kwa nini watu wanateswa na Maagano?


MATESO YA AGANO







Kama kunamateso yanayoweza kumtesa mtu kwa muda mrefu ni Mateso ya Agano maana kama agano halikuharibiwa maanayake mateso hayawezi kuisha maana Agano ni kifungo cha kiroho, mbaya yaidi shahidi wa agano akiwa damu, ni shida lazima ifutwe kwa damu kwa nini ninashawishika kukuambia ukweli ili ukubali agano la kale lifutike uingie agano jipya la Damu ya yesu, kwa kumkiri awe bwana na Muokozi wa maisha yako,

 

 Yohana 1:12 Unaitwa mwana wa Mungu kwasababu ya Damu ya Yesu Kristo. Mungu ni Mungu wa Agano ndio maana anaitwa Mungu ashikaye maagano yaani ukiingia naye mikataba huwa haivunjiki na kila alipokutana na mtu kwenye agano la kale Mungu anapenda agano kuliko maneno maneno,
imeandikwa Mwanzo 6: 18 “Lakini nitafanya agano langu nawe kuwa thabiti; nawe utaingia katika safina, wewe, na wanao, na mkeo, na wake za wanao, pamoja nawe.”

imeandikwa Mwanzo 15: 18 “Siku ile Bwana akafanya agano na Abramu, akasema, Uzao wako nimewapa nchi hii, kutoka mto wa Misri mpaka huo mto mkubwa, mto Frati”

Mungu alifanya naye agano na ibrahimu kwa kumpa nchi ya watu wakanaani, wayebusi mali na mengineyo mengi wewe agano lako na Mungu ni lipi shida ya watu wengi wanapokwenda mbele za Mungu wanaenda na haja binafsi.na kelele nyingi na ushawishi wa machozi mengi,kujinyima kula chakula, wanakula baadaye,

imeandikwa Ezekieli 16:20 “zaburi 106:37 Pamoja na hayo uliwatwaa wana wako na binti zako, ulionizalia, ukawatoa sadaka kwao ili waliwe. Je! Mambo yako ya kikahaba ni kitu kidogo tu”

Kuna wakati huna watoto, nyumba, huna chochote lakini Mungu si wakati wakuvitafuta hivyo tafuta agano na Mungu maana Mungu akikuangalia anakuona unamiliki vitu vingi. Na katika agano Mungu akishaweka agano na wewe kwamba amekumilikisha au amekupa,ishi kwa agano hilo,



Kulikuwa na wazee ambao waliamua kumfuata Joshua na kumwambia wametoka mbali zaidi ya nchi ile ya ahadi wanayoiendea wana wa Israeli na nguo zao zilikuwa zimechakaa na viatu vyao pia ndipo Joshua akawaapia


kunawatu wanaweka maagano ya kimizimu na mauti imeandikwa  Isaya 28: 15 “Kwa sababu mmesema, Tumefanya agano na mauti, tumepatana na kuzimu; pigo lifurikalo litakapopita, halitatufikia sisi; kwa maana tumefanya maneno ya uongo kuwa kimbilio letu,


1Samweli 23: 17 “Akamwambia, Usiogope, kwa maana mkono wa Sauli, babangu, hautakupata; na wewe utakuwa mfalme juu ya Israeli; na mimi nitakuwa wa pili wako; ndivyo ajuavyo hata Sauli, babangu. Na hao wawili wakafanya agano mbele za Bwana; Daudi naye akakaa huko Horeshi, na Yonathani akaenda nyumbani kwake.”

Yoshua 2: 1 “Yoshua, mwana wa Nuni, akawatuma watu wawili kutoka Shitimu kwa siri, ili kupeleleza, akawaambia, Enendeni mkaitazame nchi hii, na Yeriko. Wakaenda wakafika nyumbani kwa kahaba mmoja jina lake aliitwa Rahabu, wakalala huko. Mfalme wa Yeriko akaambiwa, kusema, Tazama, watu wawili wa wana wa Israeli wameingia humu leo usiku, ili kuipeleleza nchi. Mfalme wa Yeriko akatuma watu kwa Rahabu, akasema, Watoe watu wale waliokuja kwako, walioingia ndani ya nyumba yako, maana wamekuja ili kuipeleleza nchi.

