanye nini nipate kuokoka? Wakamwambia, mwamini Bwana Yesu, nawe utaokoka pamoja na nyumba yako” (Mdo 16:30-31).

“Kwasababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, UTAOKOKA. Kwa maana moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri, hata KUPATA WOKOVU. (Rum 10:9-10)

HATUA YA TATU: ISHI MAISHA YA WOKOVU, MAISHA SAFI YA KUMPENDEZA MUNGU NA KUZISHIKA AMRI ZAKE (NENO LAKE)

“nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi… Na katika hili twajua ya kuwa tumemjua yeye (Mungu) ikiwa tunashika amri zake. Lakini Yeye asema neno lake, katika huyo upendo wa Mungu umekamilika kweli kweli, katika hili twajua ya kuwa tumo ndani yake….” (1Yoh 2:1-6). Kwahiyo sasa, kwakuwa awali hukufahamu na kutambuwa kilichokupasa kufanya anza sasa maisha mapya ndani ya Yesu. Ukifanya hivyo maisha yako hayatabaki kama yalivyo hivi sasa,

“…mtu akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya, ya kale yamepita, tazama! Yamekuwa mapya”. (2Kor 5:17) Jitenge na uovu wote na Usiishi katika maisha ya dhambi tena.

Josh 1:8 Na Rum 6:1-23.

Kitabu hiki cha torati kisiondoke kinywani mwako, bali yatafakari maneno yake mchana na usiku, upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yaliyoandikwa humo; maana ndipo utakapoifanikisha njia yako, kisha ndipo utakapositawi sana.

Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.



Blog Archive

Followers