TUNAWEZAJE KUSEMA TUNAMPENDA MUNGU,

KUZISHIKA AMRI ZA MUNGU NDIKO KUMPENDA MUNGU


Kumbukumbu la Torati 6:5 Nawe, mpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa nguvu zako zote na Pia ile Mathayo 22:37 inasema Akamwambia, Mpende Bwana Mungu wako kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote”. Hivyo basi kwa kutumia hiyo mistari miwili tunaona kwamba mtu anatakiwa kumpenda Bwana Mungu wake kwa;


Moyo wake wote, Roho yake yote, Nguvu zake zote, Na akili zake zote.


Lakini pia ukisoma kile kitabu cha 1 Yohana 5:3 Biblia inasema “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba, tuzishike amri zake, wala amri zake si nzito”. Hivyo basi kumpenda Mungu ni kuzishika amri zake. Sasa kuzishika amri za Mungu ni suala linalohitaji Moyo wako, roho yako, nguvu zako na akili zako vyote kwa pamoja vifanye kazi ya kumpenda Mungu kwa maana ya kuzishika amri zake.


Kumpenda Bwana kwa moyo wako.


Kumpenda Bwana kwa moyo wako ni kwa kuutafakarisha moyo wako amri za Bwana kwa maana ya maagizo yake unayotakiwa kuyashika. Hii ni pamoja na kutumia muda wako siku zote kuliweka neno la kristo kwa wingi ndani yako kwa kulitafakari. Unapolitafakari neno la Bwana ndipo pia unapopata mawazo na njia za Mungu za kukufanikisha kimaisha. Zaburi 27:4.


Kumpenda Bwana kwa roho yako.


Hapa unatakiwa kuitafakarisha roho yako neno la Bwana ambalo linazungumzia wakati ujao (future yako) isibishe roho yako ahadi za Mungu ili imani yako iongezeke na uanze kuona mambo ya wakati ujao kana kwamba yapo halisi kwa wakati wa sasa. Hili litakusaidia kuishi kwa Imani, maana siku zote utakuwa unafanya yale yanayompendeza Mungu.


Kumpenda Bwana kwa nguvu zako zote.


Nguvu ni uwezo alionao mtu katika kufanya kazi fulani. Sasa tumia nguvu zako zote za kimwili za kiufahamu, za kifedha nk katika kutekeleza yale yote ambayo neno la Mungu linakuagiza kila siku unapolitafakari kumbuka nimekuambia katika kulitafakari neno la Bwana utapata mawazo ya Bwana juu yako na ndani ya hayo mawazo kuna mipango na mikakati ya kuitekeleza.


Kumpenda Bwana kwa akili zako zote.


Vile vile akili ni uwezo wa kiufahamu alionao mtu katika kufanya mambo. Hivyo basi wakati unatumia nguvu kutekeleza maagizo ya Bwana basi hakikisha unatekeleza kwa kutumia akili ili ufanye kitu sahihi, kwa wakati sahihi na kwa usahii

Followers