 Yule mwanamke akawatwaa wale watu wawili, akawaficha, akasema, Naam, wale watu walikuja kwangu, lakini sikujua walikotoka; ikawa kama wakati wa kufungwa lango la mji, kulipokuwa giza, watu wale wakatoka, wala sijui walikokwenda; wafuateni upesi, maana mtawapata. Lakini yeye alikuwa amewapandisha darini, akawaficha kwa mabua ya kitani, aliyokuwa ameyatandika juu ya dari. Basi hao watu wakawafuata kwa njia iendayo Yordani mpaka vivukoni;

na mara wale watu waliowafuatia walipokwisha kutoka, wakalifunga lango. Tena kabla hawajalala akawaendea juu darini, akawaambia wale wanaume, Mimi najua ya kuwa Bwana amewapa ninyi nchi hii, na ya kuwa hofu imetuangukia mbele yenu, na ya kuwa wenyeji wote wa nchi wanayeyuka mbele yenu.

 Maana tumesikia jinsi Bwana alivyo yakausha maji ya bahari ya Shamu mbele yenu, hapo mlipotoka Misri, tena mambo hayo mliyowatendea wafalme wawili wa Waamori waliokuwa huko ng'ambo ya Yordani, yaani, Sihoni na Ogu, mliowaangamiza kabisa. Na mara tuliposikia hayo mioyo yetu iliyeyuka, wala haukusalia ujasiri wo wote katika mtu awaye yote, kwa sababu yenu; kwa kuwa Bwana, Mungu wenu, yeye ndiye Mungu, katika mbingu juu na katika nchi chini. Basi sasa, nawasihi, niapieni kwa Bwana, kwa kuwa nimewatendea hisani, ya kwamba ninyi nanyi mtaitendea ihisani nyumba ya baba yangu; tena nipeni alama ya uaminifu; ya kwamba mtawaponya hai baba yangu na mama yangu, na ndugu zangu wanaume na wanawake, na vitu vyote walivyo navyo, na kutuokoa roho zetu na kufa. Wale wanaume wakamwambia, Uhai wetu badala ya uhai wenu, ikiwa hamwitangazi habari ya shughuli yetu hii; kisha itakuwa, wakati Bwana atakapotupa nchi hii, tutakutendea kwa ihisani na uaminifu. Ndipo akawashusha kwa kamba dirishani, maana nyumba yake ilikuwa katika ukuta wa mji; naye alikaa ukutani.”

Agano lina nguvu kuliko jambo la aina yeyote japo watu wengi wanadharahu maagano waliyoyaweka sehemu Mbali mbali yapo maagano ya uchumba, biashara, kazi uganga,


  • AINA ZA MAAGANO

Maagano ya kiroho –sour tag yanafanyika rohoni, yanaitwa nadhiri

Maagano ya kimwili-yanafanyika mwilini,kwa kuchanjana chale za makubaliano au kupeana vitu flani,


Ufafanuzi wa haya maagano mawili, jampo kila agano linashahidi,mtu,sadaka,

Agano la Rohoni linadhibitishwa na maneno tu,

Agano hili linafanyika sana mahali mbali mbali katika madhabahu zinazojulikana au zisizojulikana,.
Mfano mfano wa kwanza sababu zinazowafanya watu kujenga maagano

Kutaka njia fupi ya mafanikio mwisho ni matatizo

Mashindani ya kimaisha kuwa Kama flani

Kutomtumaini Mungu katika maisha yako

Inchi au Familia au ukoo unaotokea kama ni wa maagano

Kumkataa Mungu kunasababisha kuingia katika maagano

Kuingizwa katika maagano bila kujuwa

Kutumika na madhabahu usiyojuwa agano lake

Kushikamana sana na mtu wa maagano ya mapepo

 

 

mtu anapokwenda kwa wachawi kutafuta dawa ya kumshugulikia mwenzake,au amnase,au asikilizwe na bosi wake kazini,au apande cheo,huwa wanakubaliana masharti flani,ya mdomo nenda kafanye hivi na vile,utafanikiwa,

Mfano wa pili Nanma wazazi wanavyowaingiza watoto wao katika maagano ya siyowahusu,

Kuna mtu anakwenda kumtambulisha mtoto mchanga kwao wanakaribishwa kabla hawajafika katika mji hawaruhusiwi kuingia hadi yafanyike matambiko ya maneno flani flani, mwisho mtoto anabebwa kupelekwa katika makaburi ya babu na bibi wanatamka maneno ya kimaagano,

