TUMEOKOLEWA KUTOKA KATIKA MAGONJWA.
Nanyi mtamtumikia Bwana Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako na maji yako. Nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. (Kut 23:25) … Na Bwana atakuondolea ugonjwa wote, wala hatatia juu yako maradhi yeyote, mabaya uyajuayo …” (Kumb 7:15)
Hata kulipokuwa jioni, wakamletea wengi wenye pepo, akawatoa pepo kwa jina lake, akawaponya wote waliokuwa hawawezi (wagonjwa). Ili litimie lile neno lililonenwa na Nabii Isaya akisema; “Mwenyewe aliutwaa udhaifu wetu na kuyachukuwa magonjwa yetu.” (Math 8:16-17) “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote, na udhaifu wa kila aina”. (Math 9:35) “ … Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu; wawatoe na kupoza, magonjwa yote na udhaifu wa kila aina (Math 10:1)
Yeye mwenyewe alizichukuwa dhambi zetu katika mwili wake juu ya mti, tukiwa wafu kwa mambo ya dhambi, tuwe hai kwa mambo ya haki; Na kwa kupigwa kwake mliponywa (1Pet 2:24) “Hakika ameyachukuwa masikitiko yetu, amejitwika huzuni zetu …. Bali alijeruliwa kwa makosa yetu, alichubuliwa kwa maovu yetu. Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake; Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona. (Isa 53:4 -5)
sipingi kwa mtu aliyeokoka kuuguwa, ilakama mwana wa Mungu Fahamu kuwa hustahili kukaa na magonjwa kwakuwa tayari msalaba ulichukuwa madhaifuna magonywa yote,, na ukiona kuwa imani yako nindogo au hujamwamini kristo kuwa bwana na mwokozi wa maisha yako
Ushahuri wangu kata shahuri sasa, ndipo udai uponyaji wa msalabani, vinginevyo kama hutaki kupa yesu krsto maisha ukiuguwa nenda hospitali bibilia haimzuwii mtu kwenda hosipitali, bali inadhihirisha uponyaji wa bure unaotokana na Msalaba,
Damu ya Msalaba iliyoondoa dhambi, ndiyo iliyoondoa magonywa pia. Yatupasa kuyaona magonjwa kama tunavyoiona dhambi. Hatupaswi kuyaona kuwa ni sehemu ya maisha yetu.
Magonjwa ni matokeo ya anguko la mwanadamu katika dhambi. Tukiisha okolewa toka dhambini, yatupasa kuokolewa kutoka katika magonjwa pia. Afya njema ni matunda ya msalaba kama ilivyo wokovu.
Tunatakiwa kuchukia magonjwa kama tunavyochukia dhambi, kwasababu yote haya, ni kazi za shetani. Yatupasa kuzikataa na kuzivunja katika maisha yetu. Kifo cha Yesu, kitakuwa hakina maana kamili, kama tutaokolewa katika dhambi, halafu tubaki katika magonjwa pia,
wakati Yesu aliifia dhambi, ndiye aliyefia magonjwa pia. Msalaba ulifanya vyote, uliondoa dhambi na magonjwa pia. “Mwenyewe aliutwa udhaifu wetu na kuyachukuwa magonjwa yetu.” (Math 8:16-17)
Ndugu Mtazamaji/ MSOMAJI; Bila shaka unampenda Mungu Sana tunaamini hivyo Kwa vile ulivyoweza kufika mahali hapa tulipo kupitia Mtandao huu, lipo kusudi la Mungu kutaka kukusaidia jambo Fulani ikiwa uko tayari katika yote jiepushe na mafundisho yasiyokuwa ya ki-Mungu Mathayo 16:6-12) piga simu kwa masaada zaidi huduma hii ni bure 0757328311
Blog Archive
-
▼
2012
(30)
-
▼
May
(13)
-
▼
May 04
(11)
- Nini maana ya kuokoka?(wokovu)
- Torati inasema nini juu ya Kuokoka?(Uwokovu)
- KWA NINI UOKOKE?
- Kupona kwako na Jehanamu ni Kuokoka,
- Kwanini magonjwa ya kuonee kiasi hicho? ikiwa kuna...
- Je unastahili kuwa Tajiri Ndiyo hunasababu ya kut...
- Unafahamu kuwa kuna mauti ya pili, unajua namna ya...
- Ni rahisi kabisa Kuokoka kama uko Tayari,
- UMEFANYA MAAMUZI MAZURI SANA
- kwa ushahuri na maombezi kutoka kwa balozi piga simu,
- UNGANA NA MAMIA YA WATU WALIYOKUTANA NA MAJIBU Y...
-
▼
May 04
(11)
-
▼
May
(13)