Mfano wa tatu Namna agano linavyoweza kujengwa kwa maneno

 waganga wa kienyeji pale wanapowapa Huduma ya chale za mwilini huwa wanatamka maneno flani wakati kazi ya chale tatu au mbili mbili zinaendelea lile ni agano linajengwa juu ya mwili wa huyo mtu aliyekubali hilo agano yale maneno japo yanatamkwa pole pole au kwa nguvu mapepo au mashetani huyasikia na kuyashikilia kizazi kwa  kizazi.hiyo ndiyo sababu kubwa katika familia inakuwa kama urithi kila mmoja ni mtaalamu wa hayo mauchawi kwa nini maagano waliyoyakubali wazazi,

Mfano wane namna Agano linavyoweza kuhama na kufika kwa watoto

wewe ni mzazi umechanjwa chale kila mahali kwa rithaha yako mwenyewe na hiyo ni madhabahu uliyoijenga kwa siri wewe mwenyewe ila mtakaposhiriki na mmeo,kwakua ni mwili mmoja tayari mmeshiriki agano,mtoto akizaliwa tayari yopo katika agamo moja kwa moja,bila yeye kujuwa ndipo unakuta magonjwa ya kimapepo yaliyokuwa yanakusumbuwa wewe yanahamia kwa watoto ili agano la mapepo lizidi kuimarika,
imeandikwa Mithali 6: 2 “Basi umetegwa kwa maneno ya kinywa chako, Umekamatwa kwa maneno ya kinywa chako.”

Agano la kimwili linaweza kusimamiwa na mafuta,unga,maji,au damu,
Mambo ya walawi 17: 11 “Kwa kuwa uhai wa mwili u katika hiyo damu; nami nimewapa ninyi hiyo damu juu ya madhabahu, ili kufanya upatanisho kwa ajili ya nafsi zenu; kwani ni hiyo damu ifanyayo upatanisho kwa sababu ya nafsi.14 Kwa maana kuliko huo uhai wa mnyama, hiyo damu yake ni moja na uhai wake; kwa hiyo naliwaambia wana wa Israeli, Msile damu ya mnyama wa aina yo yote; kwa kuwa uhai wa wanyama wote ni katika hiyo damu yake; atakayeila awaye yote atakatiliwa mbali.”

Kumbe uhai wa mwili upo katika damu, hivyo agano kubwa la mtu liko katika damu. Mtu akichukua damu yako anaumiliki uhai wako na mifupa yako, amechukua misuli yako amechukua kila kitu kwasababu uhai umo katika hiyo damu.

Ndani ya damu kunavitu vingi vichache ninavitaja hapa.

  • Kuna tabia ya mtu mhusika
  • Ndani ya damu kuna kumbukumbu halisi ya mtu
  • Ndani ya damu kuna sauti halisi ya muhusika
  • Ndani ya damu kuna uhai ambayo ndiyo maisha halisi
  • Ndani ya damu kuna utendaji halisi

 

Sasa unapoiacha damu kwa wachawi waganga wa kienyeji umejiacha wewe mwenyewe uko kule akikuhitaji muda wowote anauwezo wa kukuita na ukaenda, kwa maana kizibiti kinachohalalisha wewe kuitwa na kwenda bila ubishi ni ile damu yaki,

Mfano utasikia mtu anasema ukishakutana na mtu kimwili mapenzi hayafaga watarudia tena sababu ni hizi damu wazizozionganisha kwa njia ya mapenzi, hivyo hata kama wataoa na kuolewa bado nay ale masalia yamo na yanahaki katika ulimwengu wa kiroho, kwa ile damu, wanandoa kuwa makini chunguza ndani ya ndoa yako mpo wangapi?

Maagano ya wazazi,
Wewe unaweza ukawa unahisi umelogwa leo kumbe ni ile damu ambayo wewe au baba yako aliiacha kwa mganga wa kienyeji inatumika kukutesa namna hiyo.
Kuokoka hakuzuwi wewe kuteseka kwasababu hili ni agano ni makubaliano ni kama mkataba flani,unatakiwa kuufuta kwa maelekezo maalumu na kwa hatua kwa hatua kufuta hilo agano

Unaweza ukawa umeokoka lakini shida bado zinakuandama kila siku hii ni kwasababu  rohoni uko huru  kama ulivyomkiri kristo lakini mwilini  kwa sababu ya agano shetani anabaki na uhalali wa kukuonea  sababu anaimiliki damu yako uliyoiruhusu wewe mwenyewe,

Mwanzo 9: 4 “Bali nyama pamoja na uhai, yaani, damu yake, msile.”

Damu ni uhai na kitu kilicho na uhai kina tabia na inasauti na inaweza kutembea na mtu.
Damu haina mdomo ila inaongea,
Mwanzo 4: 10 “Akasema, Umefanya nini? Sauti ya damu ya ndugu yako inanililia kutoka katika ardhi.”

kama huitajiki tamko linaagizwa afee ndio sasa mashetani wanakuja kukaa kwako kuanza kazi ya kukusumbuwa ili kutafuta sababu,au chanzo kitakachoonekana ndicho kimeua, kumbe ni yale mapepo,

 damu ikizungumza asiolewe!asiolewe! Mashetani yanakuja kukaa kwenye sura yako unakuwa unatisha, damu inapozungumza talaka! Talaka! talaka mashetani yanakuja kwenye ndoa yako na kuvunja.

sisi tumechanguliwa na Yesu kristo Kwa Damu ya Yesu, na inanena mema kila saa na kila siku,

Isaya 53: 5 “Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.”

.
Mwanzo 9: 11 “Na agano langu nitalithibitisha nanyi; wala kila chenye mwili hakitafutwa tena kwa maji ya gharika; wala hakutakuwa tena gharika, baada ya hayo, kuiharibu nchi Mungu akasema, Hii ndiyo ishara ya agano nifanyalo kati yangu na ninyi, na kila kiumbe hai kilichoko pamoja nanyi, kwa vizazi vyote hata
milele;”


ISHARA YA MTU ANAYETEMBEA NA MAAGANO

Agano la kishetani linasimamiwa mapepo Kama yalivyo elekezwa,

Agano la Mungu linasimamiwa na Roho mtakatifu na malaika wa Mungu


MTU ALIYECHANJWA CHALE MWILINI
Ndio maana ukienda kwa mganga wa kienyeji anakuwekea chale kama ishara ya maagano yenu na mashetani yatakapoziona zile ishara yanakumbuka ule hilo agano. Kunasiri kubwa sana iliyojificha katika chale hebu muulize aliyekuchanja kama atakuambia sababu,

MTU ANAYETEMBEA AMEVAA MAIRIZI MWILINI
Hirizi ni alama inayoonyesha uhalali wa mtu aliyefanya agano flani hivyo hata mapepo yakiona hayo mairizi basi yajuwe hapo kuna maagano,


KUVAA PETE ZISIZO ELEWEKA MKONONI SHINGONI,PUANI,MGUUNI POPOTE SI KWA UREMBO BALI KWA MAAGANO YA KISIMATI
Huo ni utambulisho kwamba wewe ni mali ya wahusika,


KUCHORA MATATOO MWILINI KWA INA,AU PINI,AU STIKA

Hii mtu anapofanya hivi anatambulisha Nguvu au roho iliyo ndani yake


UNYOWAJI WA MASHARTI MSIBANI,
Unaendeleza mila au desturi flani kwaajili ya kukubaliana na tukio hili hivyo ni kama unasema kama ulivyoondoka wewe tunaungana na wewe na sisi tutakufa hivyo hivyo,

KUTUNZA NYELE ZA MTOTO MCHANGA AU  KITOVU
Hii ni kwaajili ya kuendeleza roho ya ukoo flani kudumisha mahusiano na kuonganishwa na ndugu walio kufa,

KUOGESHWA NA MADAWA YA KICHAWI,

Hii ni kukabithishwa mzima mzima kwa uhalali kabisa, hadi elemu,mali,na vyote ulivyo navyo,

KWENDA KATIKA IBADA ZA KIMIZIMU-40
Hii ni kuimarisha nguvu ya madhabahu ya mateso iendelee kudumu kizazi na kizazi unawasajili watoto na wajukuu,


Hitimisho

Kikubwa ni kufuta maagano uliyoyaweka au yaliyowekwa na mabibi mababu au wewe mwenyewe katika maisha yako ya kazi  wachumba,ndoa,biashara,katika viwanja au juu ya watoto waiolewe au kuowa,juu ya uasi au uharibifu wizi,ukahaba,uasherati,agano la mikoba ya kichawi,agano la kuitumikia mizimu,agano la majina, agano la Huduma ya mtoto kumtumikia Mungu, agano la madhabahu flani, agano la siri,agano la uwongo katika kazi,uchumba,ndoa,biashara,kazini,


Maombi maalumu ya kufuta maagano yanatakiwa ************

Followers